New Series I: Madudu na sifa za Edward Lowassa!

New Series I: Madudu na sifa za Edward Lowassa!

Ukiniletea mtu ambae hajawahi kufanya makosa ntakuonesha Papo hapo mtu ambae hajawahi kufanya Chochote- Mzee Maganga Songoro (1938-2009)

“Show me a person who has never made a mistake and I'll show you someone who has never achieved much” ~ Joan Collins
 
Hivi kwanini Kina Msekwa walimbeba JK katikao cha chama siku Lowassa alipomhoji kwamba kwanini anakaa kimya yeye akichekwa kwa kosa ambalo ni yeye JK aliemzuia kuifukuza Richmond? Lowassa alimkumbusha siku alimpigia simu na kumweleza kuwa anawafukuza ndipo JK akamkatalia, baada ya kuhojiwa huku JK kijasho kikimtoka wazee wa chama wakaingilia na kumbembeleza Edo
 
Waingereza wana msemo kama huu hapa:

"When the need is too high; logic suffers" Roho, moyo na fikra zako zimegubikwa (too crowded by hate!!) na chuki kubwa dhidi ya EL; nimeacha kwa makusudi pia kutaja kwamba hata mwili wako! inaelekea EL angekuwa karibu na wewe physically ungemdhuru!!

Kutokana na akili yako kuwa crowded na chuki dhidi ya EL; Matokeo yake umetapanya uzi kwa uandishi dhaifu ili ubainishe chuki yako dhidi ya EL; chonde chode! nakusihi ujaribu kutanabahisha na kuainisha kwa kituo huo unaoita uchafu au Madudu ya EL; If you have facts huna sababu ya kuogopa kutamka bayana wanajamvi wakuelewe na waelimike; Funguka mkuu!

Avoid picking up dirt from the grape vineyard na kuzileta hapa kuziandika kwa chuki na jazba ili kuwashawishi watu wote wamuone EL kupitia "screen yako"

Ni kweli yapo ambayo EL kama yeye anapashwa kuwapa maelezo watanzania; na pia yapo mengi ambayo majibu yake yanabeba uwajibikaji wa pamoja kwa maana ya kwamba kama yanastahili pongezi na EL ni mdau wa pongezi hizo na kwa yale yenye utata EL na hao unaotaka kuwasafisha na kuwapaisha wanawajibika kwa pamoja;

Usimtenganishe EL na mfumo mzima ambao ameutumikia kwa muda mrefu. "Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni"

Kama ni kumnyonga au kumsifu EL basi ni vema anyongwe au asifiwe kwa pamoja na wale wote aliotumika nao na aliotumika chini yao kwani wote walikuwa wanatekeleza dhana ya uwajibikaji wa pamoja,

EL alikubali kuwa mbuzi wa kafara kwenye sakata la Richmond mwaka 2008; leo hii tunajua mengi yaliyojiri katika sakata hilo; je ni kweli EL aendelee kuwa mbuzi wa kafara peke yake licha ya facts nyingi zilizo bayana kwamba hakuwa peke yake;

je ni nini ulikuwa mchango wa Bosi wake katika sakata hilo na alichukua hatua gani mahsusi au aliamua kumtosa EL ili "yapite??!!"
 
Mkuu pamoja na hayo yote; Amini usiamini CCM watamsimamisha Lowassa kwenye nafasi ya urais 2015. Mkuu 2015 siyo mbali tumuombe mwenyezi Mungu atupe afya na uzima sote tushuhudie haya nayo kwambia. CCM yote kwa ujumla wao wanamuogopa Lowassa kama ngoma.

Amini nakwambia,mark my word!ccm hawawezi kumsimamisha lowasa!
 
EL kama Raila Kenya
EL utaishia soma plate number tuu
 
Siku akiupata urais, sijui hiyo hotuba itakayotolewa itakuwa imeandikwaje!! sipachi, EL huyu!! anaweza kubadilika akataka kuacha historia.
 
