Ni forex tena, zamu hii pokeeni ukweli huu..

Nchi Kavu

JF-Expert Member
Sep 11, 2010
4,271
2,401
Kuna usemi mpya unasema “Heri walimkavu kuliko walimwengu.” Penye walimwengu pana pana mengi. Nasema hivi kwa nini. Kiuhalisia tuliletewa hii fursa na kijana mwenzetu ambaye naweza sema si mhangaikaji tu, bali anajua anachokihangaikia. Si mwingine ni Sirjeff, almaarufu kama Ontario. Sina sababu ya kurudia kile alichowahi kuandika kuhusu namna gani aliweza kuileta na kuitangaza forex hapa nchini.

Kabla sijaenda sana napenda kutangaza maslahi kuwa name ni mmojawapo wa wanufaika wa fursa hii ya forex. Tangu batch ya kwanza kabisa pale mwaka jana mwezi wa tisa hadi leo miezi sita naendelea na forex huku nikiendelea kujifunza mengi kila siku maana forex ni forest kweli. Baada tu ya ujio wa forex nchini ni mengi yamefanyika ikiwa ni pamoja na kusemwa, kuandikwa, na kutendwa.

Kwa kipindi chote hiki cha kuandikwa na kuzungumziwa kwa forex kwa mema na mabaya, nimewahi kuchangia tu mara chache. Aghalabu huwa nasoma kila kinachoandikwa. Walianza kuandika kuhusu forex kuwa ni utapeli. Ni DECI mpya. Ni pyramid scheme, na kwamba siku itafika watu wataficha nyuso zao na kwa kuwa yaliyosemwa yametimia. Haitokaa itokee. Bado wako watu wengi sana wanaamini kuwa forex ni kama ile michezo ya kubahatisha. Well, ukiamua kwenda kwa staili hiyo haujakatazwa. Wapo pia wanaoendelea kuamini kuwa forex ni DECI. Ni ponzi scheme. Well, wako wajanja wanaoitumia forex kuendesha hizo DECI. Hivyo forex ni kama kisu ulichonunulia kwa ajili ya matumizi ya nyumbani. Sasa akaja mtu akakitumia kumuumiza mwenzie haimaanishi kisu kibaya bali matumizi hayakuwa sahihi, hivyo aliefanya matumizi yasiyo sahihi ndiye mwenye matatizo.

Baada ya baadhi ya wale wadau wa mwanzo kupata elimu ya forex (basic knowledge) kupitia kampuni ya The Million Team (TMT) chini ya JP Markets ambaye ndiye broker tunayemtumia hadi sasa, kelele zilianza. Ukweli ni kuwa kila kitu kipya kina changamoto zake. Yawezekana malalamiko yao yalikuwa yana ukweli ila wakakosa staha na uvumilivu katika kuwasilisha na kuona wanachokitaka kinachelewa.

Yaani u introduce forex mwezi wa tisa, na baada ya miezi mitano kila kitu kiwe kama wateja wanavyotaka? Ni ngumu. Wako waliokuja humu jukwaani kukiri kuwa hakika forex ni mkombozi. Wanatengeneza pesa ambayo walikuwa hawajafikiri kutengeneza hapo awali. Kwamba forex sio imekuja wakati mwafaka, bali imechelewa sana. Forex haikuchelewa. Kutokana na ukwasi uliopo kwenye hii biashara, wako watu hapa nchini waliijua mapema na wakawa wanafanya yao kimya kimya bila kutaka wengi wajue haya. Wapo watu binafsi pamoja na taasisi za kifedha. Sasa kati ya hao ambao wameona maslahi yao yanaingiliwa na TMT basi rafu nazo zikaanza.

Sasa turudi kwa wale wafaidika wa forex ya TMT. Ni hulka ya binadamu kutaka zaidi ya kiasi, na kuwa mdadisi na kutaka kujiongeza. Sasa baada ya hawa wenzetu kuona kasi wanayoitaka na mambo wanayoyataka hayaji kwa kasi waliyojipangia, wakaanza kunena mabaya kuhusu TMT pamoja na broker husika.

Kiukweli mabaya mengi yameandikwa kuhusu TMT pamoja na JP Markets. Kwa mtu asiyependa kutafakari atasema basi tena, pale hamna kitu. Lakini sisi ambao bado tupo tunajua nini tunataka, nini tunapata, na tufanye nini panapotokea changamoto kadhaa. Matatizo yalianzia na broker, kisha TMT. Mbaya zaidi ikashuka hadi kwa CEO wa TMT – Ontario. Yote hii ikiwa ni harakati za kuvuruga na kuona jamaa wanakufa kibiashara na kupotea. Si rahisi hivyo. Nitaeleza kwa nini.

Broker

Suala la broker ni suala tete sana, watu hawajui tu. Wengi wa brokers tunaowatumia, nje ya huyu ambaye wawakilishi wake wapo hapa nchini, tunafanya nao miamala kwa ile tunaita mutual trust. Lolote laweza kutokea na hela yako ikapotelea huko nje. Kwenye forex kuna brokers wengi sana! Inatakiwa upembuzi wa kutosha kujua unafanya biashara yako na broker wa aina gani. Wengi wamepoteza hela zao huko nje bila kujua wanafanya biashara na broker wa aina gani. Wengi wa waliokuwa wanakuja hapa jukwaani kuiponda TMT, CEO wake, pamoja na JP Markets walikuwa/wanatoa mbadala wa brokers wao ambao kwa namna moja ama nyingine wana maslahi nao.

