New Barrick Group kuinunua Acacia

New Barrick Group kuinunua Acacia

Punguza mihemuko ili uweze kuelewa kinachosemwa! Ni wapi paliposemwa thamani ya Acacia ni USD 303 Million?!
Soma vizuri hiyo taarifa utapata jibu.

"Once the merger with Randgold is complete, the enlarged group will look for solutions for Acacia, with Barrick favoring taking full ownership of the unit, Bloomberg News said. A 36% stake in the company would be valued at about $303m, based on the closing price in London on October 23, it added".

Baada ya Kampuni ya Barrick Gold kuungana na Kampuni ya Randgold Resources na kuwa kampuni inayoitwa New Barrick Group yenye thamani ya US$18.3 bilioni. Kwa sasa kuna taratibu zinazofanyika ili kuzinunua hisa zilizobakia za Acacia ambazo ni asilimia 36 zenye thamani ya US$303 milioni kwa hesabu iliyofanya Jumanne wiki hii.

Bado hujaelewa?
 
Baada ya Kampuni ya Barrick Gold kuungana na Kampuni ya Randgold Resources na kuwa kampuni inayoitwa New Barrick Group yenye thamani ya US$18.3 bilioni. Kwa sasa kuna taratibu zinazofanyika ili kuzinunua hisa zilizobakia za Acacia ambazo ni asilimia 36 zenye thamani ya US$303 milioni kwa hesabu iliyofanya Jumanne wiki hii.

‘’Baada ya kukamilisha kazi ya kuziunganisha kampuni za Barrick Gold na Randgold Resource, tutakaa na Acacia na Serikali ya Tanzania ili kumaliza tofauti zilizopo’’, Alisema Mark Bristow ambaye kwa sasa ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa New Barrick Group.

Acacia ilinukuliwa ikisema kuwa ilikuwa ikisubiri kupewa taarifa rasmi na Barrick kuhusu mazungumzo yake na serikali ya Tanzania.

Serikali ya Tanzania imekataa kukutana na Acacia kutokana na suala la ukwepaji wa kodi.

"Kama ilivyoshauriwa hapo awali, Barrick bado haijaipa Acacia mapendekezo ya ufumbuzi kamili wa migogoro ambayo Barrick ameweza kukubaliana na Serikali ya Tanzania licha ya majadiliano yao ya moja kwa moja yalifanywa mnamo Oktoba 2017," ilisema Acacia.

Katika mahojiano na Globe and Mail mnamo Septemba John Thornton, mwenyekiti mtendaji wa Barrick Gold, alisema Acacia "hakuwahi kulipia kodi ya mapato" kwa serikali ya Tanzania na njia bora ya kukabiliana na tatizo hili ilikuwa kupitia majadiliano na serikali.

Mkurugenzi Mtendaji wa Randgold Resources ambaye kwa sasa ni Mkurugenzi Mkuu wa New Barrick Group, Mark Bristow aliliambia gazeti la Miningmx mnamo Oktoba 1 kwamba alikuwa na nia ya kuwekeza Tanzania. Alisema, "Je, sisi, kama Randgold, tunaenda Tanzania? Kabisa. Je! Tumefanya kazi na serikali ya Tanzania kama Randgold? Ndio, tumefanya "alisema.

Habari kwa lugha ya Kiingereza:


SOURCE: Bloomberg and Financial Times newspaper.
Sawa,tunataka vitendo sio maneno,mkono mtupu haulambwi.We are waiting.
 
Soma vizuri hiyo taarifa utapata jibu.

"Once the merger with Randgold is complete, the enlarged group will look for solutions for Acacia, with Barrick favoring taking full ownership of the unit, Bloomberg News said. A 36% stake in the company would be valued at about $303m, based on the closing price in London on October 23, it added".

Bado hujaelewa?
Wewe ndo hujaelewa na ndio maana nikakuambia punguza mihemuko, soma kwa vituo ili uelewe! Hiyo $303M ni thamani ya 36% ya hisa za Acacia na sio thamani yote ya Acacia kama unavyodai.
 