CCM ni machizi lakini kumteua LoWaSsa kugombea urais kwa Tiket ya CCM hawawezi fanya hivyo!
Lowassa ndo injinia wa kuivuruga CCM
Lowassa ndo mzee alie zalisha makundi
Lowassa ndo alifanya juu chini kumwaribia PM pinda iliaonekane ovyo
Lowassa ndo mpikaji udini nchini kwa kutumia Dini kuivuruga serikali lakini ndani ya Bunge kimyaaaaaa
Lowassa ndo Mr Dowans aka Richmond maumivu yake tunayabeba mpaka kesho
Lowassa ni silent killer anaeutaka urais kwa cost yoyote But we will be very kin on that

Lowassa ana Kampuni inayolipa kodi na kwenye Statement of Comphrehensive Income kuna Donation yaani zile pesa atoazo?, Je kampuni inaitwaje na Kodi inalipa sh ngapi? (10 marks.)
Lowassa anatoa misaada mingi sana je pesa hizo zinatikana na biashara gani yenye turnover ya sh ngapi na faida ya sh ngapi kwa mwaka (10 marks.)
Me and you tukianza kuiombea nchi itapona. ALL MARKS.
 
Nimeisoma habari yote kwa kina, ina mapungufu ya kiuandishi lakini kilichomo acha tuendelee kukitafakari kwa maslahi ya umma wote wa Tanzania.

Mwandishi aendelee kuleta thread nyingine pia za watu wengine na pia kama kuna mazuri wamefanya tujuzeni pia.

kuna mawaziri57,maRC26,maDC144 na wabunge kibao sasa mkuu aanze na nani amalize na nani?
Imemukuuma kusikia mabaya ya Lowassa anzisha uzi kuelezea mazuri yake kama mikataba ya RICHMOND.
Hapo vipi?
 
Waingereza wana msemo kama huu hapa:
"When the need is too high; logic suffers" Roho, moyo na fikra zako zimegubikwa (too crowded by hate!!) na chuki kubwa dhidi ya EL; nimeacha kwa makusudi pia kutaja kwamba hata mwili wako! inaelekea EL angekuwa karibu na wewe physically ungemdhuru!!
Kutokana na akili yako kuwa crowded na chuki dhidi ya EL; Matokeo yake umetapanya uzi kwa uandishi dhaifu ili ubainishe chuki yako dhidi ya EL; chonde chode! nakusihi ujaribu kutanabahisha na kuainisha kwa kituo huo unaoita uchafu au Madudu ya EL; If you have facts huna sababu ya kuogopa kutamka bayana wanajamvi wakuelewe na waelimike; Funguka mkuu!
je ni nini ulikuwa mchango wa Bosi wake katika sakata hilo na alichukua hatua gani mahsusi au aliamua kumtosa EL ili "yapite??!!"

Yaani hata sikuelewi kwani unapenda kukashifu wenzako kwa vihela unavyolipwa au unaandika kwa kumjua EL?
Hebu ishia hapo hapo maana huyu mtu tumeshamjadili sana na hasafishiki
Ukitaka kufunguka zaidi tembelea Ofisi Waziri Mkuu Dodoma, upate aliyoyafanya hiyo miaka miwili tu
mpaka kwenye Makazi ya PMO ya hapa Dodoma alibadili KWA KUWAFUKUZA KAZI kuanzia Bodyguard hadi mpishi mkuu (Mama aliyekuwa tangu Msuya, Salim, Sumaye) licha ya kumbakiza Dobi
Kwa hiyo usimsingizie Bosi wake kwani hakuhusika na hujuma zozote ambazo hata kina Mwakyembe hawakuziona (Huwezi kuwa na akili timamu ukahujumu mali za watanzania na kuwapandishia umeme hadi leo ukijua Bosi atakulinda ni ,,,,,,)
humu watu mmetumwa mmeyaona ya Kibanda kwani hapo mwanzo alishabikia na kuchangia lakini alipogundua ukweli akabadilika je? aliyoyapata mtamsaidia ?
 
kuna mawaziri57,maRC26,maDC144 na wabunge kibao sasa mkuu aanze na nani amalize na nani?
Imemukuuma kusikia mabaya ya Lowassa anzisha uzi kuelezea mazuri yake kama mikataba ya RICHMOND.
Hapo vipi?