Hatukatai kuna ushindani. Waswahili wanasema usiache mbachao kwa msala upitao. Tena wakasema usitukane mamba ungali hujavuka mto. Singependa sana kuwazungumzia brokers hao ambao wamekuwa sababu ya huyu waliyekuwa naye mwanzo kunenewa mabaya. TMT walituletea JP Markets. Tunawajua TMT na ofisi zao tunazijua. Kwa tatizo lolote ofisi zao ziko wazi, hivyo hakuna namna yoyote unaweza kufanya miamala yako na broker akashindwa kukulipa halali yako wakati TMT tuko nao.

Tuko na JP kwa kuwa waliingia makubaliano na TMT, na kwa lolote wako tayari kushughulikia. Yako mambo kadhaa ambayo kati ya hayo ndiyo yalipelekea wadau kufitini na kuja huku na kuanza kumwaga ugali na mboga. Mambo waliyoona kwao ni kero sasa yapo ambayo yameshafanyiwa kazi, ikiwa ni pamoja na spreads kupunguzwa. Kama si mdau wa forex itakusumbua kujua baadhi ya masuala. Wapo ambao waliona urahisi wa kufanya miamala yao kwa njia ya mobile money kama mpesa, tigopesa na airtel money kupitia kwa hao broker wengine. Uzuri ni kuwa wakati sio mwingi huduma hiyo itaanza kufanya kazi kupitia JP Markets. Hata hivyo kwa sasa ukihitaji kuwithdraw cash yako toka JP Markets inakuchukua saa kadhaa tu.

TMT

The Million Team ambao ndio wanaoiwakilisha JP Markets uzuri tunawajua. Tunakutana nao na kuwasiliana nao wakati wowote. Wao kama kampuni wana wajibu wa kuhakikisha kuwa sie wateja wao tunapata kile tunachohitaji, ikiwa ni pamoja na urahisi wa huduma ya uwekaji na utoaji pesa toka kwa broker. Kingine kupata elimu ya forex na mafunzo endelevu hadi hapo mtu atakapoona anaweza kujisimamia.

Kama kuna tatizo limetokea, suluhu si kutoka na kwenda pembeni kutukana na kuleta ujuaji. Mtu mzima, tena mwanaume unakuja kupandisha uzi humu kuwasema watu wengine, kisa hujulikani, ni uzezeta tu. Mtu anakuvusha mto kwa kukubeba mgongoni unafika ng’ambo unasema, ‘limgongo lake linanuka…!’ Si watu hao. Zikitokea kasoro tunapeana ukweli humo humo kwenye grupu zetu na kwa uwazi na mwisho wa siku zile kasoro zinaondoka.

Yapo mengi tuliyowashauri TMT kama kampuni. Nao kwa uchanga wao wanaendelea kujifunza mengi. Nao siku na wakati ukifika kulingana na malengo yao wamepanga kuwa broker hapa nchini. Kama wamekuwa wa kwanza kutuletea elimu hii kwa uwazi, tuwatakie heri pia wafanikiwe kuwa broker wa forex hapa nchini ili hii huduma iwe rahisi zaidi nay a uhakika zaidi na karibu zaidi.

HITIMISHO

Forex ipo na itaendelea kuwepo. Kama hatuwezi nasi kuwa hao broker, sembuse kuleta elimu hii kwa wengi na kwa uwazi, tuwaunge TMT mkono katika kufanikisha haya. Tuone kuwa forex inakuwa sehemu ya ajira kwa vijana wengi ambao ajira imekuwa changamoto. La msingi ambalo TMT wakishirikiana na wadau wengine wanapaswa kufanya ni kutoa elimu sahihi kuhusu forex. Kwamba forex sio a get rich quick scheme. Kwamba forex sio bahati na sibu. Kwamba forex ni uwekezaji kama uwekezaji mwingine. Forex inahitaji muda kujifunza kama zilivyo taaluma zingine.

Tumpe moyo kijana mwenzetu, mtanzania mwenzetu Sirjeff ambaye ameiona fursa ilipo akaona sio vibaya kuwapa na wengine fursa hii. Tukiweka nidhamu katika kuifanya forex kulingana na misingi na taratibu zetu, basi lengo na kusudi la mwenzetu huyu litatimia – kuwezesha wengi kujiajiri. Lakini tukianza pupa na kutaka kutajirika na kuwa na ulafi na mwisho kujenga chuki na kuchafuana, forex itaonekana ni blah blah (kitu ambacho si sahihi kabisa) na mwisho lengo la mleta fursa halitatimia.

Tena wahenga wakaendelea, usidharau nazi. Embe tunda la msimu. Uzuri itafika siku na wale wote waliokuwa na nia mbaya na hawa jamaa (TMT) watarudi kuwa sehemu ya TMT. Wako watakaorudi kimya kimya na wako watakaokiri hawakuwa sahihi kutupa jongoo na mti wake. Hivyo basi natoa wito kwa wale ambao kwa namna moja au nyingine walikatishwa tamaa na hoja nyingi mfu zilizoletwa humu jukwaani waone tena sababu ya kujitafakati tena na kuichangamkia fursa hii. Kwa wale ambao hawaijui TMT na mahali ilipo, ni Oyaterbay karibu na kituo cha mbuyuni barabara ya Ali Hassani Mwinyi. Jingo linaitwa Jangid Plaza.
 
