Ngassa ni wetu - Simba

Ngassa ni wetu - Simba

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,346
Reaction score
26,138
Klabu ya Simba imedai kuwa mchezaji Mrisho Halfan Ngassa bado ni mchezaji wao halali kwakuwa wana mkataba naye hadi mwisho wa msimu ujao.

Hayo aliyasema Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Hanspope alipokuwa akihojiwa na Radio One jana. Hanspope alidai kuwa Ngassa alipelekwa Simba kwa mkopo akitokea Azam FC lakini baadaye alisaini mkataba wa hadi msimu wa 2013/2014.

Ngassa tayari ameshatambulishwa rasmi kuwa amejiunga na Yanga.

Yetu macho...
 
sio mpenzi wa simba lakini katika watu walio makini pale Hans Pope ni mmojawapo na hana uswahili mwingi kama tulivyo wengi wetu, anaweza akawa na point!
 
Klabu ya Simba imedai kuwa mchezaji Mrisho Halfan Ngassa bado ni mchezaji wao halali kwakuwa wana mkataba naye hadi mwisho wa msimu ujao. Hayo aliyasema Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba,Hanspope alipokuwa akihojiwa na Radio One jana. Hanspope alidai kuwa Ngassa alipelekwa Simba kwa mkopo akitokea Azam FC lakini baadaye alisaini mkataba wa hadi msimu wa 2013/2014. Ngassa tayari ameshatambulishwa rasmi kuwa amejiunga na Yanga. Yetu macho...

Tatizo wachezaji wetu wengi wa bongo hawana elimu ya kutosha hivyo kuna uwezekano mkubwa wa ku sign mikataba wasiyoielewa vizuri.
 
sio mpenzi wa simba lakini katika watu walio makini pale Hans Pope ni mmojawapo na hana uswahili mwingi kama tulivyo wengi wetu, anaweza akawa na point!

Mkuu siamini hili, Simba wanaweza jichanganya kama walivyo jichanganya kwa Kelvin Yondan
 
Huyu hans muhaini hana lolote muongo tuu.
 
Mbona mnarukia conclusion wakati sakata ndo kwanza linaanza? Tusubiri majibu kutoka TFF ndo mseme mtakavyo.
 
Hii ni sinema nyingine kutoka kwa Rage, tusubiri tuone.
 
Rage alishawahi kutoa machozi katika usajiri wa Yondani na Mbuyu Twite mwisho ya yote walikua hawajafuata utaratibu. Pia ikumbukwe kua Hans Pop ndiye aliyekua mwenyekiti wa Kamati ya usajiri. Sasa anayesema Hans Pop ni makini sijui atatuthibitishiaje. Inawezekana ikama kweli kuna tatizo lakini Abdalah bin Kreb naona huwa yupo makini zaidi ndio maana alimfanya hadi Maharage kumwaga Chozi.
 
Alienda kwa mkopo afu akapewa mkataba duu,. Hii inatokea bongo tu
 
Tatizo wachezaji wetu wengi wa bongo hawana elimu ya kutosha hivyo kuna uwezekano mkubwa wa ku sign mikataba wasiyoielewa vizuri.

Wao hawana elimu ya kutosha lakini wewe uliyonayo umeshindwa kuitumia.......pathetic!

Kanuni za usajili zinasema kuwa mchezaji anakuwa huru kufanya makubaliano na klabu nyingine (tofauti na iliyomsajili) ndani ya miezi 6 ya mwisho ya mkataba wake. Hans Pope (Huyu jamaa anaitwa Zakaria) anadai Ngassa alisaini mkataba mwingine wa kumbakiza Simba kwa msimu 2013-2014. Swali la kujiuliza hapo, Ngasa angeweza vipi kusaini mkataba huo katika kipindi ambacho yeye (Ngasa) alikuwa mchezaji wa Azam bila ridhaa ya Azam?

Kabla hujawashambulia wachezaji na kuwaita wenye elimu ndogo, napenda nikukumbushe kuwa, wanaoongoza kwa kusaini mikataba wasiojua imeandikwa nini hapa Tanzania ni 'wasomi' na sio wachezaji wa Simba Koko na Yanga Africa.

Tuache kuwasakama wachezaji kwa kuwa tu hawakufanya yale tunayotaka sisi. Kama nchi inamsomesha mtu kiasi anaaminika kuwa mwanasheria mkuu wa serikali, halafu anatusainia mkataba wa madini wa miaka 100 kwa uwiano wa WAO 97%, SISI 3% na hatuna namna ya kuchunguza quantity, tuna haja gani ya kuwashikia bango wachezaji ambao hatukuwapa elimu wala mtaji?

Wakati Rage na huyo huyo 'Hans Pope' wanaingizwa mjini usajili wa Mbuyu Twite na wao walikuwa hawana elimu? Si walikuwa na makelele kama haya haya mpaka tukaambiwa kwamba Mbuyu Twite hatacheza na akachukuliwa RB, sasa kuna lipi jipya hapa la kuanza kumshutumu Ngasa hakusoma? Hawa wasomi si ndio hawa wanaandaa bajeti ya 1bn kwa makaburi huku wengine wanakunywa maji machafu kwa kukosa 8m za kununua pump ya kisima cha kijiji?
 
Alienda kwa mkopo afu akapewa mkataba duu,. Hii inatokea bongo tu

Mkuu hawa wanawazuga wanachama wao ili wasiwape maelezo ya wenendo wa timu. Kama unakumbuka wakati ule wa sakata la Ngasa kuuzwa Sudan, utata ulitokea kiasi ikabidi TFF watoe ufafanuzi juu ya nani ana mamlaka ya kuidhisha usajili wa Ngasa kati ya Simba na Azam.

