Crucifix
JF-Expert Member
- Feb 20, 2011
- 1,651
- 588
Tumeshuhudia utawala wa sasa ukitumia vyombo vya dola kama nyenzo na matokeo yake wote mmeona. Nchi imekuwa ngumu kutawalika, ufisadi umeongezeka, rushwa hadi bungeni!!! Uchaguzi uliopita ulimleta msemaji wa jeshi kuhusu utaratibu; lakini hapaswi kuongea hata pale nchi inapovamiwa - bali waziri ndiye mwenye jukumu. Mabomu ya machozi yamerindima kila kona na sasa hadi watoto wa shule (primary) nao wamepuliziwa. Usalama wa Taifa leo ni mtuhumiwa wa utekaji na utesaji, lisemwalo lipo...........
Kada zote, kuanzia rais, makamu hadi mlalahoi tumekuwa wajasiriamali; wakubwa kwa wadogo. Na hatulipi kodi ipasavyo. Kodi wameachiwa walevi (samahani kwa wanywaji) na wavuta sigara. Sisi ni taifa la wabangaizaji! AIBU. Usistaajabu utakapoambiwa SIDO wanalipa kodi kuliko benki.
Leo wamegoma madokta, kesho walimu, jana wa migodini. Life expectancy 44yrs mafao uyasubiri 55yrs. Sheria za game zinabadilishwa dakika 90 bado! Wakitangaza kugoma serikali inakimbilia mahakamani. Majaji na mahakimu ni wateule wa rais. Duh! Utawala unatumia mabavu zaidi! Polisi wamekuwa watii hata kuwapiga virungu watu wanaotetea maslahi yao!
Chama cha wafanyakazi (TUCTA) mimi nakiita 'bukta' hakina meno! Bunge haliwezi kukemea serikali tena! Kila mbunge wa CCM anavizia uwaziri. Vyama vya upinzani vinafukuza wabunge machachari. NGO zinajaribu lakini ndio kila siku utawasikia kina 'analialia' Nkya tu! Hao hao. Ina maana hakuna wanaharakati wengine wa kuongeza nguvu? Akina Baregu walinyimwa ajira na kina Marando 'imara' wanatetea watuhumiwa wa serikali, hiyohiyo wanayoipinga!
Wenye 'kiherehere' wanalishwa 'polodium' na wakinusurika wanazawadiwa uwaziri. Urais unatafutwa hadi kwa waganga wa jadi. Uhasama katika siasa unatisha. Hii nchi inakwenda wapi? Leo mgomo wa wafanyakazi wa mgodi mmoja tu unatikisa matajiri wa marekani, nchi yenye akiba kubwa ya dhahabu kuliko zote duniani.
SITASUBIRI 2015. NITATUMIA FURSA YOYOTE ITAKAYOPATIKANA KUELEZA UKWELI NA KUUTEKELEZA. LIWALO NA LIWE. MKINIOKOTA MABWEPANDE MJUE NA NYINYI MKO NJIANI.
Ngumu kumeza lakini ndiyo Tanzania yetu aliyotupatia Mungu, ni sisi wenyewe tunashindwa kuibeba.
Kada zote, kuanzia rais, makamu hadi mlalahoi tumekuwa wajasiriamali; wakubwa kwa wadogo. Na hatulipi kodi ipasavyo. Kodi wameachiwa walevi (samahani kwa wanywaji) na wavuta sigara. Sisi ni taifa la wabangaizaji! AIBU. Usistaajabu utakapoambiwa SIDO wanalipa kodi kuliko benki.
Leo wamegoma madokta, kesho walimu, jana wa migodini. Life expectancy 44yrs mafao uyasubiri 55yrs. Sheria za game zinabadilishwa dakika 90 bado! Wakitangaza kugoma serikali inakimbilia mahakamani. Majaji na mahakimu ni wateule wa rais. Duh! Utawala unatumia mabavu zaidi! Polisi wamekuwa watii hata kuwapiga virungu watu wanaotetea maslahi yao!
Chama cha wafanyakazi (TUCTA) mimi nakiita 'bukta' hakina meno! Bunge haliwezi kukemea serikali tena! Kila mbunge wa CCM anavizia uwaziri. Vyama vya upinzani vinafukuza wabunge machachari. NGO zinajaribu lakini ndio kila siku utawasikia kina 'analialia' Nkya tu! Hao hao. Ina maana hakuna wanaharakati wengine wa kuongeza nguvu? Akina Baregu walinyimwa ajira na kina Marando 'imara' wanatetea watuhumiwa wa serikali, hiyohiyo wanayoipinga!
Wenye 'kiherehere' wanalishwa 'polodium' na wakinusurika wanazawadiwa uwaziri. Urais unatafutwa hadi kwa waganga wa jadi. Uhasama katika siasa unatisha. Hii nchi inakwenda wapi? Leo mgomo wa wafanyakazi wa mgodi mmoja tu unatikisa matajiri wa marekani, nchi yenye akiba kubwa ya dhahabu kuliko zote duniani.
SITASUBIRI 2015. NITATUMIA FURSA YOYOTE ITAKAYOPATIKANA KUELEZA UKWELI NA KUUTEKELEZA. LIWALO NA LIWE. MKINIOKOTA MABWEPANDE MJUE NA NYINYI MKO NJIANI.
Ngumu kumeza lakini ndiyo Tanzania yetu aliyotupatia Mungu, ni sisi wenyewe tunashindwa kuibeba.