Ngeleja anastahili hili kwa uwezo wake

Ngeleja anastahili hili kwa uwezo wake

Joined
Oct 9, 2014
Posts
95
Reaction score
13
Mwaka huu Ni mwaka wa kusimamia maslahi ya taifa bila kusita tunayo nafasi ya pekee Na nafasi hii Ni ya kumpata mtu mwadilifu,mchapakazi Na anayeuzika .

Kusema hivi hakutoshi. Tunao watu wengi waliotangaza Na ambao inaonekana wana nia ya kwenda Magogoni.
Kuna makundi sita ambayo mpaka Sasa uchunguzi unaonesha kuna makundi matano.
1. Kundi la kwanza Ni la wanaotka Tanzania visiwani
2. Kundi la pili Ni la mawaziri wakuu wastaafu.
3. Kundi la jinsia ya kike.(Gender factor)
4. Kundi la wanaopitia mgongo wa dini
5. Kundi la mawaziri walio madarakani mpaka Sasa.
6. Kundi la vijana.

Kila mwaka makundi haya matano ya kwanza huwa yapo ila mwaka huu tumepata mtu ambaye anazo sifa Na anaingia katika kila kundi Na kuonekana Ni mtu sahihi.

Mtu huyu Ni Willium Ngeleja.
Kiukweli ukiangalia vijana wote kila mmoja bila kumungunya maneno lazima umtaje mtu huyu.

1. Wakati akiwa naibu Waziri wa nishati Na madini ilimchukua mwaka mmoja tu kupandishwa ngazi na kuwa Waziri kamili.
Hii inaonesha kuwa anao uwezo binafsi ambao wengine wameukosa Na mpaka Sasa wamekuwa manaibu Waziri kwa miaka hata minne bila promotion.

Niseme kuwa hata MH Rais kama anasita kuwaamini hata kuwakabidhi hizo wizara rasmi. Hii inaonekana kuwa uwezo wao bado Ni mdogo ukilinganisha Na kundi la vijana ambao bado Ni mawaziri mpaka Sasa.

3. Siasa anazotumia Mh Ngeleja Ni siasa safi ambayo ukiangalia utaona kuwa hana chembe ya shaka lolote. Makundi mengine haya yameufanya kusaka urais kama vita ya Simba Na swala. Watu wanawindana kila mahali kwa kupandikiziana kashfa ila hata kwa watu wa team ya T2015WMN tumeshuhudia wakifanya siasa safi bila kuwachafua wengine.

4. Nidhamu binafsi kwa chama Na watu wengine. Mfano miezi kadhaa iliyopita chama kiliwapiga ban Na mpaka Sasa hatujaona akivunja misingi ya adhabu hiyo. Pia Mh Ngeleja amekuwa mtiifu wakati wote Na haswa lilipokuja suala la kujiuzulu nyadhifa alizokuwa nazo baada ya sakata la Escrow

5. Matumizi yake ya vyombo vya habari. Mpaka Sasa Takwimu zinaonesha kuwa WMN anatumia vizuri media Na hii inamtofautishinamtofautisha Na wagombea wengine ambao kila kukicha mawakala wao wanahangaika huku Na huko wakuwatafutia public sympathy kwa watanzania. Matumizi mazuri ya media yanafanya watu kumwamini sana Kijana huyu ambaye amejiandaa kuwafanyia ma kubwa watanzania.

6. Kukubalika Eneo analotokea. William Ngeleja Ni mkazi wa mkoa wa Mwanza Na jimbo la Sengerema. Pia Ni mtu peke anayetoka kanda ya ziwa. Wote Ni mashahidi kuwa katika uchaguzi Wa s/mtaa waziri huyu mstaafu katika jimbo lake CCM ilishinda kwa 83%.

Pia anakubalika kanda ya ziwa amapo ndipo walipo wapiga kura wengi. Situmii hili kama sababu ya kuligawa taifa na ya kuwagawa wananchi.( nisinukuliwe vibaya). Bali huu ndo ukweli kuwa WMN amejipambanua kanda ya ziwa vya kutosha.

Ukiangalia umri, uwezo binafsi Na vitu vingine vingi na ukamchambua kila mmoja mmoja bila kupinga wala kusita mtu sahihi kwa wakati huu Ni WMN. Mambo yapo mengi Na siwezi yasema yote ila kusema kweli WMN Ni mtu wa kuaminiwa ili apeperushe bendera ya chama 2015.

Viva Ngeleja 2015.
 