Ni kweli yanaweza yakawepo makosa aidha kwa TMT au kwa JP lakini haiondoi fursa ya kuwakosoa na ikibidi kuwashauri nini cha kufanya ili waboreshe huduma tupate kile tunachostahili.
Hili TMT walichukue kama lilivyo, wawe na mtu hasa wakupokea na kushughulikia mapendekezo au malalamiko toka kwa wadau walio jenga imani kwa TMT tangu awali cc: ONTARIO
Sasa hao broker wa huko London, Cyprus, n.k. wakizingua unaanza wapi kufuatilia? Utafuatilia ndio ila unaweza kupoteza muda na gharama pia. Sisemi ni wabaya maana tunafanya nao biashara pia, ila sio reliable sana.
Umetumia kigezo kipi kusema kuwa sio reliable?
Kama walikuwepo basi walikuwa kisirisiri na walikuwa wanakula kisirisiri na hawakutaka wengine wafaidi. Sasa walipoweka mambo hadharani, wale waliokuwa wanafaidi kimya kimya wakaona kuwa maslahi yao yamevamiwa. Pengine ndio hao wanaoongoza kwa kuichafua TMT huku wakipigia chepuo broker wengine wa nje.
Kuna ukweli hapa.
 
Hili TMT walichukue kama lilivyo, wawe na mtu hasa wakupokea na kushughulikia mapendekezo au malalamiko toka kwa wadau walio jenga imani kwa TMT tangu awali cc: ONTARIO
Umetumia kigezo kipi kusema kuwa sio reliable?

Kuna ukweli hapa.
Mwalimu RCT naamini bado tupo kwenye boti moja. Yapo mabadiliko kidogo yamefanyika hapo. Twende nayo haya
 
Umeandika kirefu lakini kuna mambo umeshindwa kuyajibu. Kifupi Umepayuka tu badala ya kujenga hoja au kujibu hoja.

Kwa mfano.
-Nini majibu yako dhidi ya shutuma moja moja kwa TMT?
-Changamoto za TMT ni zipi hizo hasa?
-Kwanini wadau waje TMT na sio kwingine?
-Forex ni biashara halali na Uwazi kwanini hizo kasoro za utapeli wa TMT uogope kujadiliwa humu na upange kujadiliwa kwenye magroup closed ya Whatsapp?

Binafsi nilidhani ulipaswa Kuja na Uzi kamili wa kujibu zile tuhuma nzito za utapeli wa TMT au Ungekwenda moja kwa moja kwenye ule uzi wa tuhuma dhidi ya TMT na kuja na majibu kamili na yakawa attached kwenye ule uzi.

Yote kwa yote, bado huwezi kuwajibia TMT kama wewe sio mfanyakazi wa TMT, maana baadhi ya tuhuma ni za ndani sana ambapo mteja wa TMT huwezi kuzijibu na ukaeleweka vyema.
 
Umeandika kirefu lakini kuna mambo umeshindwa kuyajibu. Kifupi Umepayuka tu badala ya kujenga hoja au kujibu hoja.

Kwa mfano.
-Nini majibu yako dhidi ya shutuma moja moja kwa TMT?
-Changamoto za TMT ni zipi hizo hasa?
-Kwanini wadau waje TMT na sio kwingine?
-Forex ni biashara halali na Uwazi kwanini hizo kasoro za utapeli wa TMT uogope kujadiliwa humu na upange kujadiliwa kwenye magroup closed ya Whatsapp?

Binafsi nilidhani ulipaswa Kuja na Uzi kamili wa kujibu zile tuhuma nzito za utapeli wa TMT au Ungekwenda moja kwa moja kwenye ule uzi wa tuhuma dhidi ya TMT na kuja na majibu kamili na yakawa attached kwenye ule uzi.

Yote kwa yote, bado huwezi kuwajibia TMT kama wewe sio mfanyakazi wa TMT, maana baadhi ya tuhuma ni za ndani sana ambapo mteja wa TMT huwezi kuzijibu na ukaeleweka vyema.
Kwa ufupi uelewe kuwa kazi kubwa ya TMT ni kuunganisha wateja wake na broker ambae ni JP Markets wa Afrika ya Kusini. kazi hii inajumuisha kutoa mafunzo juu ya forex pamoja na namna ya kufanya forex chini ya uangalizi wa mwalimu (mentor). wakati ukifika, huyu anayeelekezwa akiona amekomaa yuko huru kuondoka kwenda kujitegemea. Wanaitwa independent traders. Katika mchakato wote huo haiwezekani pakosekane kasoro za hapa na pale pamoja na changamoto ambazo kiuhalisia zinafanyiwa na zimeshafanyiwa kazi. Nazo ni pamoja na mwalimu. Walio ndani ya TMT ndio wanajua mchakato ukoje. sasa kama kuna mtu huko nje ana maelezo mengine ni yake.

Kadhalika jambo kubwa na ambalo bado linasababisha kila kitu kuonekana ndivyo sivyo ni kwamba watu wanaamini kuwa forex ni mgodi ambao unaokota tu madini bila kuchimba au kutumia nguvu ya ziada. Changamoto iko hapo kwamba TMT hawakuwa bayana sana katika hili. Baada ya kuongea nao sasa wameona uhalisia wa kuweka ukweli katika taarifa zao. Mwanzo tuliamini kuwa forex ni mteremko, na unachota tu. Kwa kadiri tulivyoendelea tunakutana na ukweli kuwa forex inahitaji ujuzi na wa muda wa kutosha ili kuweza kusimama na kuitwa kweli Trader.

Pia zipo tahadhari kila sehemu, pamoja na kutoka kwa mentor kuwa tumia Risk management kwenye trade zako. Pia unaambiwa Read more than you trade na bado ukakiuka unategemea nini? sasa mtu akipoteza hela yake kwa kuacha kufuata kanuni hizo unaweza kulaumu kweli? Bado nakubali kuwa mwalimu wa forex kwa tmt kuna tatizo na inabidi pawepo na namna, hata kuongeza nguvu ili hizi kelele zisiwepo. Hili mhusika analifanyia kazi. Mwanzo walisema jamaa si msikivu na mwenye kiburi. Watu hubadilika kwa kusemwa na kupewa ushauri pia. Hili ndio jambo kubwa.

