nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
na Mwandishi wetu
MFANYABIASHARA anayedaiwa kuwa ni kinara wa biashara ya dawa za kulevya nchini, amenaswa na shehena ya dawa za kulevya aina ya Heroine na Cocaine.
Mfanyabiashara huyo, ametajwa kwa jina moja la Asad na anadaiwa kuwa na uhusiano wa kindugu na mmoja kati wabunge maarufu nchini, mwenye asili ya Kiasia.
Habari ambazo Tanzania Daima Jumatano imezipata, zilisema kuwa mfanyabiashara huyo alinaswa na dawa hizo za kulevya nyumbani kwake, Mikocheni na kiasi kingine kilinaswa Kabuku, mkoani Tanga.
Mmoja wa maafisa wa polisi wanaohusika na kitengo cha kupambana na dawa za kulevya, aliliambia gazeti hili kuwa mfanyabiashara huyo alinaswa mkoani Arusha, akijaribu kuwatoroka polisi waliokuwa wakimsaka kwa muda mrefu.
Kwa mujibu wa habari hizo, mfanyabiashara huyo ambaye ni mmoja wa vigogo wa biashara hiyo amekuwa akisakwa na polisi kwa muda mrefu na kuwatoroka mara kwa mara.
Amekamatwa na kiasi kikubwa cha Heroin Kabuku Tanga, alikamatwa pia na shehena nyingine ya dawa za kulevya aina ya Cocaine nyumbani kwake Mikocheni na mwenyewe amekutwa mjini Arusha akiwa kwenye harakati za kuwatoroka polisi, kilisema chanzo chetu cha habari.
Akithibitisha kukamatwa kwa mihadarati hiyo, Kamanda wa Kikosi cha kupambana na dawa za kulevya, Godfrey Nzowa, alikiri kukamatwa kwa kigogo huyo.
Alisema mfanyabiashara huyo anatarajiwa kufikishwa mahakamani kesho mjini Tanga kujibu tuhuma hizo.
Hata hivyo hakuwa tayari kueleza mahusiano ya kigogo huyo na mbunge mmoja maarufu nchini kwa madai kuwa taarifa zote zitapatikana mahakamani hapo. Kweli tumemkamata na kiasi kikubwa cha mihadarati na kesho (leo) atafikishwa mahakamani mkoani Tanga. Taarifa zingine zote za uhusiano wake na mbunge uliyemtaja, mtazipata mahakamani hapo kesho, alisema Kamanda Nzowa.
MFANYABIASHARA anayedaiwa kuwa ni kinara wa biashara ya dawa za kulevya nchini, amenaswa na shehena ya dawa za kulevya aina ya Heroine na Cocaine.
Mfanyabiashara huyo, ametajwa kwa jina moja la Asad na anadaiwa kuwa na uhusiano wa kindugu na mmoja kati wabunge maarufu nchini, mwenye asili ya Kiasia.
Habari ambazo Tanzania Daima Jumatano imezipata, zilisema kuwa mfanyabiashara huyo alinaswa na dawa hizo za kulevya nyumbani kwake, Mikocheni na kiasi kingine kilinaswa Kabuku, mkoani Tanga.
Mmoja wa maafisa wa polisi wanaohusika na kitengo cha kupambana na dawa za kulevya, aliliambia gazeti hili kuwa mfanyabiashara huyo alinaswa mkoani Arusha, akijaribu kuwatoroka polisi waliokuwa wakimsaka kwa muda mrefu.
Kwa mujibu wa habari hizo, mfanyabiashara huyo ambaye ni mmoja wa vigogo wa biashara hiyo amekuwa akisakwa na polisi kwa muda mrefu na kuwatoroka mara kwa mara.
Amekamatwa na kiasi kikubwa cha Heroin Kabuku Tanga, alikamatwa pia na shehena nyingine ya dawa za kulevya aina ya Cocaine nyumbani kwake Mikocheni na mwenyewe amekutwa mjini Arusha akiwa kwenye harakati za kuwatoroka polisi, kilisema chanzo chetu cha habari.
Akithibitisha kukamatwa kwa mihadarati hiyo, Kamanda wa Kikosi cha kupambana na dawa za kulevya, Godfrey Nzowa, alikiri kukamatwa kwa kigogo huyo.
Alisema mfanyabiashara huyo anatarajiwa kufikishwa mahakamani kesho mjini Tanga kujibu tuhuma hizo.
Hata hivyo hakuwa tayari kueleza mahusiano ya kigogo huyo na mbunge mmoja maarufu nchini kwa madai kuwa taarifa zote zitapatikana mahakamani hapo. Kweli tumemkamata na kiasi kikubwa cha mihadarati na kesho (leo) atafikishwa mahakamani mkoani Tanga. Taarifa zingine zote za uhusiano wake na mbunge uliyemtaja, mtazipata mahakamani hapo kesho, alisema Kamanda Nzowa.