Ni bora CHADEMA ifutwe

OOOOOOOOH GUYS,, :hungry: THIS MAN WHO POSTED THE TOPICS ANAFIKIRI WE LIKE SUCH CCM WE TIRED FOR EXPLOITATION WE NEED RIGHT TOWARDS OUR OWN LIFE....SASA YEYE HAS LIFE GIVEN BY CCM THATS WHY ANATAKA CDM IFUTWE MY FRIEND UR STILL ASLEEP WHILE US WE WAKED UP WE DONT WANT TO BE RULED OUT LIKE CUF. MTAISHIA KUSHIND KIUJANJA UJANJA KILA SIKU. WANASEMA MAENDELEA HAYAJI KWA BAHATI MBAYA LAZIMA WATU WAJITOE MUHANGA...NDIO CHADEMA YENYEWE... POLE SANA FOR FEW SUPPORT. TEHE TEHE TEHE.
 
Inaonekana kama ungekuwa wewe ni msajiri WA VYAMA VYA SIASA..........UNGESHATUINGIZA VITANI
 
Jaribu kuficha upumbavu wako mara mojamoja!!

Ndugu yangu MWIBA umejiachia saana ndio tatizo la kuwa kibaraka huoni aibu kuandika utumbo against chadema siku zote -ile kwa sasa ni taasisi na ina nguvu ya umma, umma unakubali kazi ya chadema.
 

Mwiba utapata shida saana kufanikiwa na agenda za kuwa kibaraka wa ccm ndani ya jf, these are great thinkers -njaa inakusumbua nitafute nikupe ajira rasmi sio kuwa kibaraka na kufungwa uwezo wako wa kufikiri. Sioni mantiki ya post zako zaidi ya orders ninzoziona katka post zako.
 
Wakuu wote JF naomba mnisaidie. Mimi huwa nikiona posts kama hizi huwa sizijibu lakini naona ninyi mnazijibu. Sababu ya mimi kutojibu posts kama hizi:

  1. Huwa nagundua kabisa feeling ya aliyeiweka. Ikiwa yuko serious huwa nagundua, tena kirahisi. Asipokuwa serious pia nagundua kirahisi. Kwa mfano huyu aliyeweka hii post (Mwiba) hayuko serious kwa sababu mambo anayoyataja so far yalishatolewa majibu na ufafanuzi. Mwiba si mgeni hapa JF hivyo anafahamu vizuri majibu ya hoja zake ndani na nje ya JF, hivyo kuweka post hii ni katika kurusha roho vijana wenye kuhangaika kujibu kila hoja.
  2. Msimamo wa baadhi ya members ambao wako very biased humu JF unafahamika, hivyo ni rahisi kutambua ajenda ya chini ya kapeti ya mtu anayeweka post. Kwanini kupoteza muda kujibu? Hata kama itawekwa post ya namna hii hata kupitia yule tusiyekubaliana naye basi kuwe na hoja.Sasa hoja hakuna, tunachojibu ni nini? Au ni raha ya kutukanana?
Mi nadhani JF inatakiwa kutumika kujadili masuala mazito zaidi na kwa mtindo wa hoja. Dah! Kuna wakati huwa najiuliza hivi JF ndiyo hii niliyokuwa naisikia?

Wakuu naomba kwa taadhima mnijibu mnapata wapi moyo wa kujibu mizaha? Mi naona nashindwa "kufanikiwa" kama ninyi!!

Asanteni.
 

Inategemea mtazamo wako uko compatible kiasi gani na muanzisha hoja!!

Pengine hatanii na ndivyo alivyo, pengine hana mawaza ya siri na pengine yuko serious

Huwezo wako wa kugundua post ya mtu ni very unique mwambie Invisible akuweke uwe MODS!

