Ni bora kumiliki gari au nyumba?

Ni bora kumiliki gari au nyumba?

najiuliza mtu kakopa 600m alafu hajui anunue gari au ajenge nyumba???
 
Nunua gari ukaishi kwa baba yako. Jenga nyumba uombe lifti kwangu kila siku......tena siku nyingine nikutimue.....
 
Jamani kuna jamaa yangu kapata pesa ya mkopo sasa kanifuata nimshauri je ajenge nyumba au anunue gari? Wakuu karibuni kwa ushauri zaidi

Alipoenda kukopa alikua na wazo la kuzifanyia nn?
 
Mkuu toa uzoefu wako wengine tujifunze kidogo kidogo!
Mkuu nimecoment kama utani lakini believe or not gari ikitulia inakuzalishia nyumba
nina mifano mingi sana ikiwa ni pamoja na mimi mwenyewe kufanikiwa kujenga kutokana
na mapato ya gari.
 
Hapa kila mtu atakua na mawazo yake,kama swala ni kuzalisha basi nyumba itachukua namba1 kwa maana ya kujenga na kuuza na si kupangisha watu ndani..gari unaweza kununua leo milion 20 na ukaliuza kesho yake tu kwa 18milio lakini nyumba unaweza kujenga kwa hiyo hiyo m20 na miezi sita tu baadae ukaiuza kwa 40milion ikitegemea na mji iliyopo nyumba hiyo,kwa hiyo kimsingi hapa kutakua na mawazo mengi tofauti
 
India mtu alinunua nyumba ina mke kabisa ndani. Awasiliane na madalali maarufu huenda hata Bongo ipo hiyo.
Wakati mnatafakari si Vibaya kuanza kujenga heshima bar kwanza. Kule matumizi ya huja bila kuomba ushauri wa mtu.
Kakopa bank gani? Au bank ya Ngende?
 
Million 600 ni hela ya mboga ya siku 60 kwa mama Tibaijuka. Hapo hamna nyumba wala gari
 
Duh naona mawazo ya vilaza kweli hapa...yaani ujenge nyumba wakati huna gari?Huko site unaenda na boda boda au daladala?Mafundi hawawezi hata kukuita boss ilhali wao wana bodaboda zao na wewe unapanda dala dala
 
Duh naona mawazo ya vilaza kweli hapa...yaani ujenge nyumba wakati huna gari?Huko site unaenda na boda boda au daladala?Mafundi hawawezi hata kukuita boss ilhali wao wana bodaboda zao na wewe unapanda dala dala
Kwa mawazo haya unaweza ukawashawishi wengi. lakini Hebu nikuulize ; kwamfano ukianza Kununua gari ilhali huna kibunda kingine utakuwa unalipack wapi??😁
 
Anunue daladala apige mavumba,tena aombee ruti ya huku kwetu ina nyomi sana mwaka mmoja tuu anarudisha hela zote!.
 
Kwa mawazo haya unaweza ukawashawishi wengi. lakini Hebu nikuulize ; kwamfano ukianza Kununua gari ilhali huna kibunda kingine utakuwa unalipack wapi??

Unakuwa unalipaki kwenye nyumba uliyopanda na kama ni zile za maeneo ya Tandale unapaki CCM...kwani ukienda nao mjini kwa wale wanaofanya Kariakoo na Posta wanapaki wapo?Apply the same rules
 
Cha kushangaza wanaoponda kununua gari wao ndio wa kwanza kuwasumbua wenye magari kwa kuomba lift,ndio wa kwanza kukusubiri getini mda wa kutoka,ukichelewa kidogo kashapiga simu vp leo bado umalizia kazi? Huyo huyo anayesema bora ujenge nyumba,hiyo nyumba yenyewe kaijenga nje ya mji mapinga,mwasonga,gezaulole au chanika,kazi anafanya posta,k/koo au mwenge na hiyo nyumba si nyumba bali ni pagale,nahita pagale kwa sababu haina hata ceilin board,haina hata plasta,dirishani umeweka nyavu,kwakua nyumba ipo mbali hawezi kukaa huko itambidi apange,sasa una pagale halafu umepanga si bora mie nilieamua kununua mkoko kusave mda maana naamka saa kumi na mbili unusu mpaka saa moja natoka kazini ndani ya dkk 45 nishafika kimbembe wewe lazima kwanza uamke saa kumi na moja kuwahi lifti au kurusha mkuki(kupanda dala dala).
 
Back
Top Bottom