Ngoja niropoke

Ngoja niropoke

Ha haa unachukua hatua wakati bado upo nae. Mtaishia kukomoana mpeane stress mwishowe muuane. Hiyo ni love au?
Sisi tunapendana sana maana pia tulifanya na kolabo ya kilingeni.. hapa nina ruhusa ya kuongeza msaidizi kiroho safi kabisa...! Kupuliza kidoho muhimu sana ujue
 
Sometimes ni huruma tu na msaada kwakuwa ndoa ina maana kubwa kwa mwanamke kuliko mwanaume
In his late fifties mwanaume anaweza kuoa binti wa under 25 kitu ambacho ni kinyume kabisa kwa wanawake
Ha haa eti huruma. You are not serious.
Anakupelekesha maugomvi kila siku, ni msomi ana pesa zake unamuonea huruma ili iweje?
Hapo wewe ndo unamuhitaji zaidi ya yeye anavyokuhitaji.
Mwanamke yoyote akikuhitaji atanyenyekea...ukiona hakunyenyekei ujue hajali umuache usimuache yeye sawa.
 
Takwimu zinaonesha Wakala wa usajili, ufilisi na udhamini (RITA), kwa mwaka unapokea maombi ya talaka yasiyopungua 500+ Tanzania nzima.

Kilichonishangaza ni kwamba asilimia 78% ya Ndoa zinazovunjika ni wanawake ndio wanaoomba talaka na kupeleka maombi hayo.

Kilichonishangaza na Kunimaliza zaidi ni kwamba asilimia 89% ya wanawake wanaoomba talaka ni WANAWAKE WASOMI (Intellectual Women)

Swali; Wanawake wasomi wana SHIDA GANI, kwanini kwao talaka ziwe nyingi, kwanini wengi wanasumbuka na mahusiano na kwanini wengi ni single mothers?

Honestly kuna kitu hakiko sawa kwa hawa Intellectual women, kwa takwimu hizi tunaweza kusema elimu zimewaharibu badala ya kuwatengeneza wawe wake bora.

Ndio, haiwezekani asilimia 89% ya maombi ya talaka yakaliwe na wao pekeao, ina maana elimu zao zinawaambia kwamba solution pekee ni talaka, nawaza sana yani

Ngoja niropoke; wanawake wengi wasomi wana kakiburi ka maarifa kanaitwa "INTELLECTUAL ARROGANCE"

Haka kakiburi kanawaambia hivi "wewe ni msomi, una akili, unajiweza na mwanaume hatakiwi kukusumbua kwa lolote lile"

Haka kakiburi kamewafanya wengi washindwe kuwa wanyenyekevu kwa sababu wanajiona ni classy and high, inafika hatua wanaanza kuvimba.

Wengi walifanikiwa sana kielimu kiasi cha kupata fedha, vyeo na status katika jamii vichwa vikaelemewa sifa na kujiona wanajua na kuweza kila kitu.

Pengine ofisini kwao yeye ndo Managing Director na ana watu wengi wakiume wako chini yake kikazi, anataka na mumewe awe chini yake pia.

Elimu yake, cheo na fedha vinamwambia "Unastahili kunyenyekewa na sio kunyenyekea na unaweza kila kitu" wengi hapa ndipo wanapofeli sasa na kuleta mabalaa.

Pengine walipokuwa wanasoma waliambiwa maneno kama "Soma sana, tafuta fedha zako ili mwanaume asikusumbue kwa lolote lile" (hii ndo shida kubwa)

Kwahiyo wengi kuanzia hapo wakawa wanatembea na competetive mentality (fikra za kishindani) na muda wote wapo kinyume na jinsia ya kiume.

Kinachotokea, wakiolewa wanafanya mambo kama washindani (competetors) kwa wanaume wao na sio wapambanaji wenza (teammates)

Kitu kingine kinachowaharibu ni hizi FEMINISTS MOVEMENTS (harakazi zinazodaiwa kumpa nguvu mwanamke na kumkomboa kifikra)

Ukizifuatilia vizuri hizi harakati zinawafanya wanawake wahisi kwamba hata wao wanaweza kuwa kama wanaume since they can pay bills na ada za watoto.

