ommy15
JF-Expert Member
- Jan 23, 2011
- 670
- 1,012
Hela anapata mikoba(kondakta) mimi ilibidi niwe kimakakati sana. Ikifika saa 4 natoa buku 5 naweka kwenye kamfuko ka jeans kale kadogo. Saa 10 naweka tano tena. So jioni kwenye mgao wa posho nakuwa nmemtangulia dereva kwa 10,000. Nakama unavyojua kwenye mgao kondakta anapata kidogo na dereva anapata hela nyingi zaidi. Yaani kama baada ya kujaza mafuta na kutoa malengo ya boss mkabakiwa na 50,000 inamaana dereva 30,000 na kondakta 20.Kazi ya daladala sitaki hata kuikumbuka kwakeli, na kushuka na 30 au 40 sio jambo la kushangaa ila ishu niza msimu, mara nyingi ni yale majira ya mwisho wa mwezi, ila kuanzia hapo niaumivu, na bahati mbaya nyingine sikua kondakta pengine ndio maana nilipata maumivu makubwa
Siku nzuri ilikuwa mkipata watu wa kukodisha kwenye harusi mnapata hela nyingi sana coz mnatumia mafuta kidogo,mnalipwa kibunda,mnapata msosi wa bure na ndio mnapata muda wa kulala sana.
Kipindi hicho ndio nilielewa thamani ya usingiz yaaani. Nalijizoelea mkoani kwetu kuamka saa 1 au 2 sikuwa kuelewa kwanini binadamu anaamka saa 10 alfajiri. Ilikuwa nikipata nafasi ya kulala aiseee nilichagua kulala kuliko kula