NHIF yakanusha kadi za wanachama kutotumika katika hospitali binafsi

Rare Sapphire

JF-Expert Member
Jul 24, 2021
576
1,626
416600594_337212192572848_5045905412067654046_n.jpeg



WIZARA YA AFYA
MFUKO WA TAIFA WA BIMA YA AFYA

TAARIFA KWA UMMA

KUKANUSHA TAARIFA ZA UPOTOSHAJI ZINAZOSAMBAA KUHUSU KUTOKUTUMIKA KWA KADI ZA WANACHAMA KATIKA VITUO BINAFSI

Januari 07, 2024 Dar Es Salaam,

  • Mfuko wa Taifa ya Bima ya Afya (NHIF), unakanusha taarifa za upotoshaji zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii zikielezea kuzuiwa kwa kadi za wanancham kupata huduma ama kupewa rufaa kwenye hospitali za binafsi zilizosajiliwa na Mfuko.
  • Taarifa hizi hazina ukweli wowote na badala yake zina nia ovu ya kuleta taharuki kwa wanachama wa mfuko. Ukweli ni kwamba huduma za matibabu kwa wanachama wake zinaendelea kama kawaida kupitia vituozaidi ya 9,000 vilivyosajiliwa na Mfuko vikiwemo vya Binafsi, Madhehebu ya Dini na Serikalli.
  • Kutokana na hayo, Mfuko unapenda kuwahakikishia wanachama wake kuwa huduma za matibabu zinaendelea kama kawaida katika vituo vyote vilivyosajiliwa na Mfuko na endapo kutakuwa na mabadiliko yoyote taarifa rasmi itatolewa kupitia njia rasmi ikiwemo kurasa za Mfuko zilizoko kwenye mitandao ya kijamii.
  • Endapo mwanachama atakutana na changamoto ya kukatliwa huduma katika kituo cha huduma atoe taarifa kupitia ofisi za Mfuko zilizo karibu au kupiga simu namba 119.
Imetolewa na;

Grace Michael
KAIMU MENEJA UHUSIANO
===

Pia soma:

Hebu tuambizane, hospitali binafsi zimeanza mgomo baridi Kwa wanaotumia Bima za NHIF?

Hospitali za private (binafsi) zatishia kutohudumia wagonjwa wanaotumia bima ya afya ya NHIF
 
Hawa NHIF wamikurupuka na kufuta toto card ili Watoto wa kitanzania wafe.

Kwa Nini hawakuandaa utaratibu kabla ya kufuta ghafla?

Bla bla
 
Hii ishu ya afya inachukuliwa poa sana. Serikali kupitia wizara husika itafakari upya. Nchi haiwezi kupiga hatua bila kuwa na huduma nzuri ya afya.
 
Back
Top Bottom