Ni bora kumiliki gari au nyumba?

Ni bora kumiliki gari au nyumba?

Jamani kuna jamaa yangu kapata pesa ya mkopo sasa kanifuata nimshauri je ajenge nyumba au anunue gari? Wakuu karibuni kwa ushauri zaidi

Alikopaje bila kuwa na malengo na hiyo hela. Aliyakiwa ajipange kabla hapo ataishia kufanya kitu asichotarajia aje ajute baadaye.
 
Duh naona mawazo ya vilaza kweli hapa...yaani ujenge nyumba wakati huna gari?Huko site unaenda na boda boda au daladala?Mafundi hawawezi hata kukuita boss ilhali wao wana bodaboda zao na wewe unapanda dala dala

Cpt. PHILIPS Gari itakuja baada ya.nyumba...mm nilianza na nyumba, ile hela niliyokuwa natumia kulipia kodi ya nyumba nili save nikanunua gari then nikauza nikanunua kiwanja na kuanza msingi wa nyumba ya pili, ile hela ya service na mafuta ya gari sasa hivi.natumia kujenga nyumba ya pili...nawasilisha
 
Cha kushangaza wanaoponda kununua gari wao ndio wa kwanza kuwasumbua wenye magari kwa kuomba lift,ndio wa kwanza kukusubiri getini mda wa kutoka,ukichelewa kidogo kashapiga simu vp leo bado umalizia kazi? Huyo huyo anayesema bora ujenge nyumba,hiyo nyumba yenyewe kaijenga nje ya mji mapinga,mwasonga,gezaulole au chanika,kazi anafanya posta,k/koo au mwenge na hiyo nyumba si nyumba bali ni pagale,nahita pagale kwa sababu haina hata ceilin board,haina hata plasta,dirishani umeweka nyavu,kwakua nyumba ipo mbali hawezi kukaa huko itambidi apange,sasa una pagale halafu umepanga si bora mie nilieamua kununua mkoko kusave mda maana naamka saa kumi na mbili unusu mpaka saa moja natoka kazini ndani ya dkk 45 nishafika kimbembe wewe lazima kwanza uamke saa kumi na moja kuwahi lifti au kurusha mkuki(kupanda dala dala).

Si bora hata uwe na pagale kuliko hayo mabati siku wakikufukuza hako kakazi ndo hiyo utajua.
 
Cpt. PHILIPS Gari itakuja baada ya.nyumba...mm nilianza na nyumba, ile hela niliyokuwa natumia kulipia kodi ya nyumba nili save nikanunua gari then nikauza nikanunua kiwanja na kuanza msingi wa nyumba ya pili, ile hela ya service na mafuta ya gari sasa hivi.natumia kujenga nyumba ya pili...nawasilisha

You only need reliable source/s of income to do both in any order!
 
Back
Top Bottom