Mtanzania Safi, well said. Ngeleja anastahili sana na amekidhi vigezo kuwa next president 2015
 
Mtanzania Safi, well said. Ngeleja anastahili sana na amekidhi vigezo kuwa next president 2015

Kama kiongozi wa umma amekosa maadili ya kiuongozi kwa kupokea pesa za Rugemalila, chama kimempa ban ya kutohudhuria vikao vya maamuzi, hana sifa kuwa mkuu wa nchi
 
Mtanzania Safi

Umesema vyema mtanzania safi. Ukiangalia umri wake bado ana uwezo mkubwa wa kimwili Na akili yake inachemka Na Kijana wa kizazi hiki. Viva T2015WMN
 
Last edited by a moderator:
Tangu mpenziwe FaizaFoxy awe rais kila MTU sasa anaamini anaweza kuwa rais.
 
Last edited by a moderator:
Ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha
Mkuu lusungo acha kucheka. Unajua taifa hilisio kwamba ni masikini kwa bahati mbaya LA hasha, Bali in kwa sababu Lima watu kama mleta mada wengi. Yaani wale watu wenye kashfa za rushwa,ufisadi nk ndio wanapigiwa chapuo bila aibu hats kidogo. No aibu kweli.
 
Last edited by a moderator:
Kama kiongozi wa umma amekosa maadili ya kiuongozi kwa kupokea pesa za Rugemalila, chama kimempa ban ya kutohudhuria vikao vya maamuzi, hana sifa kuwa mkuu wa nchi
Kuna rafu nyingi katika siasa zinazoxhezwa ili kuwamaliza nguvu watu wanaoonekans kuwa na uwezo Na Ni threats kwa baadhi ya watu .
Hoja ya ESCROW Ni kitu kilichotengenezwa ili kumchafua baadhi watu ambao waliona anao uwezo. Kama kweli hoja ya ESCROW ndio itumke kummaliza WMN je wale waliochukua hela kule STANBIC Mbona hawatajwi. Mimi naona wanataka wamtoe kama mbuzi wa kafara ili kujisafisha kupitia Ngeleja. Binafsi naamini katika uwezo wa mti Na sio kashfa. Ngeleja ana uwezo Na hizo kashfa tutaona mwisho wake.
 
Mwaka huu Ni mwaka wa kusimamia maslahi ya taifa bila kusita tunayo nafasi ya pekee Na nafasi hii Ni ya kumpata mtu mwadilifu,mchapakazi Na anayeuzika .
Kusema hivi hakutoshi. Tunao watu wengi waliotangaza Na ambao inaonekana wana nia ya kwenda Magogoni.
Kuna makundi sita ambayo mpaka Sasa uchunguzi unaonesha kuna makundi matano.
1. Kundi la kwanza Ni la wanaotka Tanzania visiwani
2. Kundi la pili Ni la mawaziri wakuu wastaafu.
3. Kundi la jinsia ya kike.(Gender factor)
4. Kundi la wanaopitia mgongo wa dini
5. Kundi la mawaziri walio madarakani mpaka Sasa.
6. Kundi la vijana.
Kila mwaka makundi haya matano ya kwanza huwa yapo ila mwaka huu tumepata mtu ambaye anazo sifa Na anaingia katika kila kundi Na kuonekana Ni mtu sahihi.
Mtu huyu Ni Willium Ngeleja.
Kiukweli ukiangalia vijana wote kila mmoja bila kumungunya maneno lazima umtaje mtu huyu.
1. Wakati akiwa naibu Waziri wa nishati Na madini ilimchukua mwaka mmoja tu kupandishwa ngazi na kuwa Waziri kamili.
Hii inaonesha kuwa anao uwezo binafsi ambao wengine wameukosa Na mpaka Sasa wamekuwa manaibu Waziri kwa miaka hata minne bila promotion.
Niseme kuwa hata MH Rais kama anasita kuwaamini hata kuwakabidhi hizo wizara rasmi. Hii inaonekana kuwa uwezo wao bado Ni mdogo ukilinganisha Na kundi la vijana ambao bado Ni mawaziri mpaka Sasa.
3. Siasa anazotumia Mh Ngeleja Ni siasa safi ambayo ukiangalia utaona kuwa hana chembe ya shaka lolote. Makundi mengine haya yameufanya kusaka urais kama vita ya Simba Na swala. Watu wanawindana kila mahali kwa kupandikiziana kashfa ila hata kwa watu wa team ya T2015WMN tumeshuhudia wakifanya siasa safi bila kuwachafua wengine.

