NEC, hili ni bao la mkono?

NEC, hili ni bao la mkono?

Dangire

JF-Expert Member
Joined
Oct 5, 2011
Posts
221
Reaction score
68
Katika magazeti ya leo Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) amenukuliwa akisema kuwa:
1. jumla ya vituo vya kupigia kura ni 64,736
2. Kila kituo kitakuwa na wapigakura 450.
3. jumla ya wapiga kura waliothibitishwa ni 23,254,485 (22,751,292 (Bara), 503,193 (Zanzibar)

Ukokotoaji:
1. jumla ya wapiga kura (23,254,485) ugawe kwa idadi ya wapiga kura kila kituo (450) = 51,677
Hii ina maana kwamba, vituo vilivyohitajika kupigia kura ni 51,677 tu na sio 64,736. hii ina maana kuna nyongeza ya vituo 13,059. HIVI NI VITUO 'HEWA'? vya nini na kwa faida ya nani?

2. Ikiwa kila kituo ni watu 450 na vituo hewa ni 13,059, hii ina maana kuwa jumla ya wapiga kura katika 'hewa' (Maruhani) ni 450x13,059 = 5,876,555. Maruhani karibu milioni 6 watapiga kura! wanatoka wapi? nani atawaleta? kwa faida ya nai? je tume inawahitaji hawa?

3. Kwa idadi ya vituo 64,736 na wapiga kura 23,254,485, maana yake ni kuwa kila kituo kinapaswa kuwa na watu 360 tu, na sio 450 kama tume inavyotueleza.(chukua idadi ya wapiga kura ugawe kwa idadi ya vituo vya kupigia kura vya NEC - 450). hII INA MAANA KUWA kwa kila kituo kutakuwa na nyongeza ya watu (Maruhani) 90 (450-360). tunajiuliza, hawa wameongezwa kwa faida ya nani?

4. Ikiwa idadi ya vituo ni 64,736 na kila kituo wapiga kura 450, hii ni sawa sawa na idadi ya wapiga kura 29,131,200 (64,736x450). maana yake ni kuwa wapiga kura waliozidi (kutoka 23,254,485) ni 5,876,715.

NB: Tume itoe maelezo ya kina na watuambie wametumia 'calculation' za mtaala wa hesabu wa nchi gani ambao ni tofauti kabisa na huu wa kwetu?

Mwl. D. Kitwana
TUDARCo.
 
hapa ni vita kali kila moja anawaza mbinu ya kushinda iwe halali au isiwe halali
 
Ufafanuzi wa kuaminika unahitajika katika hili. Lubuva waondoe watu na shaka ya bao la mkono. Tunaomba uwazi katika hili. La sivyo yatakugeukia wewe mwisho wa siku. ICC iko mlangoni kusikilizia bao la mkono.
 
Siku alipohojiwa na Tido Mhando azam tv, jaji Lubuva alisema tutakuwa na vituo 72000/= leo naona wamepunguza tena.

Mimi niwakumbushe tume, kama wanataka kujua neno la Peoples power lililoimbwa na Chadema kwa Miaka 10 basi wafanye Makosa ya kijinga kama Haya, yataigharimu Nchi hii. Kwasasa watu uvumilivu wao upo kwenye Ncha.

Mungu epushia mbali.
 
Mi binafsi sina wasiwasi na uchakachuaji kwa njia ya vituo hewa vya kupigia kura. Hiyo idadi ya wapiga kura 450 kwa kila kituo ni maximum number ya wapiga kura kwa kila kituo lakini kuna vituo vingine vitakuwa na watu wachache kuliko hiyo idadi. Hata wakati wa uandikishwaji ktk daftari la wapiga kura baadhi ya vituo vilikuwa na watu wengi na vingine watu wachahe.

Suala la kuwa na vituo hewa linadhibitika kiurahisi sana kuliko inavyodhaniwa. Kila chama kiandae mawakala kulingana na idadi ya vituo. Na kwa vile list ya vituo (majina ya vituo) yanajulikana basi kama kituo hicho hakitakuwepo kwenye list automatically kitakuwa feki. Au kama kituo kipo kwenye list lakini haiko mahali popote then mawakala waripoti kwenye vyama vyao ili hatua zichukuliwe mapema.
 
Duuuu jamani tuwe makini hasa vijana walio omba uwakala kusimamimia kura wananchi wanahasira sana
 
Na matokeo ya udanganyifu huu sheria ianzuia kupingwa mahakamani.
Hapa ujanja ni kulinda kura na kama viongozi wa UKAWA mko serious vya kutosha jaribuni kwenda mahakamani ili kupata ufafanuzi wa mambo yanayoonekana madogo kwa sasa lakini ndio yatatuletea majonzi!
 
