GUSSIE
JF-Expert Member
- Dec 2, 2014
- 3,866
- 11,100
Picha ni edited
Mkuu mbona unaleta photoshop hapa Jf
Unatengeneza picha yako na kuedit
Shameless, Jipange upya umechemka
Mwambie aliyekutuma ashindwe
Mkuu mbona unaleta photoshop hapa Jf
Unatengeneza picha yako na kuedit
Shameless, Jipange upya umechemka
Mwambie aliyekutuma ashindwe
Nimeamua kuweka picha hii baada ya kumwona Makamu mwenyekiti wa Chadema Kanda Ya Kaskazini Kaka yangu Joseph Selasini Mbunge wa Rombo akihusishanisha tukio iliyofanyika Mbeya ya wanachama wa Chama Cha Mapinduzi wakifanya Igizo la kubeba jeneza yenye bendera ya chadema ikiwa na msalaba.
Jambo lililomfanya Kaka Joseph Selasini kuhusisha tukio ilo la Mbeya na kudhalilisha Ukristo kwakuwa ilihudhuria na Naibu Spika Dr Tulia Akson.
Ndugu yangu Selasini katika andiko lake iliyobandikwa kwenye kurasa la social media ya Chadema kanda ya Kaskazini amelaumu sana Naibu Spika kushiriki kudhalilisha Ukristo kutokana na tukio Ilo.
Nikiri kuwa kaka yangu Joseph Selasini nimefahamiana naye muda mrefu wakati huo akiwa Katibu wa Vijana Taifa wa NccrMageuzi mwenyekiti wake akiwa Msafiri Mtemelwa ambaye kwa sasa ni Naibu Katibu mkuu wa Act Wazalendo.
Miye nikiwa ccm mwaka 1994 yeye na wenzanke akina Mosena Nyambabe, james Mbatia, Hemed Sabula, Evod Mmanda, akina Chitanda wakiwa NccrMageuzi sisi tulikuwa wadogo zao ktk siasa akina mbatia wakiwa Udsm sisi Ndiyo tunamaliza sekondari ukweli Selasini ni mwanasiasa mwenye Jaziba asiyetumia akili hata kidogo.
Nirudi kwenye picha hii hapa chini
Ili tukio iliyotokea katika kata ya Iyela mkoani Mbeya kwenye maandamano mwaka 2013/2014 na kupokelewa na aliyekuwa katibu mkuu wa Chadema DR Wilbroad Peter Silaa na aliyekuwa mwenyekiti wa Bavicha Taifa Tanzania Mh John Heche katika Ile vuguvugu ya akina Samson Mwigamba na Zitto Kabwe.
Kipindi icho kaka Joseph Selasini alikuwa Mbunge chadema lakini hakuona kama ni Udhalilishaji wa Ukiristo Leo kwakuwa imefanywa na mtu wasiyempenda anataka kuchonganisha Imani ya Ukristo na siasa zetu.
Ni vyema sisi wafuatiliaji wa mambo ya siasa kukemea tabia hii ya viongozi wa chadema kutaka kuonyesha Umma kuwa wanaonewa hata kama hayo mambo wameanzisha wenyewe.View attachment 1213819