Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,789
- 218,427
Kwa Mujibu wa Wakili wa Dkt. Slaa , Dickson Matata ni kwamba, Dkt. Slaa alikamatwa kwa tuhuma za uchochezi na hata kwenye hati ya mashitaka ya Polisi iliandikwa hivyo. Sasa baada ya kupelekwa nyumbani kwake kupekuliwa na kurejeshwa kituoni , Polisi wakamtaka aandike maelezo kuhusu uchochezi wake. Dkt. Slaa alikataa kuandika maelezo hayo na kuahidi kutoa maelezo yake mbele ya Mahakama (sheria za Tanzania zinaruhusu jambo hili).
Kosa la Uchochezi linadhaminika, inadaiwa baada ya wakili wake kuanza utaratibu wa kushughulikia dhaman Mkuu wa kituo cha polisi Oysterbay akafanya mawasiliano na Polisi Makao Makuu. Inadaiwa baada ya mawasiliano hayo ndipo ikaamriwa Kuliko apewe dhamani ni heri abadilishiwe mashtaka na kupewa kosa la Uhaini ambalo halina dhamana (hapa bila shaka Polisi hawakujipanga) basi ile hati ya Uchochezi ikachanwa na kuandikwa mpya ya Uhaini ambayo haina dhamana ili kumkomesha.