Neno la Faraja kwa Joyce Kiria

Neno la Faraja kwa Joyce Kiria

Lugulu

JF-Expert Member
Joined
Mar 27, 2013
Posts
482
Reaction score
176
Joyce!!! Leo ni siku ambayo hutakaa kuisahau maishani mwako. Nasema hivi kwa sababu jana tu ndo umetoka Tabora kumwona rafikiyo wa karibu sana, namanisha mmeo. Leo tena tena kupitia hapa JF tunajuzwa habari ya msiba wa babako, Pole sana dadangu... Kuna mambo mawili nataka yakufariji; 1. Mungu anaweza kuonekana zaidi wakati wa furaha na aman na wakati wa shida asionekane kabisa. Hapa nina maana kwamba Mungu yupo pamoja nasi kila wakati ila tunapokuwa na furaha na amani yeye huwa pembeni yetu na ndiyo maana unamuona, lakini tunapokuwa na woga au kupita ktk shida na majaribu yeye hutuchukuwa na kutufunika na uwepo wake na ndiyo maana hatumuoni. So, hupaswi kuogopa chochote kwani yeye atakuvusha kwenye bonde la uvuli (Zaburi 23:1-6). 2. Joyce, kila jambo linalotokea hapa dunian liwe zuri au baya, iwe furaha au huzuni fahamu kuwa Mungu karuhu. Mungu ndiye ajuaye sababu. Umesikia habari ya Ayubu, ndo maana tumeagizwa kushukuru kwa kila jambo... 3. Mwisho, ucmtafute mtu yeyote juu wakati huu ila MUNGU pekee. MANGU NA AKUSAIDIE
 
Mtihani juu ya mtihani, tupo pamoja na wewe kimaombi, M/Mungu akizidishie subra
 
Pole sana joyce kiria. Haijalishi unapiyia mitihani gani, huu ni wakayi wa kujihakikishia wewe ni mwanamke jasiri kiasi gani. Kamzike baba, Mungu akutie nguvu ili next hearing usikose. Huu ndio wakati wa kusimama ukahesabiwe, kama mke na kama binti. Taji utaipata usipozimia moyo. Kila la kheri dada.
 
Mungu ndio ajuaye kesho yetu
Leo manyang'au ya CCM yanapandikiza kesi za uongo kwa makamanda kama makaburu ya Afrika Kusini yalivyofanya dhidi ya wapigania Uhuru, kamwe tusife moyo ushindi mwisho ni wetu nao watatafuta pa kujificha ni suala la muda tu na wanalijua hili
 
Pole sana dada na mtani wangu nakuombea upate nguvu ktk kipindi hiki kigumu. Tupo pamoja kwenye dua zetu Mola akipe nguvu upite salama kwenye hii mitihani. pole sana dada yetu jikaze tupo pamoja.
 
Rudi kwa mumeo dada. Mungu ni mwenye huruma atakusamehe.
 
Rudi kwa mumeo dada. Mungu ni mwenye huruma atakusamehe.
Una maana arudi kule Tabora gerezani kwa mumewe, itasaidia nini?
Pole Joyce. Kaa ukijua kuwa kuna binadamu kama wewe ambao pia hupata madhila, tena makubwa hata kupita ya kwako.
 
Yatasemwa mengi ila before success there must be a way to pass through!!..pole sana Dada Joyce Kiria Dua yangu ni ujaliwe faraja hata katika wakati huu
 
Joyce Kiria hiki ni kipindi chako kigumu cha kupimwa imani yako, unatakiwa shinde. Nina neno dogo kwako, Kwa kipindi hiki jihadhari zana na media zote, (nasisitiza zote kuanzia mitandao ya kijamii) tulia na familia yako na jikite zaidi ktk imani na kutafakari matatizo yako. Media zinamuinua mtu na kwa ajabu sana zinambomoa mtu zikamtia mfadhaiko (Tuliyashuhudia kwa Amina Chifupa)
 
mitihan ya dunia inapita. unapoona mambo magumu usikate tamaa ujue mambo mazuri yanakuja cha muhimu kusali na kushukuru mungu. dada mwenyez mungu akupe ujasiri kwenye kipind iki kifup cha mpito. mungu ailaze roho ya baba pema pepon amen.
 
Pole sana Dada.Mungu akutie nguvu katika kipindi hiki kigumu.

Sent from my BlackBerry 9380 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom