The Zanzibar Echo
JF-Expert Member
- Apr 21, 2025
- 490
- 836
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema Kundi la Wanamgambo wa Kipalestina la Hamas linatafuta mabadiliko "yasiyokubalika" kwa pendekezo jipya la kusitisha mapigano huko Gaza Ukanda.
Netanyahu amenukuliwa na Shirika la Habari la DPA, akisema mabadiliko ambayo Hamas inataka kuyafanya katika pendekezo la Qatar yaliofikishwa kwao usiku wa jana hayakubaliki kwa Israeli. Maafisa wa Hamas waliiambia DPA kuwa bado kuna haja ufafanuzi kuhusu kuendelea kwa usitishaji mapigano baada ya kipindi cha awali cha siku 60, kuondolewa kwa wanajeshi wa Israel Gaza na upatikanaji wa misaada ya kibinadamu katika eneo hilo pasina vikwazo.
Mazungumzo hayo yanayoratibiwa na Qatar, Misri na Marekani yanalenga kufanikisha makubaliano ya kusitisha mapigano kwa siku 60 huko Gaza na kuachiliwa kwa mateka ambao bado wanashikiliwa na Hamas, na baadhi ya wafungwa wa Kipalestina wanaoshikiliwa na Israel.
Netanyahu amenukuliwa na Shirika la Habari la DPA, akisema mabadiliko ambayo Hamas inataka kuyafanya katika pendekezo la Qatar yaliofikishwa kwao usiku wa jana hayakubaliki kwa Israeli. Maafisa wa Hamas waliiambia DPA kuwa bado kuna haja ufafanuzi kuhusu kuendelea kwa usitishaji mapigano baada ya kipindi cha awali cha siku 60, kuondolewa kwa wanajeshi wa Israel Gaza na upatikanaji wa misaada ya kibinadamu katika eneo hilo pasina vikwazo.
Mazungumzo hayo yanayoratibiwa na Qatar, Misri na Marekani yanalenga kufanikisha makubaliano ya kusitisha mapigano kwa siku 60 huko Gaza na kuachiliwa kwa mateka ambao bado wanashikiliwa na Hamas, na baadhi ya wafungwa wa Kipalestina wanaoshikiliwa na Israel.