Wao hawana elimu ya kutosha lakini wewe uliyonayo umeshindwa kuitumia.......pathetic!
Kanuni za usajili zinasema kuwa mchezaji anakuwa huru kufanya makubaliano na klabu nyingine (tofauti na iliyomsajili) ndani ya miezi 6 ya mwisho ya mkataba wake. Hans Pope (Huyu jamaa anaitwa Zakaria) anadai Ngassa alisaini mkataba mwingine wa kumbakiza Simba kwa msimu 2013-2014. Swali la kujiuliza hapo, Ngasa angeweza vipi kusaini mkataba huo katika kipindi ambacho yeye (Ngasa) alikuwa mchezaji wa Azam bila ridhaa ya Azam?
Kabla hujawashambulia wachezaji na kuwaita wenye elimu ndogo, napenda nikukumbushe kuwa, wanaoongoza kwa kusaini mikataba wasiojua imeandikwa nini hapa Tanzania ni 'wasomi' na sio wachezaji wa Simba Koko na Yanga Africa.
Tuache kuwasakama wachezaji kwa kuwa tu hawakufanya yale tunayotaka sisi. Kama nchi inamsomesha mtu kiasi anaaminika kuwa mwanasheria mkuu wa serikali, halafu anatusainia mkataba wa madini wa miaka 100 kwa uwiano wa WAO 97%, SISI 3% na hatuna namna ya kuchunguza quantity, tuna haja gani ya kuwashikia bango wachezaji ambao hatukuwapa elimu wala mtaji?
Wakati Rage na huyo huyo 'Hans Pope' wanaingizwa mjini usajili wa Mbuyu Twite na wao walikuwa hawana elimu? Si walikuwa na makelele kama haya haya mpaka tukaambiwa kwamba Mbuyu Twite hatacheza na akachukuliwa RB, sasa kuna lipi jipya hapa la kuanza kumshutumu Ngasa hakusoma? Hawa wasomi si ndio hawa wanaandaa bajeti ya 1bn kwa makaburi huku wengine wanakunywa maji machafu kwa kukosa 8m za kununua pump ya kisima cha kijiji?