4. Nidhamu binafsi kwa chama Na watu wengine. Mfano miezi kadhaa iliyopita chama kiliwapiga ban Na mpaka Sasa hatujaona akivunja misingi ya adhabu hiyo. Pia Mh Ngeleja amekuwa mtiifu wakati wote Na haswa lilipokuja suala la kujiuzulu nyadhifa alizokuwa nazo baada ya sakata la Escrow

5. Matumizi yake ya vyombo vya habari. Mpaka Sasa Takwimu zinaonesha kuwa WMN anatumia vizuri media Na hii inamtofautishinamtofautisha Na wagombea wengine ambao kila kukicha mawakala wao wanahangaika huku Na huko wakuwatafutia public sympathy kwa watanzania. Matumizi mazuri ya media yanafanya watu kumwamini sana Kijana huyu ambaye amejiandaa kuwafanyia ma kubwa watanzania.

6. Kukubalika Eneo analotokea. William Ngeleja Ni mkazi wa mkoa wa Mwanza Na jimbo la Sengerema. Pia Ni mtu peke anayetoka kanda ya ziwa. Wote Ni mashahidi kuwa katika uchaguzi Wa s/mtaa waziri huyu mstaafu katika jimbo lake CCM ilishinda kwa 83%.
Pia anakubalika kanda ya ziwa amapo ndipo walipo wapiga kura wengi. Situmii hili kama sababu ya kuligawa taifa na ya kuwagawa wananchi.( nisinukuliwe vibaya). Bali huu ndo ukweli kuwa WMN amejipambanua kanda ya ziwa vya kutosha.
Ukiangalia umri, uwezo binafsi Na vitu vingine vingi na ukamchambua kila mmoja mmoja bila kupinga wala kusita mtu sahihi kwa wakati huu Ni WMN. Mambo yapo mengi Na siwezi yasema yote ila kusema kweli WMN Ni mtu wa kuaminiwa ili apeperushe bendera ya chama 2015.

Viva Ngeleja 2015👍👍

Mimi nimtakie kila la kheri katika safari yake...mm simuungi mkono...mm nipo Team UKAWA...Magamba sina hamu nayo tena since Richmond, EPA, ESCROW, etc
 
Watu wengine ni ngumu sana hata kuwauza kwa wapiga kura. Mleta maada umejitahidi kumpamba mtu wako lakini sidhani kama anastahili na kama anaweza kupitishwa na magamba wenzake. Anyway endelea kukamata fursa kama anakupa za kumfanyia promo zipige!!
 
Mkuu lusungo acha kucheka. Unajua taifa hilisio kwamba ni masikini kwa bahati mbaya LA hasha, Bali in kwa sababu Lima watu kama mleta mada wengi. Yaani wale watu wenye kashfa za rushwa,ufisadi nk ndio wanapigiwa chapuo bila aibu hats kidogo. No aibu kweli.
Bw Bill Clinton alipingwa alipotangaza nia ya urais Na baadaye akashinda. Mzee Mwinyi naye akipingwa kabla ya kugombea urais kuwa ana kashfa Na hana uwezo ila mwisho wa siku akashinda. Rais Barack Obama naye alipingwa mno eti Ni mweusi Na hafai kuongoza ila mwisho wa siku akashinda. Uhuru Kenyata naye ilikuwa hivi hivi ila baadaye mambo yakawa imara na maadui zake akawafunga mdomo. Sishangai hata mwaka huu maneni yatasemwa dhidi ya WMN Na mwisho atapita. Watu hawaangalii vioja vya wizi n.k watu wanaangalia je kiongozi wao atawasaidia nini?
 
Last edited by a moderator:
Urais umekuwa urahisi.... Hata siamini kilichoandikwa.... Yaani Ngeleja yule??? Bora Ukawa kuwapa Nchi akisimamishwa kugombea huyu Mh.Ngeleja
 
naona wakala umejitahidí kumpamba kweli mtangaza nia wako,xaxa tukwambie kweli,huyo unayemmwagia misifa yote hyo ambayo hafanani nayo hakuna asíyejua mautumbo na mauozo yake tena usidhani watanzania ni matahira watu wameamka poyoyo we tena asipoangalia hata ubunge utamshinda mwaka huu nyang'au we!
 
Ngeleja anastali kuongoza nchi, kwanza hakurupuki anapoamua kufanya maamuzi. Ni mtu makini sana. Jambo moja muhimu ambalo napenda kuwakumbusha wanatanzania na wazalendo wenzangu kuhusu Ngeleja ni kwamba Ngeleja ndiye aliyeasisi mradi wa bomba la gesi kutoka mtwara mpaka dar es salaam na hatimaye kusambazwa nchi nzima. Mradi ambao ndiyo muarobaini wa Tatizo la umeme Tanzania, pia ,mradi ambao utaiwezesha nchi kuzalisha zaidi ya MW 10000, na kuiwezesha nchi kuuza nje ya nchi zaidi ya mega watt 7000 baada ya kukizi matumizi ya ndani ya megawatt 3000.
Akiwa kama kijana shupavu mzalendo na mpenda maendeleo ya nchi na watanzania kwa ujumla anatosha kuongoza nchi kama rais ajaye 2015.
 