Sikatai, ni kweli kabisa kuna majukumu mwanamke anaweza kuyaperform kama mwanaume lakini haitatokea hata siku moja akawa kichwa cha familia.

Elimu walizopata wengi wao zimewasababishia kakitu kanaitwa "Control Freak Disorder" (unajua ni kanini haka, soma hapa chini)

Ni kale ka akili ka kumtaka mwanamke amcontrol mwanaume na kumfanya mwanaume aenende vile mwanamke anataka (amuweke chini)

Na hii inatokana na ukweli kwamba wengi wameweza kuongoza kakundi ka watu, wengi wameweza kufanya vitu vikubwa katika academic fields zao.

Kitendo cha kufanikiwa kuongoza kakundi ka watu kinawafanya hata kwenye ndoa nafasi ya kuongoza ambayo ni ya mwanaume aitake mwanamke, yaani yeye ndo awe kichwa.

Msuguano unaanzia hapo, mwanaume yeyote yule anataka yeye ndo awe top, ikitokea mwanamke akataka kumshusha mwanaume ili mwanamke awe top balaa linaanza.

Fuatilia, wanawake ninaowazungumzia hapa wengi wana kakiburi, wanajiona, na wanaamini kwamba hakuna kitu wanahitaji kutoka kwa wanaume na wanaweza kila kitu pekeao.

Wanaume wengi wanatafuta fedha ili wahudumie familia zao na kuwatimizia mahitaji, ila kwa wanawake mambo yako kinyume kabisa!

Wengi wanasoma na wanatafuta fedha ili waweze kuthibitisha kwamba wanaweza kufanya kama wanaume, wanaweza kuishi bila wanaume na hawawezi kusumbuliwa kwa lolote.

Ndio maana, kukiibuka kaugomvi kadogo wengi solution inakuwa ni kuachana ili kuthibitisha kwamba "NINAWEZA KUISHI MWENYEWE NA KAMA NI MTOTO/WATOTO NITALEA COZ NINA FEDHA"

Dear ladies, black brother wenu nawakubali kinoma na nafurahi kuwaona vile mnastrugle kupambania ndoto zenu (hongereni kwa hilo)

Lakini, jitahidi kadri uwezavyo fedha zako, elimu yako na cheo ulichonacho/utakachopata visikutie Kiburi mbele ya mumeo uliyenae/utakaekuwa nae.

Ni kweli umefanikiwa kielimu, pengine una mshahara mkubwa, au biashara zako zinaenda safi, una cheo/position fulani somewhere lakini WEWE BADO NI MWANAMKE.

Wakati wowote uwapo mke, mpe nafasi mwanaume awe mume, awe baba, awe kuongozi, awe dereva wa familia huku wewe ukiwa kwake msaidizi.

Hata kama ofisini kwenu una wanaume wengi unaowaongoza na wananyenyekea mbele yako usitake na mumeo akunyenyekee..

Mpe yeye nafasi ya kuwa king, mtii, msikilize na panapohitajika ushauri mpe ushauri kwa upole huku ukionesha kwamba unamuheshimu na kuamini..

Kwanini wanawake wa sahivi wamesoma lakini hawadumu kwenye ndoa kama mama na bibi zetu walioishia darasa la nne/la saba.

Kadri mwanamke anavyoanda juu kielimu, kuna namna anapoteza WIFE TRAITS umakini unahitajika sana ndo mana wengi wanabaki single/single mothers.

Fuatilia wanawake woote unaowajua Tanzania ambao wana vyeo vikubwa, wamefanikiwa kibiashara au wapo top kwenye eneo lolote lile.

Wengi utagundua kwamba hawajawahi kuolewa, waliolewa wakaachika, walizalishwa na wakabaki hapo.

Elimu sio mbaya, fedha sio mbaya..lakini inakuwa mbaya pale inapoanza kumfanya Quuen atake kuwa king, haiwezekani!

