Nembo ya Taifa letu - Bibi na Bwana - ibadilishwe!!!

Nembo ya Taifa letu - Bibi na Bwana - ibadilishwe!!!

Mwanamayu

JF-Expert Member
Joined
May 7, 2010
Posts
11,701
Reaction score
6,936
hqdefault.jpg


Mambo yafuatayo yamenifanya kupendekeza kubadilishwa kwa nembo hii ya Taifa letu:
1. Hivi hayo mavazi ndio ya Taifa? Kwa hiyo wadada na wamama wakivaa gauni kama la huyo mwanamama kwenye ngao ni sahihi?
2. Huyo mwanaume kushoto, hiyo nguo aliyovaa inaitwaje? Mimi naona kama gauni vile!! Maanake design yake ni kama haina tofauti na ya yule mwanamama upande wa kulia!!!
 
Acheni kuanza kutindua historia ninyi. Ulizeni kwanza wazee wa Tanganyika, siyo mnakurupuka tu na hisia zenu za kukosa mada minaanza kuleta uharibifu hapa.
 
Halafu naona pia kama kuna promotion ya meno ya tembo! Kwa nini wasingeweka tembo mzima!!
 
kweli kabisa hiyo gauni aliyovaa jamaa waitoe maana hana tofauti na shoga... bora hata angetupia kipensi matataa huku akiwa kifua wazi sio hiyo gauni

plz govn change this!
 
hiyo nembo haijatambulisha utamaduni wala desturi ya watanzania hapo...ipo tu kma picha..!!
 
Kila mtu akija na hisia zake si kila kitu kitabadilishwa?,we kiache ti kama unavyokiona
 
Acheni kuanza kutindua historia ninyi. Ulizeni kwanza wazee wa Tanganyika, siyo mnakurupuka tu na hisia zenu za kukosa mada minaanza kuleta uharibifu hapa.

Ni lini umepita lumumba kwa mara ya mwisho. Tukikubaliana awekwe fisi sawa tu!!!
 
Kwa nini karafuu na sio korosho,
Kwa nini karafuu na sio pamba,
Kwa nini karafuu na sio alizeti,

Naunga mkono hoja, tuibadilishe ili "tuitumie fursa kutangaza vivutio" kwanza huyo mama hata wilaya hapati anawakilisha nini sasa.
 
Halafu naona pia kama kuna promotion ya meno ya tembo! Kwa nini wasingeweka tembo mzima!!

Nami sioni tatizo la hizo nguo. Kwa mwanaume huo ni mgolole. Mimi tatizo langu tangu zamaani nikiwa mdogo nilikuwa nashangaa hayo meno ya tembo kuwekwa kwenye nembo yaondolewe kwa kweli. Tena ile zamani uharamu wa meno ya tembo ulikuwa zaidi nadhani kuliko hata sasa. Nilikuwa tu najiwazia sina pa kusemea. nembo naipenda sana hasa katika kudisplay message ya usawa wa wanawake na wanaume. Lakini Meno ya tembo yatolewe kabisa.
 
Acheni kuanza kutindua historia ninyi. Ulizeni kwanza wazee wa Tanganyika, siyo mnakurupuka tu na hisia zenu za kukosa mada minaanza kuleta uharibifu hapa.
Tabby wasichojua ni kuwa nembo hiyo ilishabadilishwa tokae 2013 kivitendo baada ya Chama kongwe kumpata huyo Katibu mkuu waliyenaye.
ImageUploadedByJamiiForums1426570871.549765.jpg
 
Last edited by a moderator:
Kwa nini karafuu na sio korosho,
Kwa nini karafuu na sio pamba,
Kwa nini karafuu na sio alizeti,

Naunga mkono hoja, tuibadilishe ili "tuitumie fursa kutangaza vivutio" kwanza huyo mama hata wilaya hapati anawakilisha nini sasa.

Pamba huioni mkuu. Km ujuavyo hii ni nembo ya Tanzania si Tanganyika hivyo karafuu muhimu!
 
waje wanahistoria watueleze maana na kusudi ya kuwepo kila kitu kilichoko kwenye nembo hii ndipo tuone umuhimu wa kubadirisha au kuiacha iliyopo iendelee
 
Back
Top Bottom