Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,010
- 9,875
NEC YAKABIDHI NAKALA YA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KWA VYAMA VYA SIASA
Tume ya Taifa ya uchaguzi leo imevikabidhi vyama vya siasa nakala tepe ya daftari la kudumu la wapiga kura pamoja na orodha ya vituo vya kupigia kura.
Pia wamekabidhi Karatasi ya mfano ya kupigia kura yenye orodha ya wagombea nafasi ya urais na makamu wa rais
Kanuni ya 37 ya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura mwaka 2018 inaelekeza Tume inaweza kuvipatia vyama nakala ya Daftari hilo kwa ajili ya utambuzi wa wapigakura wanaoingia Kituoni.
Masharti ya kanuni ya 50 (1) ya uchaguzi wa Rais na wabunge ya mwaka 2020, wasimamizi wa uchaguzi watavipatia vyama vya siasa orodha ya vituo vya kupigia kura ili vyama vipange mawakala.