WanaJF, utaratibu wa kupata huduma ya afya kwa wenye bima ya NHIF, sijui bima zingine inakuwaje, huwa huduma na dawa zote ulizopewa katika hospitali fulani zianandikwa na doctor kwenye fomu ya NHIF alafu wewe mgonjwa au ndugu anasaini kuonyesha kuwa kweli ulipewa huduma hizo na fomu hizo baadae hupelekwa NHIF ili walipie huduma uliyopata. Imenitokea mara kadhaa nikieenda hospital hasa za private na doctor anaprescribe dawa mbili au tatu lakini nikienda pharmacy kuchukua dawa pharmacist ananipa dawa pungufu na kuniambia kuwa dawa fulani niliyoandikiwa imeisha lakini wakati huo tayari nimesaini fomu ya bima na kusaini inamaanisha kuwa huduma na dawa zote zilizoorodheshwa kwenye fomu ile nimepewa! NHIF wakipelekewa fomu ile wanalipia hata dawa ile niliyoambiwa imeisha. Sasa huwa najiuliza, je kweli dawa hiyo inakuwa imeisha? Je haiwezekani kuwa huu ni ujanja tu unaofanywa na private health providers kujipatia free money? Je wadau mmewahi pia kukutana na hali kama hii? Kama ndiyo, je nini kifanyike kurekebisha hali hii?