Kiukweli hata kama kungekuwa na matatizo mengine mengi wala wadau wasingejihangaisha kuyajua, mradi tu akaunti zao na hela zao ziko salama na zinazaa, na wana uhakika wa kutoa hela pale wanapoona wanahitaji.

Kadhalika sidhani kama kuna uficho TMT. Kama upo ni ule wa kawaida wa siri za kampuni. Si kila jambo linaenda hadharani. Kama kuna mambo ambayo hayaendei sawa kwa mujibu wa sheria na kanuni sidhani kama jamaa wangeendelea kuwepo. Uficho walikuwa nao hao walioijua forex ila hawakuwa tayari kushiriki fursa hii na wenzao.

Suala kwa nini TMT na si wengine, ndio ambaoTMT waliingia mkataba na JP Markets. sasa wewe umeingia mkataba wa ndoa na mkeo halafu mkeo anaanza kuchepuka, na anakwambia anachepuka. Wewe utakuwa kiazi kiasi gani kumkubalia? Kihalali TMT wana haki ya kuona wateja wake wanamtumia broker ambaye wameingia naye mkataba. Huwezi ukawa unakula kwako kisha unaenda kujisaidia kwa jirani.

Kadhalika JP Markets kama nilivyosema awali ni broker aliye karibu. Japo kulikuwa na tuhuma za hapa na pale juu yake, imethibitika, na broker amethibitisha kuwa tuhuma hizo si za ukweli na biashara inaendelea kama kawaida. Ni wa uhakika kwa kuwa yuko jirani na wawakilishi wake (TMT) wako nasi kama nilivyosema.

Mwisho, haimaanishi kuwa jambo baya leo ni baya kesho. Kwenye biashara yoyote kuna fitna na wafitini na washindani. Inategemea unatumia mbinu gani kujitetea na kujihami
 
Anayeamini kuwa fx ni utapeli aendelee kuamini hivyo... Nimeatach screenshot ya nilichovuna asubuhi hii (115$= zaidi ya laki mbili).
Screenshot_2018-04-19-09-03-31-525_net.metaquotes.metatrader4.jpg
 
Umeandika sana, lakini niseme tu pamoja na kuandika sana huko haujajibu au kuelezeamambo muhimu. Ni maandishi mengi tu ila yasiyo na uhalisia na yako too gerenal.

Mfano kuna shutuma kua PIPS za JP markets zinampa yeye kwanza profit kabla ya mteja, yaani pale faida inapoanza kuingia basi inaingia kwanza kwa broker kisha ndio ziingie kwako, na inawezekana kabisa isifikie wewe kupata profit lakini Broker Jp market anakua ashadaka zake kupitia wewe, hili hujalizungumzia.

Pili kwenye Pips hizi hizi, zipo ambazo ziningia kwa TMT/Ontario na hapo mwanzo ilikua ni siri. Yaani ku trade ni trade mimi, lakini kwenye Pips zangu, ONTARIO anachukua na JP nae anachukua hapohapo, hili sijaona ukiliongelea katika uzi wako uliouandika mambo meeengiii. TMT walifanya hivi bila kututaarifu sisi members wao na hakipo kwenye makubaliano yetu sisi na wao, kitu ambacho ni sawa na wizi

Yule Msouth CRE kwa sasa ni chui na paka na JP market, yeye anadai kua swala la kukatwa Pips ndio ameligundua sasa ndio maana eti amemaindi kwanini Pips zetu zichukuliwe na JP. Ukweli ni kua hili swala alilijua kitambo tu maana tumeanza kulilalamikia toka kitambo. Habari tulizonazo ni kua CRE na ONTARIO wamegundua kua JP anawapiga panga kwenye commission zao za kuwatafutia vichwa ndio maana wamemaindi.

Wewe umeandika tu in general lakini kuna vitu vya kwenda in deep hukuandika
Kiufupi kuna mambo mengi huyajui kuhusu forex. Pia inainekana hauko na TMT. Kwanza ishu ya pips unazosema iko wazi. Vingine iite spreads. Ni tozo ambayo kila broker lazima achukue kabla ya wewe kuanza kupata faida yako, ndio maana kila unapoweka trade unakutana na manamba mekundu, baada ya broker kuchukua chake, na kama trade iko upande wako ndio utaona blue zinakuja. Hivyo usiongee usichojua.

Kuhusu Cre na JP Markets kuwa na uhasama si kweli. Wewe hauko TMT. Kila kitu kipo kwenye mstari kwa sasa japo kweli palitaka kutokea mtafaruku, ambao popote pale unaweza kutokea
 
Utapeli kwa kwenda mbele. Huna hoja za msingi wala hujatoa ufafanuzi wa shutuma zinazowakabili TMT. Achane utapeli nyie watu. Forex market haipo hivyo mnavyoiongelea bali mnajaribu kuwaibia watanzania wasioielewa. Haya mambo ni mapana mno, inahitaji mtu kuwa na idea ya International Finance, siyo nyie mnataka hata walio wakulima wawaelewe kwa maneno yenu matamu ya utapeli.
Brother, hapa jf sio padogo kuna watu wasomi wa kada mbalimbali na hii kitu wengi waliipinga sana lakini mkafanikiwa kuwashawishi baadhi ya watu na hatimaye mkawatapeli (mnadai wameunguza accounts zao). This is pathetic. Kiufupi Forex ni matokeo ya International trade and Multinational companies activities. Tuanzie hapo kwanza. Mleta mada lete hoja zako tukuelewe ni kwa nini mimi binafsi niingie kwenye Forex? Na kwa nini usinishauri nifungue Bureau de Change kama nina mtaji wa kutosha?
 
