Tango73
JF-Expert Member
- Dec 14, 2008
- 2,128
- 1,225
HIli neno "huyu anakubalika" ni neno la kitapeli ambalo lengo lake ni kumtaka mtu ampigie kura au ampende mtu ambaye hana sifa za kutawala au kuwa mbunge. Utakuta mtu anakuambia au uvumi unaenea mitaani kuwa , mtu "huyu anakubalika", lakini hata mara moja huambiwi sifa za mtu huyo katika Jamii na mafanikio yake.
Watanzania tusipokuwa makini na usemi huu wa kishetani wa" mtu huyu anakubalika" tutazidi kupata matapeli wa kisiasa wa kuendesha nchi hii na ambao watatucheleweshea maendeleo. Mkoa wa Ruvuma unaongoza hapa tanzania kwa kutumia usemi usemi huu wa "Huyu anakubalika kichama" bila kutaja sifa za mgombeaji.
Mgombeaji wa uraisi au mbunge lazima achambuliwe ki undani sifa zake zote za kijamii na elimu. Hata kama aliwahi kuvuta bange au kubaka msichana , lazima zianikwe ili watu wamfahamu kwa undani maisha yake ya kiadilifu. Utakuta mtu anagombea uraisi au Ubunge, lakini ofisini kwake , kalala na mke wa mtu, kazaa nje ya ndoa, kaiba kiwanja na kujenga nyumba katika viwanja vya kuchezea watoto na haja retire Imprest nne, wewe unategemea nini kama mtu huyu akiukwaa ubunge au Uraisi?
Sasa madhala ya neno , mtu huyu anakubalika yanapoficha maovu ya mgombea Ubunge au Uraisi yanapojitokeza.
Jamani watanzania tukue na kukomaa kiakiri na kuachana na maneno ya kitapeli ya kisiasa ya enzi za Ujamaa na kujitegemea.
Watanzania tusipokuwa makini na usemi huu wa kishetani wa" mtu huyu anakubalika" tutazidi kupata matapeli wa kisiasa wa kuendesha nchi hii na ambao watatucheleweshea maendeleo. Mkoa wa Ruvuma unaongoza hapa tanzania kwa kutumia usemi usemi huu wa "Huyu anakubalika kichama" bila kutaja sifa za mgombeaji.
Mgombeaji wa uraisi au mbunge lazima achambuliwe ki undani sifa zake zote za kijamii na elimu. Hata kama aliwahi kuvuta bange au kubaka msichana , lazima zianikwe ili watu wamfahamu kwa undani maisha yake ya kiadilifu. Utakuta mtu anagombea uraisi au Ubunge, lakini ofisini kwake , kalala na mke wa mtu, kazaa nje ya ndoa, kaiba kiwanja na kujenga nyumba katika viwanja vya kuchezea watoto na haja retire Imprest nne, wewe unategemea nini kama mtu huyu akiukwaa ubunge au Uraisi?
Sasa madhala ya neno , mtu huyu anakubalika yanapoficha maovu ya mgombea Ubunge au Uraisi yanapojitokeza.
Jamani watanzania tukue na kukomaa kiakiri na kuachana na maneno ya kitapeli ya kisiasa ya enzi za Ujamaa na kujitegemea.