Nenda tu CCM, sitakukumbuka wala kukuchagua daima

Nenda tu CCM, sitakukumbuka wala kukuchagua daima

bodaboda2

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
872
Reaction score
231
Nenda tu CCM sitakukumbuka daima, umesababisha shida zote za nchi hii wakati wewe ukineemeka na familia yako, huku watoto wako wanasoma Australia wa kwangu st. Kayumba tena anakaa chini bila hata uji wa Dona!!

Wewe na family yako unatibiwa nje ya nchi Mimi Baba yangu kalazwa muhimbili chini, dawa hamna!! Dr anamwangalia mwenye nacho ndiyo hamtibie, nitakuwa zuzu number 1 kuendelea kukukumbatia CCM, uliyeiba EPA, ESCROW, MEREMETA, uliyeiba kupitia Rada huku Mimi mnyonge nataabika maisha magumu wewe umeficha madolari Uswisi unakula vizuri na familia yako!!

Ulikuta dolla inauzwa Tzs.650, leo hii inaiuzwa Tzs.2200...nenda tu CCM!

-Ulikuta sarafu kibao, Tsh.5, 10, 20, leo hii hazipo tena..nenda tu CCM!

-Ulikuta nauli nalipa Tsh.250, leo hii nalipa 450...Nenda tu CCM!!

-Ulikuta pipi kali namumunya kwa Tsh.10 kila ki1, leo hii Tsh.300...nenda tu CCM!!

-Ulikuta soda nakunywa Tsh.300 leo hii
Tsh.600, hata mgeni hanunuliwi soda nenda tu CCM!!

-Wakati unakuja kitumbua kilikuwa Tsh.20 tu, leo hii Tsh.200,cnywi chai tena nikashiba...nenda tu CCM!

-Ulikuta sukari Tsh.400 tu, leo hii Tsh.2000..nenda tu CCM ya vibaka!

-Ulikuta fungu la nyanya Tsh.100 tu, leo hii Tsh.500-1000..nenda tu CCM (chama cha kinachofuga mafisadi)!

Ulikuta bia Tsh.800 leo hii
Tsh.2500 nenda tu CCM (chama cha majizi).!!

-Ulikuta sigara Tsh.50 leo hii
Tsh.200

-Ulikuta mchele Tsh.800 leo hii Tsh.1800..nenda tu CCM (chama cha majambazi)!!

-Nakuchukia CCM maana hauna tofauti na shetani

-Naona wengi wanakitaka kiti chako ila kwa kuwa nimeshagongwa na nyoka nikiona rangi ya kijani nashtuka....!!!

Nenda tu CCM, tuachie nchi yetu. Umekuwa ukidhulumu haki za wanyonge, kuuwa watu wanaotetea haki zao, kuiba Mali ya umma, kupindisha sheria ili isikutie hatiani!! Mnaiba wanyama wetu,pembe za ndovu na meno ya tembo na kuziuza kwa wazungu!!

Umekuwa ukisign mikataba mibovu ya madini na gesi ili wanyonge tuendelee kutaabika, wewe ukineemeka na familia yako! Pole CCM sina budi kukukataa sasa
 
CCM tumeshaichoka kupita kiasi na ife tu kwa kuwa hakuna namna ya kukisaidia wakati chenyewe kimeshindwa kujisaidia.
 
Ccm nenda nenda usirudi
kusoma shule ya serikali ilikua ni heshima mtaani siku hizi ndio unaonekana ni masikini huku mtaani nenda nenda labda utajifunza
 
kufa kufa ccm usirudi tena, unasamehe kodi makampuni ya madini na mengine makubwa, mi napikaga rangi tu, kibanda changu kidogo cha saloon TRA washafika wanataka kodi! kufa kufa ccm usirudi tena
 
Kufa ccm nilikua nilienda slkoni na sh elfu kumi nanurudi nyumbani na vitu kibao leo elfu kumi hata boxer hainunui.
 
kufa kufa ccm usirudi tena, unasamehe kodi makampuni ya madini na mengine makubwa, mi napikaga rangi tu, kibanda changu kidogo cha saloon TRA washafika wanataka kodi! kufa kufa ccm usirudi tena
Hawa sio watu Ni mafisi
 
Ulikuta tuna viwanda vingi, huku vingine vikiwa tishio Africa mfano General Tyres leo yamebaki magofu ya majengo huku ukosefu wa ajira ukizidi kuwa mkubwa. Kufa kufa ccm hustahili kuishi tena.

ulikuta watanzania tunashirikiana na kupendana leo mtoto wa mkuu anasubutu kutangaza rais hawezi kutoka kanda flani huku viongozi wa chama wakinyamaza kimya pasipo kukemea ubaguzi huo. Kufa kufa ccm.

Ulikuta shule za serikali zikiwa zinaongoza kwa ufaulu shule kama Ilboru, msalato hazikuacha kutoa top 10, leo imebaki kuwa historia. Kufa kufa ccm, hutanuka, nitakupa msaada wa kukuzika bure.
 