Wewe ndo hujaelewa na ndio maana nikakuambia punguza mihemuko, soma kwa vituo ili uelewe! Hiyo $303M ni thamani ya 36% ya hisa za Acacia na sio thamani yote ya Acacia kama unavyodai.
Sasa kwani hisa maana yake ni nini?
Hisa ni kiasi cha ownership ya shirika husika. Tunaposema Acacia ana hisa 36% kwenye kampuni ya Barrick Gold Mines, tunamaanisha anamiliki 36% ya mali ya Barick Gold Mines. Sasa 36% ya Barrick Gold Mines kama ndiyo umiliki wa Acacia kwenye Barrick kama ni just USD 303 hata mimi na wewe 'we can buy them off"!

By simple mathematics:
If 36% = 303 million (Acacia shares)
64% = ? million (New Barric Group shares)

Hiyo ? by cross multiplication haiwezi kuwa 18.3 billion! Hata billion moja haifiki.
 
Sasa kwani hisa maana yake ni nini?
Hisa ni kiasi cha ownership ya shirika husika. Tunaposema Acacia ana hisa 36% kwenye kampuni ya Barrick Gold Mines, tunamaanisha anamiliki 36% ya mali ya Barick Gold Mines. Sasa 36% ya Barrick Gold Mines kama ndiyo umiliki wa Acacia kwenye Barrick kama ni just USD 303 hata mimi na wewe 'we can buy them off"!

By simple mathematics:
If 36% = 303 million (Acacia shares)
64% = ? million (New Barric Group shares)

Hiyo ? by cross multiplication haiwezi kuwa 18.3 billion! Hata billion moja haifiki.
Are you serious?! We been discussing Barrick-Acacia stuff for almost a year now!! Ina maana kweli hapo juu ndio uelewa wako kuhusu hizi kampuni?!
 
The problem ni kwamba, kwa mazingira hayo ina maana tutalazimika kutumia audited finacial reports ambazo tayari nimeshataja hapo juu zinaonesha nini! Hizo dividends wanazolipwa wanahisa na zenyewe taarifa zake zipo kwenye hizo hizo audited financial reports ambazo hatuwezi kuzikwepa!

Hizi financial reports nimekuwa nikizisoma mara kwa mara... kwa mfano, 2012 to 2016 Financial Report ya Barrick Gold (Acacia ikiwa ndani) ni hii:
View attachment 910522

Nadhani unaona kama tutatumia financial reports tutakwama wapi! Hiyo inaonesha Gross Profit kwa miaka 4 mfululizo na ni mwaka mmoja tu ndipo gross profit ilifika angalau USD 5 Billion!

Kama ndivyo, tukiamua kuchukua mkondo huo, itakuwa imekula kwetu kwa 100% kwa sababu, ripoti hiyo ya Barrick ina-reflect what Acacia walichokuwa wanapata na kutulipa na kwahiyo itakuwa case closed... hatuna chetu!!

Lakini kama uchunguzi wa akina Mruma ungekuwa inclussive, ukiwahusisha na Acacia wenyewe, mosi, ndo kama nilivyosema hapo awali, Acacia wasingekuwa na grounds za kuikataa ripoti ya Mruma!

Na kama wasingekuwa na grounds za kuikataa, serikali kwa upande wake ingekuwa kwenye nafasi ya ku-discredit hizo financial records za akina Barrick kwa sababu, findings za serikali na Acacia wenyewe, zingekuwa zinaonesha udanganyifu mkubwa kwenye kiwango cha madini kwenye makinikia. Kama wote wame-confirm udanganyifu kwenye viwango vya madini, ina maana any financial reports zilizotokana na udanganyifu huo, na zenyewe credibility yake inakuwa questionable!

And remember, issue hapa haitakuwa kuiamini au kutoiamini report ya akina Mruma bali credility ya report yenyewe ambayo ndiyo zao la madai yetu! And to be honest, naogopa hizi sana hizi merger na acquisition za akina Barrick manake tusipokuwa cautious, tutashitukia tunayemdai doesn't exist!

Unaweza kuja kushitukia mwisho wa siku mmiliki mpya alinunua only assets za mdaiwa wetu ambae doesn't exist anymore and not her liabilities!
Kweli mku hapa watatuchezea kamuchezo kanunua only Assets sio Liabilities za kampuni ya Accacia na hapo ndo unasikia mtu anasema tufunge vilago turudi kwetu maana anaedaiwa hayupo tena.

Lakini serikali ikiwa makini sasa nikuangalia the way forward kuhusu haya makinikia. Kuwepo na mkataba special for makinia mgao wa hawa makonteina uwekwe kwenye contract tunagawaneje kila konteina linalopelekwa kuuzwa?