[Nimemaliza kuropoka

Credit: WhatsApp forwarded msg
Author: Unknown
Hili ni darasa tosha na mwenye masikio na asikie. Wanawake wapo vizuri pindi wakiwa na hivyo vitu i.e. Elimu, Fedha, Cheo au Madaraka au bado "anauzika" i.e. bado hajachuja. n.k.. Wengi wanasahau kuwa hivyo ni vitu vya mpito tu. Wanajisahau iko siku inakuja watakuwa ni retired officers, watakuwa ni bibi vikongwe na nguvu(Physical strength) imepungua sana. Hapo ndipo ile Asili ya mwanamke kuwa chini ya Mwanaume inarudi kwa nguvu sana lakini by then ni too late. i.e. Mwanamke kwa Asili huhitaji awepo mtu(Me) atakeyempelekea kero zake, shida au hata kumuuliza maswali na kutaka walau kusikia akijibiwa na huyo mwanaume. Kama Mume alikwisha fariki basi mwanamke atakuwa na cha kusema e.g. "Dah, angelikuwapo .......(Me)hili lisingekuwa hivi."
Asante Mshana Jr kwa somo mujarabu sana.
 
Acha niwe mshamba, wakati bado nasaka maisha niliapa kutooa msomi Wala mwanamke mwenye kazi.kwasababu sioi mfanyakazi Bali naoa mtu wa kujenga naye familia

Nilifanikisha lengo langu, sijisifu Hadi leo sijawahi kutamkiwa neno lenye kuniumiza pamoja na kwamba ndoa haikosi changamoto.

Lakini nayoyaona kwenye ndoa za wenzangu, namshukuru sana MUNGU
 
Ha haa eti huruma. You are not serious.
Anakupelekesha maugomvi kila siku, ni msomi ana pesa zake unamuonea huruma ili iweje?
Hapo wewe ndo unamuhitaji zaidi ya yeye anavyokuhitaji.
Mwanamke yoyote akikuhitaji atanyenyekea...ukiona hakunyenyekei ujue hajali umuache usimuache yeye sawa.
Maneno ya Mungu yanatuasa tuishi nao kwa AKILI! Nazingatia sana hayo maneno
 
Hili ni darasa tosha na mwenye masikio na asikie. Wanawake wapo vizuri pindi wakiwa na hivyo vitu i.e. Elimu, Fedha, Cheo au Madaraka au bado "anauzika" i.e. bado hajachuja. n.k.. Wengi wanasahau kuwa hivyo ni vitu vya mpito tu. Wanajisahau iko siku inakuja watakuwa ni retired officers, watakuwa ni bibi vikongwe na nguvu(Physical strength) imepungua sana. Hapo ndipo ile Asili ya mwanamke kuwa chini ya Mwanaume inarudi kwa nguvu sana lakini by then ni too late. i.e. Mwanamke kwa Asili huhitaji awepo mtu(Me) atakeyempelekea kero zake, shida au hata kumuuliza maswali na kutaka walau kusikia akijibiwa na huyo mwanaume. Kama Mume alikwisha fariki basi mwanamke atakuwa na cha kusema e.g. "Dah, angelikuwapo .......(Me)hili lisingekuwa hivi."
Asante Mshana Jr kwa somo mujarabu sana.
Pengine walipokuwa wanasoma waliambiwa maneno kama "Soma sana, tafuta fedha zako ili mwanaume asikusumbue kwa lolote lile" (hii ndo shida kubwa)

Kwahiyo wengi kuanzia hapo wakawa wanatembea na competetive mentality (fikra za kishindani) na muda wote wapo kinyume na jinsia ya kiume.

Kinachotokea, wakiolewa wanafanya mambo kama washindani (competetors) kwa wanaume wao na sio wapambanaji wenza (teammates)

Kitu kingine kinachowaharibu ni hizi FEMINISTS MOVEMENTS (harakazi zinazodaiwa kumpa nguvu mwanamke na kumkomboa kifikra)
 
Back
Top Bottom