lukelo sakafu
JF-Expert Member
- Feb 19, 2015
- 2,938
- 517
Jamani kuna jamaa yangu kapata pesa ya mkopo sasa kanifuata nimshauri je ajenge nyumba au anunue gari? Wakuu karibuni kwa ushauri zaidi
Mwambie ailetee mimi nimfundishe matumizi
Bora gari mkuu, wasio na magari wengi wanatembea kwa miguu lakini
wasio na nyumba wanalala kwenye nyumba.
Amepata mkopo wa shilingi ngapi.
anataka nyumba wapi eneo gani tanzania
anataka nyumba ya vyumba vingapi
anataka nyumba ya ukubwa gani
ukishasema haya naweza kukupa ushauri, kuna nyumba za hadi m500
loading....
Jamani kuna jamaa yangu kapata pesa ya mkopo sasa kanifuata nimshauri je ajenge nyumba au anunue gari? Wakuu karibuni kwa ushauri zaidi
Gari kwanza hilo ndo litakuja kuzaa nyumba.Nyumba kwanza
amepata mkopo wa shilingi ngapi.
Anataka nyumba wapi eneo gani tanzania
anataka nyumba ya vyumba vingapi
anataka nyumba ya ukubwa gani
ukishasema haya naweza kukupa ushauri, kuna nyumba za hadi m500
nlitaka kumuuliza amechukua mkopo wa sh ngapi? Kama hivi vimkopo vyetu vya mil 6 mpaka 10 sidhani kama anaweza kujenga nyumba,namshauri kama anataka gari anunue kwanza viwanja kwa hela hiyo yote hata kama vitatu sehemu tofauti tofauti,ikipita miaka miwili auze kimoja anunue gari,kingine auze ajengee nyumba kwenye kiwanja cha tatu.
lukelo;
mwambiye hivi; kama kiwanja kipo bondeni anunue gari, kikinuka mabondeni aweza kulala kwenye gari. Lakini kama kiwanja kipo mahali pazuri, ajenge nyumba.
Faida;
kukinyesha mvua ataenda huko kwa boda boda atakaa raha
akikosa kaz atapata hela za kodi ya pango hatalala njaa
unaweza kuwa na gari likakosa hata tone la mafuta
kila njia, nyumba ni bora kuliko gari. Waweza kuweka hati ya nyumba rehani ukapata gari jipyaaaa
Acha maskhara wewe mkopo wa nini wakati una scania 100?Nina muheshimu mwenye nyumba moja,kuliko mwenye scania 100!hata bank mkopo watampa mwenye nyumba sii mwenye gari