Utapeli kwa kwenda mbele. Huna hoja za msingi wala hujatoa ufafanuzi wa shutuma zinazowakabili TMT. Achane utapeli nyie watu. Forex market haipo hivyo mnavyoiongelea bali mnajaribu kuwaibia watanzania wasioielewa. Haya mambo ni mapana mno, inahitaji mtu kuwa na idea ya International Finance, siyo nyie mnataka hata walio wakulima wawaelewe kwa maneno yenu matamu ya utapeli.
Brother, hapa jf sio padogo kuna watu wasomi wa kada mbalimbali na hii kitu wengi waliipinga sana lakini mkafanikiwa kuwashawishi baadhi ya watu na hatimaye mkawatapeli (mnadai wameunguza accounts zao). This is pathetic. Kiufupi Forex ni matokeo ya International trade and Multinational companies activities. Tuanzie hapo kwanza. Mleta mada lete hoja zako tukuelewe ni kwa nini mimi binafsi niingie kwenye Forex? Na kwa nini usinishauri nifungue Bureau de Change kama nina mtaji wa kutosha?
Sasa usianze kwa mihemko hivyo. Hakuna aliyekuzuia kufungua bureau de change. Kadhalika ni kweli kabisa forex si lelemama. Wapo magwiji wa miaka na miaka kwenye forex lakini hawajawahi kusema eti ni masters katika forex. Ndio maana kuna maonyo ya kutosha tu kwenye hii biashara; kama vile usifanyie trade hela iliyoshikamana na moyo. Pia tumia risk management. Kubwa ni kuwa na mwalimu ambaye ana uwezo wa kufanya analysis na kuja na matokeo ambayo yana uhalisia kwa angalau %70. Pia si kweli kuwa kila trade lazima ufanikiwe. Kuna mazingira ambapo kutokana na mwingiliano wa taarifa [economic/pilitical news] ni rahisi kubadili mkondo wa aidha kuuza au kununua. Haya yote utayaona ya kawaida pale ambapo mtaji wako unaruhusu, pia unafuata risk management. Nakushauri kama nawe unahitaji kufanya forex nitakuwekea kanuni zake hapa ili uone utahotaji au la. La msingi ukianza kufanya forex hutoacha. Amini hivyo
 
Umeandika sana, lakini niseme tu pamoja na kuandika sana huko haujajibu au kuelezeamambo muhimu. Ni maandishi mengi tu ila yasiyo na uhalisia na yako too gerenal.

Mfano kuna shutuma kua PIPS za JP markets zinampa yeye kwanza profit kabla ya mteja, yaani pale faida inapoanza kuingia basi inaingia kwanza kwa broker kisha ndio ziingie kwako, na inawezekana kabisa isifikie wewe kupata profit lakini Broker Jp market anakua ashadaka zake kupitia wewe, hili hujalizungumzia.

Pili kwenye Pips hizi hizi, zipo ambazo ziningia kwa TMT/Ontario na hapo mwanzo ilikua ni siri. Yaani ku trade ni trade mimi, lakini kwenye Pips zangu, ONTARIO anachukua na JP nae anachukua hapohapo, hili sijaona ukiliongelea katika uzi wako uliouandika mambo meeengiii. TMT walifanya hivi bila kututaarifu sisi members wao na hakipo kwenye makubaliano yetu sisi na wao, kitu ambacho ni sawa na wizi

Yule Msouth CRE kwa sasa ni chui na paka na JP market, yeye anadai kua swala la kukatwa Pips ndio ameligundua sasa ndio maana eti amemaindi kwanini Pips zetu zichukuliwe na JP. Ukweli ni kua hili swala alilijua kitambo tu maana tumeanza kulilalamikia toka kitambo. Habari tulizonazo ni kua CRE na ONTARIO wamegundua kua JP anawapiga panga kwenye commission zao za kuwatafutia vichwa ndio maana wamemaindi.

Wewe umeandika tu in general lakini kuna vitu vya kwenda in deep hukuandika
Kwa mwandiko huu una safari ndefu sana nakuonea huruma
 
Humble man, shida yako nini? Huko uliko hutosheki? We tuachie TMT yetu na JP Markets wetu. Pupa zitakuua
Kwanza tusalimiane msukule mwenzangu maana hatuna ugomvi Bali tumetofautiana mitazamo tu ya kuuona utapeli wa kijana makini mwenzetu. Chuki ya nini sasa!? Hufaidiki na TMT kivyovyote na hata Mimi saifaidiki hivyo niliamua kusema kuonyesha wengine Shimo lilipo ili waamue kupita au kukausha..kama Snowden vile alivyobutua lile kopo la US way back.

Ila jamaa aliekuja na huu Uzi kakurupuka maana amekuja bila facts in issue kaja bila rational reasoning anadhani anasaidia kumbe ndio anazidi kuibua maswali na mashaka zaidi kwa watu walio nje ya TMT maana kaja kama anakuja Kwenye mdumange vile bila kujua hoja zinazowatuhumu TMT ni nzito na inapaswa aje CEO na maandishi yake yale matamu kama Kamasutra ili arudishe imani yake kwa watu na sio huyu jamaa asie na facts wala writing techniques anaishia kurusha mapumb.u tu. Ahahaha!