Sina hakika kama umenielewa vema kwenye andiko langu mkuu, nimesema tuendelee kutafakari alichoandika mtoa thread kwa maslahi ya umma wote wa Tanzania, hapa na mimi ni mmoja wapo na pia nikasema mwandishi alete pia thread za watu wengine hata kama pia wamefanya mabaya ama mazuri pia.

Naona unanitajia mawaziri 57, ma RC 26, ma DC 144, lakini huyu mtoa thread alilenga wale wanaotajwa katika harakati za kugombea urais ifikapo 2015 tena pasipo shaka ni kupitia CCM, na hao sio wengi kama unavyotaka kunisadikisha kwa kutaja hao uliowataja.

Ni bahati mbaya ama nzuri kuwa mimi sio mwanachama wa chama chochote cha siasa, ingawa nimekuwa mpenzi wa siasa na baadhi ya wanasiasa hasa wa vyama vya upinzani, hivyo basi kuniambia kuwa imeniuma kusikia mabaya ya Lowasa hakika hunitendei haki na wala hukutaka kujipa tafakuri ya muda kuhusu nini nilichoandika japo ni kifupi sana yaani mistari miwili.

Ushauri: unaposoma andiko la mtu mwingine kama hulielewi direct, jaribu kutafakari kwa muda kidogo uone huyu mtu anamanisha nini anaposeme sentensi hii nk kuliko kutoa hukumu ya moja kwa moja kama ulivyofanya wewe.

Ninaposema tufanye tafakari kwa maslahi ya umma, lazima tuwaangalie watu wote wanaosema wanataka kuwa marais wetu kwa kina ili tunapofanya uamuzi uwe uamuzi wenye mashiko na maslahi kwa jamii pana, na ndio maana nilisema itakuwa vema kama habari za hao watu wote kwa mabaya na mazuri yao zikawekwa humu ili umma upate kuwajua.

Ahsante, nadhani utanielewa kwa maslahi ya umma pia.
 
Kwani aliyemwambia el amezaliwa kuwa rais wa tz nani????
 
Lowassa is "less bright", but not necessarily "brightless". I take it from both sides, whether he goes through or he stumbles in his presidency bid, the death of CCM is in his golden hands.
 
Jamani watu sijui mnalipwa bei gani na huyu Bwana Lowassa, hivi tumia utashi wa akili yako na elimu yako kidogo uliyo nayo kupembua mambo: Hivi uliona wapi mtu akitumia nguvu nyingi kiasi hiki kutafuta madaraka, mtu wa namna hii hana nia njema kabisa na taifa hili! acha urais ukufwate wewe na siyo wewe uutafute huo urais kwa nguvu za fedha..... uliona wapi!!! Mi naomba ninyi washauri wake, mjitahidi kumwambia na kumshauri alionee huruma hili taifa ambalo kuna watanzania wanateseka na kuishi bila kujua kesho watakula nini na watalala wapi, awe na uzalendo na taifa hili, siyo lazima yeye awe rais jamani!
 
Elisa,

Aliyewasaidia waTz kupata maji ya Victoria si Lowasa, ni rais Mkapa kwenye ahadi yake ya 2000 kwa mkoa wa shinyanga. Wakati huo Lowasa alikuwa kama sio bench ni ofisi tofauti kabisa. Baada ya uchaguzi wa 2000 ndipo Lowasa na Dk Limbu wakaingia wizara hiyo.

Utekelezaji wa mradi wa maji ulianza 2001 wakati wa Lowassa na Diallo kama NW.

Kama nilivyosema awali, wengi mnaompigia jalamba huyu Mhe ni adui zake (kwa kujua au kutokujua) au ni wapinzani wa ccm (kwa kujua au kutojua. Kama ccm wakamteua Lowasa kugombea urais ataanguka asubuhi tu! Madhambi aliyowafanyia watanzania ni mengi afadhali wakuweke wewe Elisa hauna historia ya kuwakosea waTz.

Sifa mnazompa lowasa hanazo, alibahatika kuwa kufanya kazi na wasaidizi makini na pia Rais makini. Wengi wetu tunasahau au hatujui Lowasa na matatizo yake ya nyuma: alipokuwa tume ya Loliondo, na alivyokula hela za waarabu na kuwaacha hadi leo wapo Loliondo badala ya ilivyotarajiwa na waTz (soma tume teule ya Bunge kuhusu Loliondo) ipo hansard za bunge. Pia alipokuwa AICC kama CEO alivyopoteza fedha za ujenzi wa staff na baada ya hapo alivyojinyakulia ardhi ya AICC na baadae kuuziwa Themi Hill Suites, na wengine walio jirani ardhi iliyokuwa ya AICC!

