Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 360,098
- 828,942
Wapinzani wa nguvu za uchawi ama ni waoga sana au ni wagomvi kupitiliza
Utabishaje kuwa hiki hakipo wakati umeshaambiwa wazi kabisa kwamba IT CAN NEITHER BE CREATED NO DESTROYED! uchawi ni roho hasi (negative energy) watu wa hasi na chanya wananielewa vema... Kwamba kuna negative force na positive force! Nguvu hasi na nguvu chanya
Kibuyu ama tunguli si lolote si chochote kama kuna kolabo hazijafanyika! Haina tofauti kabisa na mashine yoyote hata zile full automatic... Bila kuwa na kianzilishi/chanzo, mashine lako automatic litabaki kama lilivyo (chukulia mfano wa gari) huwezi kutoa maelezo mafupi kwanini linatembea!
Matunguli ni makasha ama vibebeo vya kubeba nguvu isiyoonekana lakini yenye nguvu sana! Tunguli haina tofauti kabisa na mwili uliobeba roho isiyoonekana... Unapobisha kuwa hakuna uchawi ni sawa na kusema hakuna uhai na hupaswi kuwa hai... Kwahiyo wewe endelea tu kubisha
Sent using Jamii Forums mobile app
mishen town