maramia
JF-Expert Member
- Jul 17, 2015
- 2,030
- 1,344
Uchaguzi umekwisha, walioshinda wameshinda na walioshindwa wameshindwa, ninachojaribu kufanya sasa ni kuonyesha uwiano wa kile kilichotarajiwa na wengi kabla ya uchaguzi na matokeo ya matarajio hayo baada ya uchaguzi.
Kusema kweli, nikiwa mwanachama wa CCM tangu enzi za TANU, ni katika uchaguzi wa mwaka huu pekee kati ya chaguzi zote zilizowahi kufanywa nilikuwa na wasi wasi wa CCM kushindwa ama kutoa matokeo ambayo yangekaribiana sana na vyama vya upinzani.
Mtazamo wangu huu ulitokana na udhaifu mkubwa ulioonyeshwa na serikali ya Rais Kikwete katika vipindi vyote viwili vya utawala wake alivyokaa madarakani.
Watanzania wamenishangaza sana kiasi ninashindwa kuelewa ni vigezo gani hasa tunavyotumia kukipa kura chama cha siasa wakati wa uchaguzi.
Sikutegemea, kwa madudu yaliyokuwa yamefanywa na serikali ya Kikwete kama CCM ingeweza kupata ushindi huu wa 58% dhidi ya 40%.
Ebu jaribu kurejea kashfa kama za EPA, Richmond, Escrow, Kuzuia Katiba mpya, utoroshaji wanyama wetu kwenda nje, mateso, unyanyasaji na mauaji ya kinyama ya raia kutoka vyombo vya dola (Ulimboka, Mwangosi n.k), dhuruma na utesaji wa raia wakati wa oparesheni Tokomeza na mengine mengi lakini eti tayari watanzania wameishayasahau yote hayo wakaamua kuirundikia CCM kura.
Safari hii wapinzani walikuwa na turufu nzuri sana ya kuitumia dhidi ya CCM lakini kwa tamaa za kipumbavu za viongozi wao hawakukumbuka hayo, wote wakageuzia fahamu, macho na akili zao kwa akina Lowassa, Sumaye na Kingunge ambao hawakuwa na mamlaka yoyote ndani ya Ukawa, wakaachiwa majukwaa ya kampeni, matokeo yake CCM ikajikuta imeachiwa mwanya wa kupenya hadi kwenye mstari wa ushindi bila kikwazo.
Nina imani Magufuli akiutumia vizuri mwanya huu uliopatikana, ambao sasa wapinzani hawana agenda madhubuti watakayoisimamia mbele ya wananchi, akafanya vizuri ktk miaka hii mitano ya kwanza ana uwezo wa kuisambaratisha kabisa Ukawa.
Kusema kweli, nikiwa mwanachama wa CCM tangu enzi za TANU, ni katika uchaguzi wa mwaka huu pekee kati ya chaguzi zote zilizowahi kufanywa nilikuwa na wasi wasi wa CCM kushindwa ama kutoa matokeo ambayo yangekaribiana sana na vyama vya upinzani.
Mtazamo wangu huu ulitokana na udhaifu mkubwa ulioonyeshwa na serikali ya Rais Kikwete katika vipindi vyote viwili vya utawala wake alivyokaa madarakani.
Watanzania wamenishangaza sana kiasi ninashindwa kuelewa ni vigezo gani hasa tunavyotumia kukipa kura chama cha siasa wakati wa uchaguzi.
Sikutegemea, kwa madudu yaliyokuwa yamefanywa na serikali ya Kikwete kama CCM ingeweza kupata ushindi huu wa 58% dhidi ya 40%.
Ebu jaribu kurejea kashfa kama za EPA, Richmond, Escrow, Kuzuia Katiba mpya, utoroshaji wanyama wetu kwenda nje, mateso, unyanyasaji na mauaji ya kinyama ya raia kutoka vyombo vya dola (Ulimboka, Mwangosi n.k), dhuruma na utesaji wa raia wakati wa oparesheni Tokomeza na mengine mengi lakini eti tayari watanzania wameishayasahau yote hayo wakaamua kuirundikia CCM kura.
Safari hii wapinzani walikuwa na turufu nzuri sana ya kuitumia dhidi ya CCM lakini kwa tamaa za kipumbavu za viongozi wao hawakukumbuka hayo, wote wakageuzia fahamu, macho na akili zao kwa akina Lowassa, Sumaye na Kingunge ambao hawakuwa na mamlaka yoyote ndani ya Ukawa, wakaachiwa majukwaa ya kampeni, matokeo yake CCM ikajikuta imeachiwa mwanya wa kupenya hadi kwenye mstari wa ushindi bila kikwazo.
Nina imani Magufuli akiutumia vizuri mwanya huu uliopatikana, ambao sasa wapinzani hawana agenda madhubuti watakayoisimamia mbele ya wananchi, akafanya vizuri ktk miaka hii mitano ya kwanza ana uwezo wa kuisambaratisha kabisa Ukawa.