Mwananyange......nimelipenda tu hilo jinaBora umeuliza jirani, unakufaham kwa mwananyange?? Halaf naskia ukipita karibu kamauna jini kichwani waweza jiunganao kwenye ngoma yao, hapo itakua tukwa kibao
hahaha huyo mama mtaani kwangu ni maarufu kwa hizo ngomaMwananyange......nimelipenda tu hilo jina
Hujambo dada?
Hizo ngoma ni maarufu kwenye mikoa kama ya Tanga, Kigoma, Tabora, Mwanza na Dar na utashangaa kuna hata wasomi na watu wenye exposure huwa wanashirikihahaha huyo mama mtaani kwangu ni maarufu kwa hizo ngoma
Na sjui why zinajaaga mashoga ndio wachezaji
Me sjambo kaka angu hofu kwako
sjui hua zina maana gani, na ng'ombe wanaochinjwa hapo si mchezo, nakumbuka niliwah kupita karibu mana hua watu wanajaaga nikaona huyo mama memtaja kwa mbele kaweka kitu kama mapembe na manyasi nyasi pembe kazifunga na kitambaa chekundu anaenda na beat ya ngoma ile nilikua na maswali mengi sana bora hii mada imewekwa hapa nipate kujifunza halaf sasa navosikia wanawekwa maziwa sjui miwa asali wanatenga kabisa katika sinia then wanaweka kwneye chumba kinajulikana kama kilinge yan ndio wametengewa hao mashetani hahahahaha naomba tu leo nijifunze mana naona kudanganyika tu na maswali kibao kichwan kwanguHizo ngoma ni maarufu kwenye mikoa kama ya Tanga, Kigoma, Tabora, Mwanza na Dar na utashangaa kuna hata wasomi na watu wenye exposure huwa wanashiriki
Miye sijambo pia namshukuru Mola
hata ukisogelea kama hujui unakua na maswali kibao kutokana na yanayoendelea, kilichoniogopesha hata wale watazamaji nao wakawa wanapandisha wanaanguka tu nikatimka mbio kwa kweliSiku ingine ikitokea bora usogelee ili ujifunze mwenyewe zaidi
Hazina umuhimu zaidi ya watu kuzidhulumu nafsi zao.Mshana Jr Hapa mtaani kwa ndugu zangu wadigo leo ni siku ya tatu wanacheza ngoma za mashetani. Watu wamejaa, wengi. Magari huwezi amini wingi wake. Mbuzi, kondoo, kuku vinachinjwa , damu mbichi zinanyweka etc. Ebu tufahamishe ngoma za mashetani ndiyo kitu gani? Umuhimu wake ni upi?
Bro bila shaka hapa umeongelea USOMI wa usecular sio ?Hizo ngoma ni maarufu kwenye mikoa kama ya Tanga, Kigoma, Tabora, Mwanza na Dar na utashangaa kuna hata wasomi na watu wenye exposure huwa wanashiriki
Miye sijambo pia namshukuru Mola
Hiyo inaitwa chano. Inakua na vitu vitamu kama miwa, asali, ndizi kusukari, halua, mkate wa kumimina na vitu kama juice ambavyo huwekwa kwenye siniawanawekwa maziwa sjui miwa asali wanatenga kabisa katika sinia then wanaweka kwneye chumba kinajulikana kama kilinge yan ndio wametengewa hao mashetani
Hiyo inaitwa chano. Inakua na vitu vitamu kama miwa, asali, ndizi kusukari, halua, mkate wa kumimina na vitu kama juice ambavyo huwekwa kwenye sinia
Wanasema hicho ni chakula cha hao mashetani ambao huja kupitia miili ya binadamu na kuja kula hivo vitu. Katika baadhi ya makabila na koo jambo hili linafanyika kila mwaka na wanapiga na hizo ngoma za kuwaalika hao viumbe
Inasemekana kua hiyo ni aina ya matambiko kama matambiko mengine yanayofanywa kwa aina tofauti kwenye makabila mengi hapa nchini au Afrika kwa ujumla
Kuna wakati Tanga zinapopigwa hizi ngoma huwa wanatembea barabarani mchana kweupe, wanaume wakiwa vifua wazi na wanawake manyonyo nje!
Wanaoshiriki mambo haya wanadai inawafanya wakae vizuri katika maisha yao kwa mwaka mzima. Yaani ni matambiko ya kuondoa mikosi ya kuumwa, kuharibikiwa na mambo ya kazi au biashara, kuvurugikiwa na mahusiano ya kifamilia kama vile ndoa n.k
Jambo la kushangaza kama nilivosema awali ni kwamba hata waliowasomi na wenye exposure kubwa kwenye hizo koo ikiwemo waliowahi kuishi Ulaya na Amerika wanaamini na kushiriki hayo mambo!
Utakuja tupiwa zongo we endelea kupiga chabohata ukisogelea kama hujui unakua na maswali kibao kutokana na yanayoendelea, kilichoniogopesha hata wale watazamaji nao wakawa wanapandisha wanaanguka tu nikatimka mbio kwa kweli
Bro secular haina uwezo wa kumjulisha mtu kwamba jambo fulani baya na jambo fulani zuri hasa kitabia. Kwahiyo usishangae hata yule aitwae msomi wa ki secular akawa anakula huku anakimbia,akawa hajui hata kuoga janaba,vipi atajua kuhusu ubaya wa hayo mangoma ?
Tabora ndio kwenyewe sasa mkuu. Kuna baadhi ya maeneo kule kila baada ya nyumba nne au tano kuna "fundi" wa ngoma hizi!Nakumbuku nilivyokuwa mdogo haya nilikuwa naya shuhudia mkoani Tabora
na linavouma s mchezo,nilikua na safari zangu na njia lazika upite hapo pembeni ya nyumba iliokua inachezwa ngoma, niliyaona hivoUtakuja tupiwa zongo we endelea kupiga chabo
Bro mambo ya kishirikina yote huongozwa na ujinga.Kwa kiasi fulani nakubaliana nawe kua sio ustaarabu wote unaletwa na u secular. Kuna mambo mengi sana yamekwenda kombo kwa kuumbatia huo u secular. Lakini elimu ya ki secular si inapingana moja kwa moja na mambo haya mkuu?
Tabora ndio kwenyewe sasa mkuu. Kuna baadhi ya maeneo kule kila baada ya nyumba nne au tano kuna "fundi" wa ngoma hizi!
Pia kuna viongozi wakubwa Serikalini akiwemo Marehemu Chifu Abdallah Fundikira, Marehemu Samuel Sitta na wengineo walikua viongozi hasa wa waziwazi na wa kisiri wa mila na matambiko haya ya jadi
Labda kuna siri kubwa zaidi ndani ya mambo haya ambayo wajuzi zaidi watufahamishe na kutuelimisha