Kufa kufa ccm, historia yako itabaki naahidi kuwahadithia wajukuu zangu maovu na maangamizi yako. Wasije iga uovu wako wakaangamia.

sitaacha kuwahadithia jinsi ulivyotugeuza na kutufanya maskini ngali tulikuwa na mali hasili nyingi. Naapa nitawaeleza tamaa zako, jinsi ulivyokuwa mbaguzi, kama ww sio mtoto wa mkubwa sahau nafasi kubwa serikalini. Nitawaeleza jinsi Nyerere alivyompendekeza mwandishi wake kuwa rais, jinsi mwinyi alivyo msaidia kikwete kuwa waziri na sio hilo tu sitawaficha jinsi kikwete alivyo rudisha utu kwa kumpa mtoto wa Mwinyi uwaziri, sintaacha kuwaambia jinsi kikwete alivyo mpendekeza magufuli mwanasiasa asiye na mvuto na jinsi ambavyo magufuli anapaswa kuwa na utu kwa kumpa uwaziri ridhiwani. Nitawaeleza wajukuu zangu katikati ya mipango hiyo miovu ccm iliangushwa na Ukawa. Lazima wajukuu zangu watacheka na kufurahia kifo cha ccm.
 
NENDA TU MJOMBA:
Ulikuta dolla inauzwa Tzs.650, leo hii inauzwa Tzs.2200...
Nenda tu mjomba!
-Ulikuta sarafu kibao, Tsh.5, 10, 20, leo hii hazipo tena..
Nenda tu mjomba!
-Ulikuta nauli ya daladala mjini Tsh.250, leo hii 450...
Nenda tu mjomba!!
-Ulikuta pipi kali namumunya kwa Tsh.10, leo hii Tsh.50-100..
Nenda tu mjomba!!
-Ulikuta soda nakunywa kwa Tsh.300 leo hii Tsh.600, hata mgeni hanunuliwi soda...
Nenda tu mjomba!!
-Wakati unakuja kitumbua kilikuwa Tsh.20 tu, leo hii Tsh.200,cnywi chai tena nikashiba...
Nenda tu mjomba!
-Ulikuta sukari Tsh.400 tu, leo hii Tsh.2000..
Nenda tu mjomba!
-Ulikuta fungu la nyanya Tsh.100 tu, leo hii Tsh.500-1000..
Nenda tu mjomba!
Ulikuta bia Tsh.800 leo hii Tsh.2500...
Nenda tu mjomba!!
-Ulikuta sigara Tsh.50 leo hii Tsh.200..
Nenda tu mjomba!!
-Ulikuta mchele Tsh.800 leo hii Tsh.2000..
Nenda tu mjomba!!
-Ila nakusifu kwa kupiga lami feki ya 10% baadhi ya barabara ili maisha yakitushinda mjini turudi kijijini kirahiiiiiiisi kidogo!!!!!
-Naona Ukawa wanaenda kaa kwenye kiti chako ila kwa kuwa nimeshagongwa na nyoka nikiona rangi ya kijani nashtuka....!!!
NENDA TU MJOMBA!!
 
Kweli Watanzania Wameshagogwa na Nyoka ndio Maana Wale Jamaa Wanavaa Nguo za kijani Wakionekana Mchana Mtaani Wanakuwa

Kama Bundi Kwa Kuzomewa. Hadi Sasa Wameonelea Waombe Msaada Polisi. CCM Haifai Eti!!!
 
Alikuta tunabangaiza hivyo hivyo lakini katuacha na kipindupindu!
 
Alitukuta na Babu Seya wetu akiwa anatuburudisha kwa Music wake mzuri lakini leo yupo jela kwa fitina zake.
 
Hii single hii, itaua mtu kwa presha.
 
NENDA TU MJOMBA:Ulikuta dolla inauzwa Tzs.650, leo hii inauzwa Tzs.2200...Nenda tu mjomba!-Ulikuta sarafu kibaoh, Tsh.5, 10, 20, leo hii hazipo tena..Nenda tu mjomba!-Ulikuta nauli ya daladala mjini Tsh.250, leo hii 450...Nenda tu mjomba!!-Ulikuta pipi kali namumunya kwa Tsh.10, leo hii Tsh.50-100..Nenda tu mjomba!!-Ulikuta soda nakunywa kwa Tsh.300 leo hii Tsh.600, hata mgeni hanunuliwi soda...Nenda tu mjomba!!-Wakati unakuja kitumbua kilikuwa Tsh.20 tu, leo hii Tsh.200,cnywi chai tena nikashiba...Nenda tu mjomba!-Ulikuta sukari Tsh.400 tu, leo hii Tsh.2000..Nenda tu mjomba!-Ulikuta fungu la nyanya Tsh.100 tu, leo hii Tsh.500-1000..Nenda tu mjomba!Ulikuta bia Tsh.800 leo hii Tsh.2500...Nenda tu mjomba!!-Ulikuta sigara Tsh.50 leo hii Tsh.200..Nenda tu mjomba!!-Ulikuta mchele Tsh.800 leo hii Tsh.2000..Nenda tu mjomba!!-Ila nakusifu kwa kupiga lami barabara zote ili maisha yakitushinda mjini turudi kijijini kirahiiiiiiisi kabisa!!!!!-Naona wengi wanakitaka kiti chako ila kwa kuwa nimeshagongwa na nyoka nikiona rangi ya kijani nashtuka....!!!NENDA TU MJOMBA!!”9Ù9”9Ù9”9Ù9
 
Back
Top Bottom