Watu wameshtuka kama westlife vile we can't be "fool again"
 
What i know 100% ktk business yoyote ile inayolipa vizuri huhitaji nguvu kubwaaaaa kuitangaza hivyo, kuna vitu watu wanafichwa sana hata kama FOREX ni biashara halali duniani kote, ila kuna scams nyingi involved na wanatumia uelewa mdogo wa beginners kuwakamua hela kwenye hizo pips.. Biashara nzuri inayolipa huna haja ya kutumia nguvu kubwaaaaa kuinadi kuna tatizo kubwa mahali, kwanini Ontario asipige hela yake FOREX millions aachane na wateja anaowafundisha kupata hela za ada? Yeye kashatangaza, si atengeneze dollars FOREX tujue ame make figures ngapi ili tujue ukweli, sbb hapa wateja watakuwa wanaliwa kiaina ndio maana wanawakumbatia wasiende kwa brokers wengine.. Forex ni halali ila ukikutana na scammers ( Scammer | Define Scammer at Dictionary.com
www.dictionary.com › browse › scammer

a confidence game or other fraudulent scheme, especially for making a quick profit; swindle. verb (used with object), scammed, scamming. 2. to cheat or defraud with a scam. Origin of scam.)

ambao ni wengi sana Forex, ndio mtaliwa kweli kweli. So FOREX ni kuwa makini unafanya na broker unamjua kiasi gani,muaminifu na msharp kwa kiasi gani ku trade katika Financial markets. Hilo ndio muhimu kuliko yote..!!
 
Let me say something,

Ukweli ni kuwa kila kitu kipya kina changamoto zake. Yawezekana malalamiko yao yalikuwa yana ukweli ila wakakosa staha na uvumilivu katika kuwasilisha na kuona wanachokitaka kinachelewa.

Yaani u introduce forex mwezi wa tisa, na baada ya miezi mitano kila kitu kiwe kama wateja wanavyotaka?

Hapa hujatueleza kwamba ni vitu gani wateja walikuwa wanavitaka, na ni kwanini walishindwa kuvipata.

Kutokana na ukwasi uliopo kwenye hii biashara, wako watu hapa nchini waliijua mapema na wakawa wanafanya yao kimya kimya bila kutaka wengi wajue haya. Wapo watu binafsi pamoja na taasisi za kifedha. Sasa kati ya hao ambao wameona maslahi yao yanaingiliwa na TMT basi rafu nazo zikaanza.

Huenda ni kweli baadhi zilikuwa ni figisu za taasisi. Lakini ukweli utabaki kuwa ukweli daima, na ninaamini hata Ontario mwenyewe anajua wazi kwamba alichokuwa anatufanyia wateja wake hakikuwa fair, hata kama atakana hadharani. Ukweli utabaki moyoni mwake daima milele. Aliplan kutusaidia sawa, lakini je ni kwanini atuumize?.

Sasa turudi kwa wale wafaidika wa forex ya TMT. Ni hulka ya binadamu kutaka zaidi ya kiasi, na kuwa mdadisi na kutaka kujiongeza. Sasa baada ya hawa wenzetu kuona kasi wanayoitaka na mambo wanayoyataka hayaji kwa kasi waliyojipangia, wakaanza kunena mabaya kuhusu TMT pamoja na broker husika.

Ni kweli kwamba tulinena mabaya juu ya TMT, lakini huo ndio ulikuwa ukweli wenyewe na ndio mambo ambayo yalikuwa yanaexist TMT, mlitaka tuwanenee mazuri kama mna mioyo ya kondoo wakati mna mioyo ya mbwa mwitu?. TMT ni among worst broker in Africa. Anajificha kwenye kivuli cha STP lakini ni purely market marker. Kitu kibaya zaidi am sure kabisa kwamba utakuwa hujawahi hata kuisoma review ya JP markets mtandaoni bali umeishia kusimuliwa tu na akina Jeff kwamba ni broker mzuri. Naomba uchukue muda wako upite mtandaoni usome reviews zake halafu uje umsifie tena hapa. Hana review nzuri hata kidogo.

Suala la broker ni suala tete sana, watu hawajui tu. Wengi wa brokers tunaowatumia, nje ya huyu ambaye wawakilishi wake wapo hapa nchini, tunafanya nao miamala kwa ile tunaita mutual trust. Lolote laweza kutokea na hela yako ikapotelea huko nje. Kwenye forex kuna brokers wengi sana! Inatakiwa upembuzi wa kutosha kujua unafanya biashara yako na broker wa aina gani. Wengi wamepoteza hela zao huko nje bila kujua wanafanya biashara na broker wa aina gani. Wengi wa waliokuwa wanakuja hapa jukwaani kuiponda TMT, CEO wake, pamoja na JP Markets walikuwa/wanatoa mbadala wa brokers wao ambao kwa namna moja ama nyingine wana maslahi nao.

1. Hakuna unachokijua kuhusu brokers, na hili linatokana na sababu ya kwamba katika training ya TMT hakuna sehemu wanapofundisha kuhusiana na broker sababu wanajua wakiweka tu hicho kipengele, watawapata tu wale watu wenye mindset kama yako. One of qualities of good broker ni regulation, kwa mnaowafahamu brokers vizuri, tunaamini kwamba broker akiwa na license ya FCA basi ni broker mzuri. Na hapa ukweli unajieleza siyo mpaka niwalist broker wenye hiyo license. Sisi tunatrade na hao brokers na hawana Ofisi Bongo na hakuna hizo shida za kukimbia na hela kama unazoeleza ww. Acha mambo ya kumezeshwa mkuu.

2. Ni nani ana maslahi na broker kati ya nyie TMT mliokuwa mnaunga watu kwa affiliated links na wale watu ambao walikuwa wanaleta mbadala wa jp marktes kwa kutoa majina ya hao brokers tu? unajua IB ww? unaijua COI? acha kunywa maji ya bendera funguka akili.

Tunawajua TMT na ofisi zao tunazijua. Kwa tatizo lolote ofisi zao ziko wazi, hivyo hakuna namna yoyote unaweza kufanya miamala yako na broker akashindwa kukulipa halali yako wakati TMT tuko nao.