Muanzisha thread naweza kusema pengine anataka positive move from chadema, anataka chadema wawe harsh, wapenda vita, wagomvi, na hatakai upadre unaoendelea sasa hivi. wako wanachama wa hivyo ambao wanataka VIOLENCE LAKINI NI WANACHAMA HAI NA WAZURI TU, HUYU NI MMOJA WAPO,NA HII POST IS DEPICTING HIS ANGER TOWARDS RECENTLY moves.

the best way ukiona post haina maana usichangie kabisa maana kwa kufanya hivyo umeshavutwa kuchangia. personally kuna watu ambao wako kwenye ignorelist yangu. sitachangia hata iwe vipi si kwa sababu ya uwezo wa kuwazaau kujua their secret intention , hapana bali hoja zao tu.

kaka uko juu!!
 
3D umenena jambo zuri. Lakini tukumbuke kuwa kila mtu ana uhuru wa kusema mawazo yake, na Mwiba kasema ya kwake ingawa zimekuwa pumba zisizojulikana ni za zao gani, mpunga, mahindi, mbigiri? Lakini nashukuru kuwa amepata alichohitaji, watu wamemjibu na amejua sasa ni nini mapenzi ya wengi. Sauti ya watu ni sauti ya Mungu.
 

The Following User Says Thank You to Waberoya For This Useful Post:

3D. (Today)
 

The Following User Says Thank You to Nyota Njema For This Useful Post:

3D. (Today)
 

Na wewe sijui umesomea chini ya mti au vipi? Tutajie kifungu cha Sheria ya Vyama vya Siasa, 1992, kilichovunjwa na CHADEMA mpaka kistahili kufutwa, au unataka tufuate ushauri wa mkeo/mumeo kuhusu CHADEMA bila kufuata sheria?
 
Kuna watu nawashangaa sana,wakidai eti kwa kuwa chama ni cha kikabila au kidini kitakufa.Sijui hiii falsafa ameitoa wapi.Hebu fikiri je mtu anaweza kukataa kabila lake kwa ajili ya chama?.Na ikiwa ni chama cha kabila kwa nini mimi ambaye ni wa kabila hilo nisikipende chama changu??Au kama ni cha kidini kwa nini kife?Mimi ambaye ni wa dini hiyo nikiue chama changu??Ikiwa huyu aliyeandika anamaanisha hivyo.Hayo ni mawazo mepesi.Usiombe chama kiwe cha kidini au kikabila.Hujui usemalo Bull,kama huna data nyamaza mambo haya naona yanakuzidi urefu na upana.Dini imekuwepo toka kuanza kwa miaka,kabila ndio usiseme,eti kukiwa na chama kinachoungwa mkono na mihimili isiyokufa chenyewe ndio kife.Fikiria vizuri kuhusu hoja yako.Usijaribu kufikiri kiuvivu kama ulivyofikiri.Watu wako tayari kufia dini zao,watu wako tayari kufia kabila zao na ndio maana kukiwa na vita ya kabila haiishi,Bull usichochee kitu kisichokuwepo.
 
Ukisema kitu kifutwe utakuwa unazo sababu za kutosha,kwa kutoa vipengele kadhaa ambavyo wamekiuka.Ukikurupuka kama ulivyofanya,huo ndio udikteta,tunaishi kwa misingi ya sheria.Hivyo toa kifungu cha sheria na adhabu yake iwe kufutwa.Vinginevyo you are not a great thinker.Huna Data,huna kifungu huna haki ya kuandika kama ulivyofanya.Wewe ndio unatakiwa uchukuliwe hatua au ulipe gharama za kuchafua jina la CDM kwa kauli yako ambayo hujaifanyia utafiti.
 

Hujiwezi Weye!!!
 
Ndugu yangu kwanza nomba nikupe pole kwa maoni yako yasiyo na tija wala nmaslahi kwa taifa, kinachokufurahisha ni nini kwa uchafu wa ccm , hebu wahurumie watanzania maskini wanaoteseka kwa sababu ya mfumo mbovu usiojali maisha ya wanyonge , naomba jihurumie na wewe mwenyewe kwa sababu Dowans tu inaliyumbisha taifa , katiba sisemi , kagoda nanyamaza, epa yataka uvumilivu,bei mpya ya umeme ni masimango , ndugu yangu kama ni kufutwa ingeanza ccm kwanza, nihurumie mimi kwa hilo.
 
<br />
<br />
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…