Siku alipohojiwa na Tido Mhando azam tv, jaji Lubuva alisema tutakuwa na vituo 72000/= leo naona wamepunguza tena.

Mimi niwakumbushe tume, kama wanataka kujua neno la Peoples power lililoimbwa na Chadema kwa Miaka 10 basi wafanye Makosa ya kijinga kama Haya, yataigharimu Nchi hii. Kwasasa watu uvumilivu wao upo kwenye Ncha.

Mungu epushia mbali.
mkuu ulicho kiongea ni ukweli 100% wakileta ujinga nina uhakika watu hawatakubali na siku hali ya hewa ikichafuka TANZANIA UTULIFU HAUTA PATIKANA TENA DAWA YA HII NGUVU UMMA NI NDOGO NI KUIPA KITU INACHO TAKA VINGINEVYO POLISI WALA WANAJESHI HAWATAWEZA KUTULIZA MATHARA YA HII NGUVU !!
 
lubuva inabidi aweke wazi orodha na idadi ya wale wafu waliotolewa ktk daftari la kudumu la wapiga kura...
 
Wapo jumla ya wapiga kura 22,751,292 nchini katika daftari la kudumu la wapiga kura walioandikishwa na NEC na 503,525 walioandikishwa na ZEC.

Kwa idadi hiyo ya wapiga kura walioandikishwa na NEC na ZEC, Magufuli anashinda kwa asilimia 69 ya kura zote.

Yangu macho na masikio, ila watanzania tutambue amani yetu ni tunda lililotukuka Afrika na duniani kote, tuitunze, tuidumishe na tuepuke mihemuko ya kisiasa. Tuwe tayari kumpokea Kiongozi huyo wa Awamu ya Tano.
 
Sijui mimi nilisikia vibaya ila alisema ni 450-500 kwa kituo,atleast ingekuwa kati ya 350-400 ili ilete wastani wa 375 kwa kila kituo ukikokotoa ije 375X64736=24,276,000
 
hatuna aman tuna utulivu tuu, mada yko umeileta kishabiki huna jipya kikubwa umekurupuka
 
Siku alipohojiwa na Tido Mhando azam tv, jaji Lubuva alisema tutakuwa na vituo 72000/= leo naona wamepunguza tena.

Mimi niwakumbushe tume, kama wanataka kujua neno la Peoples power lililoimbwa na Chadema kwa Miaka 10 basi wafanye Makosa ya kijinga kama Haya, yataigharimu Nchi hii. Kwasasa watu uvumilivu wao upo kwenye Ncha.

Mungu epushia mbali.

ila hilo jina lako halitamkiki...
 
Wapo jumla ya wapiga kura 22,751,292 nchini katika daftari la kudumu la wapiga kura walioandikishwa na NEC na 503,525 walioandikishwa na ZEC.

Kwa idadi hiyo ya wapiga kura walioandikishwa na NEC na ZEC, Magufuli anashinda kwa asilimia 69 ya kura zote.

Yangu macho na masikio, ila watanzania tutambue amani yetu ni tunda lililotukuka Afrika na duniani kote, tuitunze, tuidumishe na tuepuke mihemuko ya kisiasa. Tuwe tayari kumpokea Kiongozi huyo wa Awamu ya Tano.

Wewe kwa akili zako mbaya ndio unataka kuleta uvunjifu wa amani kwa kumtaja mgombea wako kushinda kabla ya kupiga kura!
 
Bukama Batoko kwan ww ulikua unaelezea idadi ya wapiga kura au ushindi wa magufuli??? n waz kwamba elimu yko haijakukomboa kama ulitaka kuelezea ushindi wa magifili ungeeleza kwa data hzo asilimia 69 zinatoka wp kingine narudia tena n ushabik na mkumbo kwa sababu kuelezea idadi ya wapigakura na ushindi wa magufuli ni dhair umekosea mambo hayaendi ivo
 
Last edited by a moderator:
Na matokeo ya udanganyifu huu sheria ianzuia kupingwa mahakamani.
Hapa ujanja ni kulinda kura na kama viongozi wa UKAWA mko serious vya kutosha jaribuni kwenda mahakamani ili kupata ufafanuzi wa mambo yanayoonekana madogo kwa sasa lakini ndio yatatuletea majonzi!

Baada ya kupiga kura tu mimi na familia yangu natafuta mahali pa kwenda kujificha mbali kabisa na mji maana haya mnayoendelea na kuyaamasisha humu ndani wengine yatatuletea shida kubwa sana na hasa ukizingatia tunawatoto wadogo wengine ni wachanga bado wananyonya. Ee MUNGU eeeeeeee....rehemu Tanzania na watoto wangu!!!
 
Back
Top Bottom