cocastic
JF-Expert Member
- Nov 30, 2019
- 85,683
- 137,421
Unapiga mule mule yaaan,Mleta mada ulikula pizza gani, au vile vidude wazenji wa forodhani waita pizza?
Githeri/Makande ni namna ya upishi tu na aina ya makande yenyewe (kuna ya mahindi mabichi, makavu na makavu yaliyokobolewa)...
Kwa sisi wapenda misosi, huwa hakuna msosi over or underrated labda uwe umechacha...
Ukitaka uenjoy wali ndondo basi kuna ule wali ndondo uliolala kwenye jokofu, au ulilala kwenye chungu halafu ile morning unaugonga na chai ya maziwa...
Kula mboga za majani zozote zile sijui mchunga, majani ya kunde, majani ya maharage, sukuma, kabichi (ukitaka uinjoi imiksiwe na nyama), kisamvu (hili dude kula kiporo chake na wali nazi)...
Nafasi hata haitoshi hapa...