Mwaka huu Ni mwaka wa kusimamia maslahi ya taifa bila kusita tunayo nafasi ya pekee Na nafasi hii Ni ya kumpata mtu mwadilifu,mchapakazi Na anayeuzika .
Kusema hivi hakutoshi. Tunao watu wengi waliotangaza Na ambao inaonekana wana nia ya kwenda Magogoni.
Kuna makundi sita ambayo mpaka Sasa uchunguzi unaonesha kuna makundi matano.
1. Kundi la kwanza Ni la wanaotka Tanzania visiwani
2. Kundi la pili Ni la mawaziri wakuu wastaafu.
3. Kundi la jinsia ya kike.(Gender factor)
4. Kundi la wanaopitia mgongo wa dini
5. Kundi la mawaziri walio madarakani mpaka Sasa.
6. Kundi la vijana.
Kila mwaka makundi haya matano ya kwanza huwa yapo ila mwaka huu tumepata mtu ambaye anazo sifa Na anaingia katika kila kundi Na kuonekana Ni mtu sahihi.
Mtu huyu Ni Willium Ngeleja.
Kiukweli ukiangalia vijana wote kila mmoja bila kumungunya maneno lazima umtaje mtu huyu.
1. Wakati akiwa naibu Waziri wa nishati Na madini ilimchukua mwaka mmoja tu kupandishwa ngazi na kuwa Waziri kamili.
Hii inaonesha kuwa anao uwezo binafsi ambao wengine wameukosa Na mpaka Sasa wamekuwa manaibu Waziri kwa miaka hata minne bila promotion.
Niseme kuwa hata MH Rais kama anasita kuwaamini hata kuwakabidhi hizo wizara rasmi. Hii inaonekana kuwa uwezo wao bado Ni mdogo ukilinganisha Na kundi la vijana ambao bado Ni mawaziri mpaka Sasa.
3. Siasa anazotumia Mh Ngeleja Ni siasa safi ambayo ukiangalia utaona kuwa hana chembe ya shaka lolote. Makundi mengine haya yameufanya kusaka urais kama vita ya Simba Na swala. Watu wanawindana kila mahali kwa kupandikiziana kashfa ila hata kwa watu wa team ya T2015WMN tumeshuhudia wakifanya siasa safi bila kuwachafua wengine.

4. Nidhamu binafsi kwa chama Na watu wengine. Mfano miezi kadhaa iliyopita chama kiliwapiga ban Na mpaka Sasa hatujaona akivunja misingi ya adhabu hiyo. Pia Mh Ngeleja amekuwa mtiifu wakati wote Na haswa lilipokuja suala la kujiuzulu nyadhifa alizokuwa nazo baada ya sakata la Escrow

5. Matumizi yake ya vyombo vya habari. Mpaka Sasa Takwimu zinaonesha kuwa WMN anatumia vizuri media Na hii inamtofautishinamtofautisha Na wagombea wengine ambao kila kukicha mawakala wao wanahangaika huku Na huko wakuwatafutia public sympathy kwa watanzania. Matumizi mazuri ya media yanafanya watu kumwamini sana Kijana huyu ambaye amejiandaa kuwafanyia ma kubwa watanzania.

6. Kukubalika Eneo analotokea. William Ngeleja Ni mkazi wa mkoa wa Mwanza Na jimbo la Sengerema. Pia Ni mtu peke anayetoka kanda ya ziwa. Wote Ni mashahidi kuwa katika uchaguzi Wa s/mtaa waziri huyu mstaafu katika jimbo lake CCM ilishinda kwa 83%.
Pia anakubalika kanda ya ziwa amapo ndipo walipo wapiga kura wengi. Situmii hili kama sababu ya kuligawa taifa na ya kuwagawa wananchi.( nisinukuliwe vibaya). Bali huu ndo ukweli kuwa WMN amejipambanua kanda ya ziwa vya kutosha.
Ukiangalia umri, uwezo binafsi Na vitu vingine vingi na ukamchambua kila mmoja mmoja bila kupinga wala kusita mtu sahihi kwa wakati huu Ni WMN. Mambo yapo mengi Na siwezi yasema yote ila kusema kweli WMN Ni mtu wa kuaminiwa ili apeperushe bendera ya chama 2015.

Viva Ngeleja 2015👍👍
Kwa kashfa ya Escrow bado tu mnamuuza?ama kweli tumbo litawaua
 
Back
Top Bottom