Naona makinikia yana deal kwasababu jama hawa wazungu walichang'achikiwa kuwakataza makinikia. Mbona kwenye Madini-Dhahabu yenyewe wako kimya hawapigi kelele?
 
Kweli mku hapa watatuchezea kamuchezo kanunua only Assets sio Liabilities za kampuni ya Accacia na hapo ndo unasikia mtu anasema tufunge vilago turudi kwetu maana anaedaiwa hayupo tena.

Lakini serikali ikiwa makini sasa nikuangalia the way forward kuhusu haya makinikia. Kuwepo na mkataba special for makinia mgao wa hawa makonteina uwekwe kwenye contract tunagawaneje kila konteina linalopelekwa kuuzwa?

Naona makinikia yana deal kwasababu jama hawa wazungu walichang'achikiwa kuwakataza makinikia. Mbona kwenye Madini-Dhahabu yenyewe wako kimya hawapigi kelele?
Issue ndo sana hii na hapa ndipo ninaposhindwa kuielewa serikali! Haya makinikia tunayohangaika nayo ni sehemu tu ya kile ambacho ndicho haswa tulitakiwa kufanyia kazi!

Sio kwamba hakuna utajiri kwenye makinikia lakini utajiri mkubwa bado upo migodini na hautokani na makikinia. Kati ya migodi yote Tanzania, ni migodi miwili tu ndiyo inayozalisha makinikia ambayo uchenjuaji wake unafanyika nje ya nchi lakini uchenjuaji wa aina nyingine yote unafanyika Tz.

Ni kutokana na hilo ndio maana hapo juu nikashauri kama serikali wapo serious basi ifanyike special minerals audit kwa kampuni zote za uchimbaji madini badala ya kuhangaika na makinikia peke yake! Wakati tunahangaika na makinikia, wala sijasikia mpango wa makusudi wa kuhakikisha ikiwa madini yanayokuwa declared ndio hasa yanayozalishwa!

Geita Gold Mine kwa mfano... takwimu zinaonesha ndie mzalishaji mkubwa wa dhahabu nchini! Swal ni je, kiwango kinachorekodiwa ndio hasa kinachozalishwa na GGM? Viwango vinavyorekodiwa na kampuni zingine including Acacia ndio hasa vinavyozalishwa?

Sasa basi, cha kufanya ni serikali kuunda timu ya watu ambao inawaamini sio corrupt. Na kila kampuni ya madini iwe na watu wake inaowaamini kwamba sio corrupt! Baada ya hapo ndipo ifanyike hiyo special mineral audit itakayowahusisha pande zote mbili! Hata haya makinikia nayo yanakuwa audited na watu toka pande zote mbili!

Matokeo tutakayopata hapo ndiyo yatatupa base ya nini tunatakiwa kudai and way forward. Tukiweka uzalendo fake pembeni, hawa Acacia wana haki ya kuikana ripoti ya Professor Mruma kwa sababu hawakuhusishwa!

Ni nani anaweza kukubali uchunguzi wa upande mmoja? Na serikali wanalazimika kuwa wapole kwa sababu nadhani hatimae na wenyewe wamegundua kwamba walifanya kosa kufanya uchunguzi wa upande mmoja! Na hili suala niliongea sana tangia day one lakini watu walikuwa wanakejeli lakini hatimae nadhani na wenyewe wameanza kuona ni wapi tulikosea!
 
Mazungumzo yanayoongozwa na prof kabudi yamefikia wapi?

Nani atakae lipa zile trillion?

Sarakasi na ngonjera
 
Tundu Lissu aliyesema haya haya!

Tumezuia makinikia lakini bado wanatupiga kwenye mawe yenyewe:

Financial Times wanasema:

Despite its political challenges, Acacia has performed strongly this year despite not having underground gold production from Bulyanhulu, its flagship mine, which was mothballed last year following an export ban on mineral concentrate from the mine, and that of Buzwagi.

Kwa hiyo juhudi na Magufuli na Waziri Kabudi na maprofessa wao na propaganda zao hazijazaa matunda yeyote. Lakini kwa wananchi wa vijijini huko ukiwaambia nimezuia makontena inatosha, ukija kwa watu wenye uelewa wanadai facts and figures, takwimu. Kuna sababu ya kwa nini wamepiga marufuku takwimu, sio wajinga hawa watawala, wanajua kutawala werevu kati ya wajinga.
 
Back
Top Bottom