Simba Koko walieleweshwa kwamba mchezaji si wao kwa hiyo hawana mandate ya kufanya mkataba wowote wa kumuuza, sasa cha ajabu Simba Koko hao hao wanayo haki ya kumsainisha mkataba na wao wenyewe.....blah blah blah za Msomali na Msaidizi wake.

Tangu wakung'utwe Libolo hawa jamaa akili haiko sawa.
 
Wao hawana elimu ya kutosha lakini wewe uliyonayo umeshindwa kuitumia.......pathetic!

Kanuni za usajili zinasema kuwa mchezaji anakuwa huru kufanya makubaliano na klabu nyingine (tofauti na iliyomsajili) ndani ya miezi 6 ya mwisho ya mkataba wake. Hans Pope (Huyu jamaa anaitwa Zakaria) anadai Ngassa alisaini mkataba mwingine wa kumbakiza Simba kwa msimu 2013-2014. Swali la kujiuliza hapo, Ngasa angeweza vipi kusaini mkataba huo katika kipindi ambacho yeye (Ngasa) alikuwa mchezaji wa Azam bila ridhaa ya Azam?

Kabla hujawashambulia wachezaji na kuwaita wenye elimu ndogo, napenda nikukumbushe kuwa, wanaoongoza kwa kusaini mikataba wasiojua imeandikwa nini hapa Tanzania ni 'wasomi' na sio wachezaji wa Simba Koko na Yanga Africa.

Tuache kuwasakama wachezaji kwa kuwa tu hawakufanya yale tunayotaka sisi. Kama nchi inamsomesha mtu kiasi anaaminika kuwa mwanasheria mkuu wa serikali, halafu anatusainia mkataba wa madini wa miaka 100 kwa uwiano wa WAO 97%, SISI 3% na hatuna namna ya kuchunguza quantity, tuna haja gani ya kuwashikia bango wachezaji ambao hatukuwapa elimu wala mtaji?

Wakati Rage na huyo huyo 'Hans Pope' wanaingizwa mjini usajili wa Mbuyu Twite na wao walikuwa hawana elimu? Si walikuwa na makelele kama haya haya mpaka tukaambiwa kwamba Mbuyu Twite hatacheza na akachukuliwa RB, sasa kuna lipi jipya hapa la kuanza kumshutumu Ngasa hakusoma? Hawa wasomi si ndio hawa wanaandaa bajeti ya 1bn kwa makaburi huku wengine wanakunywa maji machafu kwa kukosa 8m za kununua pump ya kisima cha kijiji?

mkuu umemaliza!
 

Angalia usikurupuke kufananisha scenario mbili tofauti. And Carrol ni mchezaji wa Liverpool anayechezea West Ham kwa mkopo. Waliochukua £15m za usajili ni Liverpool ambao ndio wenye mchezaji wao, kwa hiyo hilo halina ajabu na inafahamika kwamba dili hiyo ikikamilika basi Andy Carrol atakuwa mali ya West Ham moja kwa moja.

Kwa issue ya Ngasa, alikuwa mchezaji wa Azam anayechezea Simba Koko kwa mkopo. Anachodai Zakaria ni kwamba yeye (Ngasa) amesaini mkataba wa kuichezea Simba Koko kwa msimu wa 2013/14 jambo ambalo haliwezekani kwani by then Ngasa hakuwa mchezaji huru. Madai haya yatakuwa na mashiko kama Azam hawatayakana kwamba wao waliamua kumuuza Ngasa kwa Simba Koko jumla. Na kama kuna mkataba uliwahi kufanywa kati ya Azam, Ngasa na Simba Koko, basi Ngasa atakuwa anaujua.

Nachojaribu kukutofautishia hapa ni kwamba si kwamba Andy Carrol amejiamulia kusaini mkataba wa kudumu na West Ham, bali ni Liverfool ndio wameridhia kumuuza kwa kuwa ni mchezaji wao.

Ngasa yeye mara baada ya kunusurika kuuzwa utumwani Sudan, alieleza wazi kwamba yeye ana mkataba na Azam ambao unaisha mwisho wa msimu wa 2012/13 na yupo Simba Koko kwa mkopo na hatosaini mkataba wowote mpaka mwisho wa msimu atakapoamua hatma yake.
 
Mkataba unasigniwa hotel? mbona hata ile gari walompa ili ajiunge (VEROSSA) hana tena sijui mwenyewe amechukua maana ilikuwa ya Kaburu na sasa huyu Kaka hayuko tena Simba, watulie Simba huyu mtoto hana mapenzi na soka ana mapenzi na team..kama ni Soka hasingetoka Azam
 
sio mpenzi wa simba lakini katika watu walio makini pale Hans Pope ni mmojawapo na hana uswahili mwingi kama tulivyo wengi wetu, anaweza akawa na point!
Hans Pope ni Mwenyeketi wa kamati ya usajili ya Simba ambayo imefanya usajili wa wachezaji wabovu kama

  • Dan Mrwanda
  • Salum Kinje
  • Daniel Akuffor
  • Kanu Mbiyavanga
  • Pascal Ochieng
  • Abdala Juma
  • Konabil Keita
  • ​Derick Waluya

Sasa sijui huo umakini ni upi,pia kumbuka sakata la Mbuyi Twite na Kelvin Yondani
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom