Ndugu yangu kaoa kahaba? Tumshauri basi

Ndugu yangu kaoa kahaba? Tumshauri basi

Nimejitahidi nimeisoma yote ila kwa shida sana mkuu..

Dah!!..huyo mdada kapitia magumu sana na amekuwa na wanaume wengi kwenye uhusiano wa kimapenzi ila hakuwahi kupata mimba/ujauzito.

POLE SANA KWA JAMAA YAKO
Nimeruka ruka kuokoa muda ametoa mimba nyingi sana kupima kwake ilikuwa kama kunywa Maji, hivi Jana Nilikuwa Kinyerezi kuongea na Shemeji yangu kwani jamaa bado anaishi kwangu
 
Ni hadithi tu hii, maana kwenye uhalisia haiwezekani mwanamke amwelezee mume wake matukio yote haya tena kwa mtiririko na mpaka wanaotaka kumla soon, huyo mwanamme si atazimia.
Mzee ningeshare screenshorts nawe kuamini ni kuchagua tuu
 
BABU KIDUDE
Jamii forum ilikuwa zamani ila kwa sasa ni kazi bure. Hii forum kipindi cha nyuma ilikuwa ina watu waelewa na wenye kujitambua japokuwa wapo ila kwasasa ni wachache sana. Kama una masuala yako yanayohitaji ushauri bora ukayamaliza nje ya jamii forum kuliko humu maana watu badala ya kujadili mada yako wanaanza kujadili uandishi wako japokuwa umewaomba radhi kwa uandishi. Hii forum ishavamiwa na watoto na siyo salama tena kwa masuala nyeti kama ya kwako.
Huyo mwanamke bado anampenda jamaa ila shida bado anatabia ya huruma na jinsi mlolongo wa wanaume wanaomfuatilia lazima wamtafune kama ataendelea na kazi. Kama ikiwezekana jamaa amtafutie kazi ya kujiajiri tofauti na hapo hao jamaa lazima wamtafune tu na wala haiepukiki kuliwa.
Kabisa mkuu now days watoto fb wamejaa huku
 
Nimejitahidi sana Kuficha vitu Vingi, nimepitia comments nyingi wenye Ushahuri ni wachache sana wengi wamekosoa na kama kawaida waswahili wengine wamejikita kweye udhaifu wangu uandishi pamoja na kuomba Radhi, wengine wamehusisha hii story na mimi yote ndo Jamiiforum hiyooo uhuru wa kutoa maoni.

Jana baada ya kutoka kazini nilipita Kinyerezi kwa shemeji yangu huyo kituo kinaitwa Saloon, Tuliongelea swala hili shemeji yangu alibaki analia tuu haku akinipa simu yake kuonyesha hayo na yeye yupo tayali kwa adhabu yoyote na kwa kiasi kikubwa anajuta kuzaliwa na anaomba hata afe azaliwe upya hili afanyie marekebisho makosa yake. Muda Mwingi alikuwa anamuulizia mume wake anaendeleaje kama anakula...
 
Nimejitahidi sana Kuficha vitu Vingi, nimepitia comments nyingi wenye Ushahuri ni wachache sana wengi wamekosoa na kama kawaida waswahili wengine wamejikita kweye udhaifu wangu uandishi pamoja na kuomba Radhi, wengine wamehusisha hii story na mimi yote ndo Jamiiforum hiyooo uhuru wa kutoa maoni.

Jana baada ya kutoka kazini nilipita Kinyerezi kwa shemeji yangu huyo kituo kinaitwa Saloon, Tuliongelea swala hili shemeji yangu alibaki analia tuu haku akinipa simu yake kuonyesha hayo na yeye yupo tayali kwa adhabu yoyote na kwa kiasi kikubwa anajuta kuzaliwa na anaomba hata afe azaliwe upya hili afanyie marekebisho makosa yake. Muda Mwingi alikuwa anamuulizia mume wake anaendeleaje kama anakula...
kweli mkuu ni ngumu sana na hata jamaa yako inabidi afanye maamuzi magumu sana:
1. Tayari wana mtoto na ndoa wameshafunga hivyo yeye ni mke halali wa jamaa
2. mwanamke ajijue yeye ni mke wa mtu na mambo ya kugawa namba yake aache kabisa
3. mawasiliano na ma ex zake yafe kabisa yaani mimi nikiachana na mtu sinaga muda wa kumtafuta bora kuwablock tu
4. yaliyopita yamepita akubali kuanza upya tu na atubu kabisa maana historia yake amepitia magumu sana
5. Mleta uzi kama shemeji unaweza mtafuta mwanasaikolojia akaongea naye maana kuna hali bado binti anaipitia
 
Fupisha weka main points tu. Tutaweza to a mawazo
 
Sipendi mtu aandike MBAKA aseee!!imagine anayeandika ni mwingine lakini ninayeteseka ni mie

Ukifika mwisho wa stori yako nitasoma
Halafu unafuatilia story kwa umakini....ndefu huku ukidhani anafinalize lakini wapi.... sasa ndo unakutana na hizo MBAKA kibao. Though in most cases huwa tunaandika tukiwa occupied sana.
 
Huyo ndiye mke sasa na mpaka ameeleza yote ujue hapo kwa jamaa amefika. Kwa tuliosomea saikolojia tunajua kuwa hiyo ni step ya kwanza ya healing (kupona). Inauma lakini jamaa asijidanganye kumuacha eti atapata nafuu. Wadada wengi hawasemi ya moyoni na wanaonekana wake bora kama jamaa alivyokuwa anamuona wa kwake. Wangeamua kusema dunia ingekuwa inawaka moto kama ule wa California ama Amazon.

Kwa jinsi ulivyoielezea hii story kwa ufasaha naamini wewe ndiye mhusika ila hilo si la muhimu la muhimu zaidi ni endelea na mkeo wewe ndiye mwanaume wake utakayemtibu kumbuka hilo si tatizo tu ni TATIZO LA KISAIKOLOJIA tokea Sekondari. Ukimuamini tena na kumjali utaokoa maisha yako na ya mwanao. Siku hizi kuna tiba ya kisaikolojia kwa hili tatizo. Ukipenda nitasaidia. NISAMEHE kama nimekudhania vibaya ila kama si wewe pitisha huu ujumbe kwa mhusika.

NB: Kila binadamu ana historia na wengi wetu tupo kama shuka lenye lilotobolewa mno nikimaanisha tuna majeraha mengi sana tuliyokumbana nayo kwenye maisha na yametuachia alama nyingi. All in all yanatibika tukiamua kuyachukulia maamuzi.
 
Hakuna aliyelazimishwa kusoma kama ni story ndefu kila mmoja ale kona kivyake. Kwa wenye kupenda zile fupi ingieni fb mtazikuta.
 
Back
Top Bottom