Pia msaada wa ujenzi wa kiwanda cha vyandarua Sunflag, Sumitomo waliwekeza na serikali ya Japan na WB wakatoa grant, lowasa akalazimisha kuuziwa hisa kiwanda hicho bila kutoa hata senti kumi.

Alipokuwa wizara ya ardhi, mnakumbuka alivyokusanya fedha kwa kuuza maeneo na haraka haraka kajenga majengo masaki ambayo yalileta skandali kubwa. Ubalozi wa Afrika kusini walipangisha jengo lake kwa gharama kubwa na dili hiyo ilifanyika yeye akiwa waziri wa ardhi.
Nyerere alimuona kama mwizi tu huyo, akamchomoa kutogombea urais 1995. Wizi wa mali ya umma kaanza miaka mingi.

Hata unapodai kuwa mchapa kazi sikuelewi. Ungesema ana maamuzi ya pupa tu. Mfano, alipoamuru jengo moja karibu na mess ya polisi livunjwe kwavile wahindi walikataa kumlipa fedha; maamuzi yake yamegharimu wizara na serikali mabilioni kwa amri ya mahakama.

Leo tunalia elimu kuanguka; kisa kimojawapo ni ujenzi wa pupa wa shule za kata! Aliacha mpango wa WB na Nordic countries na kutaka utekelezwe kwa jazba! Mradi wa kuyelekezwa kwa miaka 10 yeye kaamua ufanyike miaka 2! Matokeo yake, hakuna waalimu, vifaa, maabara, uwezo kukosekana wa kuwachukua wanafunzi kuelndelea na kidato cha 5 na sita! Leo mnaunda tume kutafuta mchawi! Mchawi ni Lowassa na maamuzi yake ya pupa.
Madhambi yatoikanayo na uamuzi wa hovyo alioufanya huyo ndugu yako ni mengi na pia utajiri alio nao wa kugawa fedha kwenye makanisa hauelezeki. Anatoa fedha kwa wakristo akidhani watamsaidia. Hajasaidia msikiti hata mmoja kama kweli angekuwa na nia ya kusaidia jamii ya nchi hii. Anafanya akijua eti zamu ya mgombea kutoka kwenye ukristo ndilo linalofuata! Anasikitisha kwa kuona karibu na kijinga hivyo! Ni kati ya wanaochochea mgawanyiko wa dini nchini!

Hana maana wala sababu ya kuendelea kuhadaa waTz. Ngoja ufike muda uone kivumbi. Kajitahidi kuwanyamazisha wahariri wa magazeti mengi, hajui wakati wa chaguzi magazeti yote huhuishwa na mengine kufuka kwa kazi moja tu ya uchaguzi! Kuhonga kuna mwisho wake.

Leo wahariri wanadhuriwa na kulalamika kunyamazishwa! Ni wao wameyatafuta hayo, unakula fedha ya mtu halafu unafanya kinyume na matakwa yake unatarajia nini? Kwenye fedha mtu atakufanyia lolote akiona unataka kumdhulumu kinyume na matarajio yake.

Huu ni mchango ulioandikwa jana kwenye Jukwaa la Wanabidii na bwana Tony PT. Nitaendelea kutoa muendelezo wa sifa, wajihi na uozo wa watu mbalimbali waliojitokeza kuutaka Urais.

Kuna mazuri ambayo EL ameyafanya,kuhusu maji Mkapa alitamka wazi kuwa maji kwa Shinyanga ni ndoto,kama si juhudi za EL na ubalozi wa Sweden mambo yangekuwa magumu.Nilikuwepo kwenye mkutano huo.
 
