platozoom
JF-Expert Member
- Jan 24, 2012
- 9,365
- 11,151
Platozoom,
Nakubaliana na mengi uliyoyaandikia, nyongeza hapa ni hii; hapa mtongozwaji kwa mara ya kwanza anakabiliwa na mazingira mapya katika kutongozwa kwake. Zamani aliweza ' kumdengulia' mtongazaji kama hakumpenda,lakini sasa mtongozwaji anaweza kujikuta anakosa mwana na maji ya moto. Na kuna maisha ya kisiasa ambayo mtongozwaji anayahitaji kuyaishi hata baada ya ' Vita ya leo'.
Maggid
Maggid umenichekesha: "kuyaishi maisha mapya"? Mimi nafikiri kwa kujali mustakabali wa yajayo ni vyema mtongozwa akajitathmini kwanza kama hayo maisha anayahitaji kwa ajili ya hatma yake au ni adabcadabra ama upepo tu unapita.
Na hata kama atagundua hayo ndiyo maisha anayohitajika kuyaishi ni vyema baada ya tathmini akayaweka kwenye mizania na mtazamo wake hata kama mwenye "dhana" ni mwingine, ili huko mbele y safari aseme naam nilifanya maamuzi yangu hata kama nimekosea, na najisahihisha (kumbuka mwalimu Nyerere aliandika tujisahihishe)