Sisi kuwafahamu TMT siyo kigezo cha wao kutufanyia mabaya kwa mgongo wa wema. Ni bora mtu yule ambaye anakufanyia ubaya waziwazi kuliko mtu anayejifanya mwema kwako lakini upande wa pili anakuumiza.

Hata hivyo kwa sasa ukihitaji kuwithdraw cash yako toka JP Markets inakuchukua saa kadhaa tu.

You are talking of saa kadhaa wakati watu tunawithdraw hela kwa few minutes. Last time nimewithdraw hela nimepata hela zangu after 12minutes.

Kama kuna tatizo limetokea, suluhu si kutoka na kwenda pembeni kutukana na kuleta ujuaji. Mtu mzima, tena mwanaume unakuja kupandisha uzi humu kuwasema watu wengine, kisa hujulikani, ni uzezeta tu. Mtu anakuvusha mto kwa kukubeba mgongoni unafika ng’ambo unasema, ‘limgongo lake linanuka…!’ Si watu hao. Zikitokea kasoro tunapeana ukweli humo humo kwenye grupu zetu na kwa uwazi na mwisho wa siku zile kasoro zinaondoka.

Wewe jamaa acha unafiki, unaijua sababu iliyokuwa inafanya watu kuondolewa TMT? Aisee narudia tena acha unafiki, watu wengi nikiwemo mimi mwenyewe tuliondolewa TMT sababu ya kuongea ukweli na tukaishia kuitwa majina kama virusi na masnitch.

Mwisho naomba tu niseme kwamba Qualities of good broker zipo sita kama ifuatavyo;

1. Security- Hapa ni maswal ya Regulation ambapo regulatory body zinazotazamwa
hapa ni (NFA and CFTC) kwa USA, FCA and PRA kwa UK, ASIC kwa Australia, SFBC kwa Swiss, BaFIN kwa German, AMF kwa France and AMF kwa Canada

2. Lower transaction costs hapa nazungumzia spreads and commisions

3. Easy deposits and withdraws

4. Trading platform - user friendly

5. Faster execution at the normal market condition

6. Customer Service - good customer service

Katika vigezo nilivyotaja hapo juu, JP markets anaqualify kwenye kigezo cha 3 tu. Sasa ww na akili zako timamu how can you say kwamba huyo ni good broker?

Ni matumaini yangu kwamba hiki kipengele kingefundishwa TMT vizuri kabisa, basi wangewapata wajinga wachache. Lakini kwa sababu walikijua fika walichokuwa wanakifanya ndio maana hiki kipengele kilirukwa. Wakati hiki ni moja vipengele vya mwanzo kabisa mtu kuvijua.
 
Fanyeni kazi mnazoziona ninyi wstu! Vihela vyakubangaiza mnarusha mitandao msiyoijua mtakuwa na pressure.
 
What i know 100% ktk business yoyote ile inayolipa vizuri huhitaji nguvu kubwaaaaa kuitangaza hivyo, kuna vitu watu wanafichwa sana hata kama FOREX ni biashara halali duniani kote, ila kuna scams nyingi involved na wanatumia uelewa mdogo wa beginners kuwakamua hela kwenye hizo pips.. Biashara nzuri inayolipa huna haja ya kutumia nguvu kubwaaaaa kuinadi kuna tatizo kubwa mahali, kwanini Ontario asipige hela yake FOREX millions aachane na wateja anaowafundisha kupata hela za ada? Yeye kashatangaza, si atengeneze dollars FOREX tujue ame make figures ngapi ili tujue ukweli, sbb hapa wateja watakuwa wanaliwa kiaina ndio maana wanawakumbatia wasiende kwa brokers wengine.. Forex ni halali ila ukikutana na scammers ( Scammer | Define Scammer at Dictionary.com
www.dictionary.com › browse › scammer

a confidence game or other fraudulent scheme, especially for making a quick profit; swindle. verb (used with object), scammed, scamming. 2. to cheat or defraud with a scam. Origin of scam.)

ambao ni wengi sana Forex, ndio mtaliwa kweli kweli. So FOREX ni kuwa makini unafanya na broker unamjua kiasi gani,muaminifu na msharp kwa kiasi gani ku trade katika Financial markets. Hilo ndio muhimu kuliko yote..!!
Mkuu nikuulize, hapo si unatumia mtandao wa simu? Sitaki kujua mtandao gani ila ni mara ngapi unasikia matangazo ya huo mtandao wa simu yako? Hujui marketing wewe, hivyo katika mambo mengine ukae kimya.

Kadhalika hakuna uscammer katika TMT au JP Markets. Hiyo link na tafsiri ya scammer uliyoweka hapo haihusiani na haya ninayoandika hapa. Wacha wale wanaohitaji kusikia kinachoelezwa wasikie na watekeleze. Wakienda huko na kuona matarajio yao hayakutimia ndio wafanye wanavyoona ni sahihi
 
Let me say something,



Hapa hujatueleza kwamba ni vitu gani wateja walikuwa wanavitaka, na ni kwanini walishindwa kuvipata.



Huenda ni kweli baadhi zilikuwa ni figisu za taasisi. Lakini ukweli utabaki kuwa ukweli daima, na ninaamini hata Ontario mwenyewe anajua wazi kwamba alichokuwa anatufanyia wateja wake hakikuwa fair, hata kama atakana hadharani. Ukweli utabaki moyoni mwake daima milele. Aliplan kutusaidia sawa, lakini je ni kwanini atuumize?.