Hivi kwanini Kina Msekwa walimbeba JK katikao cha chama siku Lowassa alipomhoji kwamba kwanini anakaa kimya yeye akichekwa kwa kosa ambalo ni yeye JK aliemzuia kuifukuza Richmond? Lowassa alimkumbusha siku alimpigia simu na kumweleza kuwa anawafukuza ndipo JK akamkatalia, baada ya kuhojiwa huku JK kijasho kikimtoka wazee wa chama wakaingilia na kumbembeleza Edo

Kosa la Lowassa ni kuingia Mkataba na Richomond sio kutovunja mkataba, Hata kama JK angemruhusu kvunja isingehalalisha kitendo chake cha kuingia mkataba huo, Kosa la kuingia mkataba wa kifisadi lisingehalalishwa kwa kuvunjwa mkataba, Kamati ya MWAKYEMBE ILIMSULUBU KWA KUSHINIKIZA MKATABA!
 
Ninaamini ccm ni vichaa lakini kumsimamisha lowassa watakuwa mazezeta
 
kila m2 anauhuru wa kusema atakavyo ilimradi asivunje sheria, binafsi namuunga mkono kwa nguvu zote mzee Lowassa. 2015 akigombea natamsaidia kwa uwezo wangu wote, ninaamini anauwezo wa kuifikisha Tanzania 'next level' kimaendeleo. LONG LIVE MZEE LOWASSA.
 
Hivi LOWASSA mbona mnamuogopa sana. Sijawasikia mkisifia Wazo lake la Kujenga UDOM. Hata mkifanyaje shule za Secondary za Kata ni hatua kubwa sana.
Wenzetu nyinyi kutoka katika makabila makubwa mmeanza siku nyingi kupata FURSA za elimu kwa upendeleo wa makusudi. BABU zenu wana Degree, Baba, Mama, Bibi wote wamesoma tena kwa upendeleo wa makusudi wa kikanda.
Miaka ya nyuma, Makabila mengine tulikuwa hatuchaguliwi kuingia Secondary ilikuwa wilaya nzima wanachaguliwa vijana watatu kuingia Sekondary. Lakini huko North kwenu wanachaguliwa Darasa zima. Jamani fuatilieni historia. Si kwa Accident watu wa mikoa iliyonyuma hawakusoma. Huo ulikuwa mkakati wao uliofanywa kwa makusudi na baba zao na babu zao ili watutawale vizuri KIELIMU, NA HIVYO KIUCHUMI na sasa wanahangaikia kutawala KISIASA. TUFUATILIE HISTORIA YETU NA HALAFU TULAUMU. Sisi wanzenu tumeshukuru angalau watoto wetu wameweza kusoma kwa miaka 11 shuleni. hivyo wamekuwa na watajua la kufanya. Dar es Salaam ilikuwa na Secondary Saba tu ambazo zilijaza vijana kutoka HUKO HUKO. Na Sekondary za huko kwako zilijaza wanafunzi wa kwao tu, Mithili ya kuongea hata lugha zao shuleni. JAMANI ACHENI KUDANGANYWA. Uliza wazazi wako kwa nini hawakusoma. Jibu ni moja tu WALIKOSA FURSA TU. na wewe umepata FURSA.
 
nimekuona huna maana baada ya kukutana na huu upuuzi wako. huwezi kusema watu wanampa sija feki kikwete. mtu ambaye ameanzia from the scretch na kusimamia kila alichokianzisha mpaka kufikia hapa tulipo na kuona UDOM ikisimama. kuwa na wazo na utekelezaji ni vitu viwili tofauti kabisa. by the way how many mawazo are out there? hata wewe unaweza kuwa na wazo la kujenga kanisa hapo ulipo, na linabaki kuwa wazo tu na halina garama yoyote zaidi ya kuwaza. hivi unajua hata muasisi wa wazo la serikali ya majimbo ni Idd Simba? NAONA MNAJARIBU KUTWIST KILA ZURI ALILOFANYA KIKWETE. SHAME ON YOU.
Good 2015,sorry did u took ur tablets before your meal or not at all!?
 
Atasubiri sn , hakuna mtu aliyekuwa waziri mkuu akawa rais toka tupate uhuru , muulize Raila Odinga kilichomkuta . tupo 45 million tunataka Sura mpya , mawazo mpya . Acha copy & pest

Acha uongo ww!....J.K Nyerere alikua waziri mkuu tulipopata uhuru then later on akawa Rais!
 
Back
Top Bottom