Hapana,
Mara baada ya Mzee Karume kuuwawa, nafasi yake ingechukulkiw na Mzee Thabiti Kombo kama ilikuwa ni swala la seniority, ila Mzee Kombo alikuwa na imani sana na utaifa ya Jamhuri ya Muungani na alijua kuwa nafasi ile ilitakiwa mtu aliyesoma kukaribiana na Nyerere kuliko yeye. Kwa hiyo akashauri nafasi hiyo apewe Jumbe, na kweli Jumbe aliifanya vizuri sana akiwa analenga kwenye utaifa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania badala ya Zanzibar. Kama ulisikia ile hotuba ya Jumbe ya mwaka 1975 wakati wa uteuzi wa mgombea wa uraisi wa Tanzania wakati huo utakubaliana nami kuwa alikuwa na utaifa zaidi ya uzanzibari wakati huo. Jumbe aliipenda na aliifanya kazi yake ua umakamu wa Rais kwa ufanisi sana huenda kuliko makamu mweingine yeyote wa Rais katika historia ya Taifa hili. Wakati wa vita Uganda, Jumbe aliidhinisha hela kutoka akiba ya serikali ya mapinduzi ya zanzibar, kwa ajili ya kununulia BM40 ambazo hatukuwa nazo wakati ule na Nyerere hakuwa na hela za kupata silaha hizo mara moja katika muda mfupi ule. Maamuzi yote yaliyokuwa yakifanyika na kuigusa Zanzibar wakati huo, yalikuwa hayatimii bila ridhaa ya Mzee Jumbe na Mzee Kombo. Mzee Jumbe alighafilika kidogo tu kutokana na kuchukia popularity ya Sokoine kufuatia vita ya uhujumu uchumi ya mwaka 1983, na ikawa ndiyo mporomoko wake wa moja kwa moja kisiasa.
Kichuguu,
Uliyazungumza mengi ni ukweli ila kuna tatizo moja umelisahau kulizungumza au kulisema. Nyerere alikuwa na influence na power mpaka visiwani na aliyekuwa na uwezo wa kupambana nae alikuwa ni Marehemu Karume peke yake. Alipofariki ndipo Nyerere alikuja akabadilisha baadhi ya vipengele wakati wa kuandika constitution ya Tanzania kuimeza Zanzibar. Haya yamezungumzwa na wanahistoria wengi nchini na nje ya nchi. Sasa unafikiri Thabit Kombo au Mzee Aboud Jumbe walikuwa na uwezo wa kumpinga maamuzi yake. Pesa za vita zilitoka lakini kwa shingo upande kwani zilikuwa ziende kufinance shughuli za maendeleo visiwani badala yake zikaenda kununua vifaa vya kijeshi. Hili liliwakera wengi ndio sababu ya rebellion by mzee Jumbe kutaka Zanzibar iwe inatambulika kama nchi ili iwe na uhuru wa kufanya maamuzi yake yenyewe pasina kuingiliwa au kulazimishwa na serikali ya muungano.