Ni kweli kwamba tulinena mabaya juu ya TMT, lakini huo ndio ulikuwa ukweli wenyewe na ndio mambo ambayo yalikuwa yanaexist TMT, mlitaka tuwanenee mazuri kama mna mioyo ya kondoo wakati mna mioyo ya mbwa mwitu?. TMT ni among worst broker in Africa. Anajificha kwenye kivuli cha STP lakini ni purely market marker. Kitu kibaya zaidi am sure kabisa kwamba utakuwa hujawahi hata kuisoma review ya JP markets mtandaoni bali umeishia kusimuliwa tu na akina Jeff kwamba ni broker mzuri. Naomba uchukue muda wako upite mtandaoni usome reviews zake halafu uje umsifie tena hapa. Hana review nzuri hata kidogo.



1. Hakuna unachokijua kuhusu brokers, na hili linatokana na sababu ya kwamba katika training ya TMT hakuna sehemu wanapofundisha kuhusiana na broker sababu wanajua wakiweka tu hicho kipengele, watawapata tu wale watu wenye mindset kama yako. One of qualities of good broker ni regulation, kwa mnaowafahamu brokers vizuri, tunaamini kwamba broker akiwa na license ya FCA basi ni broker mzuri. Na hapa ukweli unajieleza siyo mpaka niwalist broker wenye hiyo license. Sisi tunatrade na hao brokers na hawana Ofisi Bongo na hakuna hizo shida za kukimbia na hela kama unazoeleza ww. Acha mambo ya kumezeshwa mkuu.

2. Ni nani ana maslahi na broker kati ya nyie TMT mliokuwa mnaunga watu kwa affiliated links na wale watu ambao walikuwa wanaleta mbadala wa jp marktes kwa kutoa majina ya hao brokers tu? unajua IB ww? unaijua COI? acha kunywa maji ya bendera funguka akili.



Sisi kuwafahamu TMT siyo kigezo cha wao kutufanyia mabaya kwa mgongo wa wema. Ni bora mtu yule ambaye anakufanyia ubaya waziwazi kuliko mtu anayejifanya mwema kwako lakini upande wa pili anakuumiza.



You are talking of saa kadhaa wakati watu tunawithdraw hela kwa few minutes. Last time nimewithdraw hela nimepata hela zangu after 12minutes.



Wewe jamaa acha unafiki, unaijua sababu iliyokuwa inafanya watu kuondolewa TMT? Aisee narudia tena acha unafiki, watu wengi nikiwemo mimi mwenyewe tuliondolewa TMT sababu ya kuongea ukweli na tukaishia kuitwa majina kama virusi na masnitch.

Mwisho naomba tu niseme kwamba Qualities of good broker zipo sita kama ifuatavyo;

1. Security- Hapa ni maswal ya Regulation ambapo regulatory body zinazotazamwa
hapa ni (NFA and CFTC) kwa USA, FCA and PRA kwa UK, ASIC kwa Australia, SFBC kwa Swiss, BaFIN kwa German, AMF kwa France and AMF kwa Canada

2. Lower transaction costs hapa nazungumzia spreads and commisions

3. Easy deposits and withdraws

4. Trading platform - user friendly

5. Faster execution at the normal market condition

6. Customer Service - good customer service

Katika vigezo nilivyotaja hapo juu, JP markets anaqualify kwenye kigezo cha 3 tu. Sasa ww na akili zako timamu how can you say kwamba huyo ni good broker?

Ni matumaini yangu kwamba hiki kipengele kingefundishwa TMT vizuri kabisa, basi wangewapata wajinga wachache. Lakini kwa sababu walikijua fika walichokuwa wanakifanya ndio maana hiki kipengele kilirukwa. Wakati hiki ni moja vipengele vya mwanzo kabisa mtu kuvijua.

TMT ulufukuzwa mwaka gani? Natumia neno ulifukuzwa maana hata lugha unayoongea ni ya ukakasi. Nitakujibu kwa ufupi tu. Hata hao brokers unaowaamini wewe leo kuna watu walipita huko na wakaumia pia. Hadi leo huwa nasoma reviews za broker wengi na unakuta clients wanalialia sana, so wakati mwingine ni suala la subjectivity. Kama wewe vile, unaonekana wazi kabisa kuwa ni mtu wa mambo ya uharaka haraka. Hata kama ulikuwa unakosoa ni wazi kuwa ulikuwa unatumia lugha ya ukakasi. Kama unatumia lugha sahihi ni wazi kabisa ungekuwepo hadi leo. Mimi ni mmojawapo wa wakosoaji wakubwa wa mambo ninayoyaona hayaendi sawa, na ninatumia lugha ya hekima. Sasa wewe, hata sijui umri wako ni wazi una mbwembwe katika ukosoaji na ndio maana unatupiwa virago.

Suala la IB liko wazi. Inaelekea hata wewe baada ya kujua jua kidogo analysis tokea TMT ukaona ni fursa ukakimbilia kwa hao wanaokupa link ili na wewe upate kamisheni kwa kila atakayetumia link yako. Sio mbaya ila ufanye kwa staha na sio tena kurudi kuanza kutukana ulikotoka ili upate na wewe vichwa.

Mwisho nasema wewe ndio uache UNAFIKI kwa kuwa unaongea mambo ya TMT kwa namna ambayo huijui kwa kuwa ulufukuzwa na hauko tena. Hata katika taasisi yoyote mfanyakazi au mteja akiwa kihrehere na mzandiki atafukuzwa tu maana kwa u-moja wako huongezi wala kupunguza kitu. TMT ipo na itaendelea kuwepo. Wanaendelea kupokea maoni na kuboresha kilichopo na mwisho wa siku usishangae na wewe ukajivuta tena TMT kisa tu kila kitu kinafanyikia hapa bongo. Kwa heri
 
Back
Top Bottom