Nimecheka kama nilikuwepo!!Kuna mzungu moja juzi akasema hivi "deni analodai Magufuli kwa Accacia ni Trip ya kwenda mwezini na kurudi" nilicheka sana. Lakini yote tisa ukweli mchungu ni kwamba hili deni haliwezekaniki kulipwa kabisa. Kibaya zaidi upande wa Serikali kumeshatokea mkanganyiko mkubwa sana kwenye TAKWIMU.
Nadhani njia pekee na ya kuweza kwenda mbele vizuri ilikuwa ni kupitia upya hii mikataba katika Sovereign Right ili kuzuia upigaji mwingine. Ila hii ya kuendelea kusaka wachawi sidhani kama itafanikisha kitu.
Mkuu Malcom, endapo serikali na timu yake wangekuwa makini na kuweka pembeni mihemuko, hili la mkanganyiko wala lisingetokea na kama lingetokea basi ungekuwa ni mkanganyiko unaokubalika hata kisayansi kwa sababu margin error ingekuwa within or not VERY VERY far from acceptable limit!
Unapoleta findings ambazo error ni above 100% hicho ni kiroja unless kama umejiandaa vya kutosha ku-defend hizo findings ambazo zina-underestimate all past findings duniani!
A moment Profesa Mruma alipotoa ile ripoti ya kwanza, nikazichakata data zake kisha nikaingia kwenye WORLD KNOWN DATA!
Hapo nimeandika kwa msisitizo kwa sababu nilijua no matter what, kuwa na logical demand ni lazima demand hiyo iendane na takwimu zinazofahamika duniani kinyume chake, tutatakiwa ku-prove otherwise!
Ilinichukua less than 30 minutes tangu wakati Mruma asome ile ripoti kugundua kwamba, kama ripoti yake ni sahihi basi maana yake Tanzania itakuwa among top 3 world gold producers wakati takwimu za dunia zinaonesha hatupo hata among top 10 !!!
Inawezekana ni kweli tupo among top 3 against world known statistics lakini hizo ni new findings known nowhere else except kwenye makarabrasha yetu au ya wale "wanaopika takwimu za uzalishaji dhahabu duniani"
Mbaya zaidi, wakati ripoti ile ingemaanisha world gold production statistics hazipo sahihi, ripoti yenyewe tulikuwa tumeiandaa wenyewe bila kushirkisha upande wa pili! Kwamba, tunatarajia ku-argue against official world gold statistics kwa kutumia data tulizotengeneza wenyewe not from new geological findings but from makontena ya makinikia!
Kuja ripoti ya Profesa Mrosso na USD 190 Billion, nikakuta hata Market Cap ya Barick Gold yenye kampuni 7 ndani yake including Acacia, haifiki hata $40 Billion (at least kwa wakati ule). Ukija kwenye annual revenue ya Barrick Gold yenye kampuni 7 ndani yake ilikuwa haifiki hata $10 na net income haifiki hata $ 5 Billion.
Kinyume chake, ilikuwa ukitafsiri ripoti ya Profesa Mrosso, unakuta Acacia peke yake walikuwa wanatuibia annual tax ya about USD 4 Billion... hiyo ni kodi tu!! Kama kodi ingekuwa ni 40% ya mapato, ina maana mapato ya Accacia peke yake ni USD 10 Billion!
Kwamba, mapato ya Acacia peke yake yanazidi mapato yote ya Barrick Gold ambayo ndani yake kuna hiyo Acacia!
Argument yetu ilikuwa simple and clear kwamba, "hizo takwimu za akina Barrick ni za uongo kwa sababu ni wezi!" Na inawezekana kabisa kwamba ni za uongo lakini tulisahau kwamba, kisheria hizo hizo takwimu za uongo ndizo zitakazotumika kwa sababu ndizo official financial statisticts zinazotumika hata kwenye masoko makubwa duniani kama New York and London Stock Exchange including NASDAQ!
Tahadhali yangu hapa ilikuwa, tusipojua tunadai nini basi itakuwa ngumu sana ku-defend madai yetu. Na haya yalitokea kwa sababu zoezi zima lilitawaliwa na mihemuko ya kisiasa!