Ni aibu Graduates kukosa Laptop

Ni aibu Graduates kukosa Laptop

Mtoa mada zuzu sana
Nimebeba laptop for 3 yrs mpaka bega limeenda upande moja juu lingine chini then unaleta ubishoo wa kubeba libegi for nothing ,tumia simu hata email inatuma na kusoma email pia
 
Mimi nna application ya microsoft office kwenye tecno f1 yangu vitu vingi naweza fanya.
 
harafu anasema miaka yote mnayokuwa chuo mnashindwa kuwa na laptop hawa ndio wale wanaopata mkopo na bado wanawadanganya wazazi wao hawapati mkopo wanapewa hela bado na wazazi wao
Huu unaoleta ww ni ulemavu wa akili na kupambana kumilik laptop sio ushua,huwez kukosa laptop ya laki 3 ukiwa km uni students ama graduate in all angles uwe mnufaika wa mkopo ama unalipiwa na wazaz tena unakuta kuna watu wanasoma vitu vya ovyo chuo na analipia fee 1.3M kwa miaka 3 knowing anaongeza umri chuo,bora ukitumiwa iyo ada uanze kujishughulisha na harakat za mtaa acha chuooo
 
Are you serious?
Hivi graduate wote wanatoka maeneo yenye umeme wa uhakika?

Maana anaweza kuwa na laptop yake lakini kwa umeme wa solar betri haina uwezo wa kuchaji laptop. Au umeme usiwepo kabisaa!!!
Na hizo used nyingi ni kama desktop! ! Na hata kama ana laptop bado ataenda tu stationary kuprint kama ni kazi za kuchapa nk. May be awe full occupied

Nadhani hata kwa kutumia simu unaweza kujaribu kufanya baadhi ya vitu kama vile kutumia excel, word nk kwa WPS wakati huo unajipanga kupata njia mbadala!

Wakati niko chuo x, niliwahamasisha sana wanakundi wenzangu kuchapa kazi zao kwa kutumia simu (kwa wasio na laptop) japo inatumia muda mrefu lakini unaokoa zile mia 5 mia 5 za kuchapa. Inabaki kuedit na kuprint! Na unapata uzoefu!

Ila kukosa laptop sio ushamba. Inategemea na mazingira! Usiwape graduate presha za bureee
Nunua mpya kwa laki tano afu km graduate unaishije sehem isiokua na uhakika wa umeme mzee,relocate ASAP
 
Aliyetoa mada anaakili ya kitoto Sana I naelekea ni mtoto wa mwisho kwao na haelewi maisha aliyonayo yeye na wenzie ni tofauti Sana ukiangalia kitaa 1. Matumizi ya laptop sio mengi kushinda simu janja yake 2.Kitochi kuchaji ni sh300 smartphone 500 ukipeleka laptop kuchaji 5000 kasoro 3.Wote tukimiliki bakery ya mikate Nani atamuuzia mwenzie
4. Tambua ukiwa na laptop lazima uwe na simu janja pembeni so unanipa gharama mbili zaidi anyway kila mtu na wazo lake
 
Mtaani vijana wetu graduates wengi wanazingua sana. Yaani graduate mzima unakuwa huna laptop kweli? Unathamini kuwa na smartphone ya laki 3 badala ya kununua laptop used ya hata 250,000 au 300,000/=?.

Maombi ya kazi online utafanyaje? Mtu alikupa kazi ndogo ya muda mfupi utafanyaje? Au mpaka uende stationary huko mtaani?!

Miaka yote unayokaa Chuo unashindwa kumiliki laptop used kweli? Kuna PC mpaka za laki 2.

Cha ajabu mtu anakuwa na Infinix Hot 11 ya 350,000, halafu laptop hana.

Ni ujinga na utoto mwingi sana.
Na wewe pia ni graduate etiii!

Kama hujui tu tofauti ya neno stationery na stationary unapata wapi nguvu ya kuwaambia wenzako kwamba kukosa laptop ni ushamba?

Usikute hapo umeahidiwa na shemeji kwamba semester hii utaenda chuo ukiwa na laptop baada ya bwana shemeji kufurahishwa na dada.
 
Back
Top Bottom