News Alert: UTAPELI UNAENDELEA KWA NJIA ZA SIMU

News Alert: UTAPELI UNAENDELEA KWA NJIA ZA SIMU

Magimbi

JF-Expert Member
Joined
Oct 18, 2011
Posts
1,434
Reaction score
1,215
Samahani wana Jamvi mnivumilie kidogo na kama sio mahala pake basi naombeni mnisamehe lakini kuwagutusha ni jukumu langu pia. Ni hivi; leo terehe 3/05/2013 siku Ijumaa majira ya saa 11.15am na saa 02.50am kuna watu wawili wamempgia jamaa yangu simu wakijifanya wanamjua saana jina ila tu hawajui anapatikana wapi wala anafanyakazi gani.. Wanamwambia kuwa wako kwenye mradi wa Kilimo Kwanza huko Rufiji na wanamatekta tisa mabovu wanataka mtu wampe tenda ya kununua spea..sijajua namba ya huyo jamaa yangu wameitoa wapi ila wanajifanya kumfahamu sana. Katika kufuatilia namba hizo ambazo ni 0714 979 167 huyu jina hajalipata na mwingine ni namba yake ni 0652 036 102 amesajili namba yake kwenye Tigo Pesa ni BONIFACE MGAMBA. Hivyo nimeona niwagutushe kuna utapeli wa aina hii unaendelea hapa kwa sasa muwe makini na hizi namba. Pia wanaweza kutumia namba nyingine ni vema kuwa mdadisi mno pindi watakapokupigia kwa namba ngeni!!

Nawasilisha kama siasa za utapeli kwa njia ya Simu
 
Washenzi tu hao ni matapeli,hata huku songea leo jamaa kataka kuatapeliwa eti wanajifanya wanamradi wa majengo ya afya namtumbo,mara wanatafuta dawa ya kuulia wadudu kwenye nafaka,mara wanataka asimamie biashara.tangu lini mtu anapewa kazi bila hata kupata cv zake/
 
Tabia za hao jamaa ni kama zile za wasenegali.spea pati za kilimo kwanza lazima atafute agenti?
 
Asante mkuu kwa kutufungua macho na masikio.Hii post hapa ni sehemu sahihi maana inaingia popote kwasababu ni elimu tosha hasa ikizingatiwa kuwa utapeli upo ktk nyanja na sekta mbalimbali.Kuna utapeli ktk mapenzi,siasa,biashara,michezo,elimu nk
 
Wanaotapeliwa kwa njia hii wana matatizo ya akili. Mimi nilishapigiwa kama mara 3 hivi kwa staili tofauti. Lakini hebu jiulize mtu msiyefahamiana vizuri anaweza kukupa deal la kutengeneza pesa bila jasho. Kwanini of all people out there akupe wewe hiyo deal.

Juzi kati hapa kuna jamaa tunafanya nae kazi kalizwa 3m. Huyu jamaa pia siyo mjanja...ni mburula fulani hivi.
 
kazi kweli kweli maana naona nchi yeti inamatatizo kila mahali
 
Shida ni kwamba watu mnatupha manamba yenu facebook mkidhani ni salama.Hayo ndo madhara yake lakini kuweni waangalifu watz maana wengine ni wadada, akikupigia anakwambia ati ulimtumia sms then ukimwambia ni2mie hiyo sms anasema nilishaifuta.
 
Wajinga ndo waliwao! Umakini unahitajika sana siku hizi! Hali ya uchumi imekuwa ngumu kiasi kwamba matapeli wanatumia kila njia kuweza kujipatia chochote!!
 
Samahani wana Jamvi mnivumilie kidogo na kama sio mahala pake basi naombeni mnisamehe lakini kuwagutusha ni jukumu langu pia. Ni hivi; leo terehe 3/05/2013 siku Ijumaa majira ya saa 11.15am na saa 02.50am kuna watu wawili wamempgia jamaa yangu simu wakijifanya wanamjua saana jina ila tu hawajui anapatikana wapi wala anafanyakazi gani.. Wanamwambia kuwa wako kwenye mradi wa Kilimo Kwanza huko Rufiji na wanamatekta tisa mabovu wanataka mtu wampe tenda ya kununua spea..sijajua namba ya huyo jamaa yangu wameitoa wapi ila wanajifanya kumfahamu sana. Katika kufuatilia namba hizo ambazo ni 0714 979 167 huyu jina hajalipata na mwingine ni namba yake ni 0652 036 102 amesajili namba yake kwenye Tigo Pesa ni BONIFACE MGAMBA. Hivyo nimeona niwagutushe kuna utapeli wa aina hii unaendelea hapa kwa sasa muwe makini na hizi namba. Pia wanaweza kutumia namba nyingine ni vema kuwa mdadisi mno pindi watakapokupigia kwa namba ngeni!!

Nawasilisha kama siasa za utapeli kwa njia ya Simu

hao watu umenikumbusha walikuja hm kujitia wanataka kununua gar bt waliposhtukiwa wakapora cm wakaanza kutuma sms kwa kila no iliyokuwepo kwenye phone bk akijitia muhusika wa cm anaazima ela akaweka namba ya tigo pesa kwa kila anayemwomba ela aitume kupitia namba hiyo.tulipotaka kumtrace jina likaja boniface mgamba. ni vijana watatu watanashati balaa na vitamb juu huwez kuwazania wanajitia wanatokea mbeya na iringa.
 
Ndo jambo hlo wanataka kufanya watu km wale waschana waliokuwa wanajfanya wakmbiz wa Senegal. Twashkuru kaka.
 
Samahani wana Jamvi mnivumilie kidogo na kama sio mahala pake basi naombeni mnisamehe lakini kuwagutusha ni jukumu langu pia. Ni hivi; leo terehe 3/05/2013 siku Ijumaa majira ya saa 11.15am na saa 02.50am kuna watu wawili wamempgia jamaa yangu simu wakijifanya wanamjua saana jina ila tu hawajui anapatikana wapi wala anafanyakazi gani.. Wanamwambia kuwa wako kwenye mradi wa Kilimo Kwanza huko Rufiji na wanamatekta tisa mabovu wanataka mtu wampe tenda ya kununua spea..sijajua namba ya huyo jamaa yangu wameitoa wapi ila wanajifanya kumfahamu sana. Katika kufuatilia namba hizo ambazo ni 0714 979 167 huyu jina hajalipata na mwingine ni namba yake ni 0652 036 102 amesajili namba yake kwenye Tigo Pesa ni BONIFACE MGAMBA. Hivyo nimeona niwagutushe kuna utapeli wa aina hii unaendelea hapa kwa sasa muwe makini na hizi namba. Pia wanaweza kutumia namba nyingine ni vema kuwa mdadisi mno pindi watakapokupigia kwa namba ngeni!!

Nawasilisha kama siasa za utapeli kwa njia ya Simu
wapuuzi sana awa jamaa eti matapeli,majuzi eti wananijaribu kunitapeli alafu status yangu aliipata wapi?wanakuja na dil za maana ukiingia choo cha kike,wanakuliza.
 
Back
Top Bottom