SubiriJibu
JF-Expert Member
- Jun 26, 2009
- 1,803
- 1,863
Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai, amesema anakerwa na tabia ya vyombo vya habari nchini kuwakosoa viongozi wa CCM na Serikali tu na kuwabeba wa vyama vya upinzani hata wanapokosea.
Amesema, viongozi wapinzani ni viongozi wa serikali watarajiwa, hivyo vyombo vya habari vina wajibu wa kuwakosoa kama ilivyo kwa viongozi wa serikali na chama tawala badala ya kuwabeba hata katika mamo ya wazi.
Aliyasema hayo katoka maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya habari Duniani jana jijini Dar.
Alisema umekuwa ni utamaduni wa waandishi wa habari kuwabeba wapinzani huku viongozi wa CCM na serikali wakikosolewa kutokana na utendaji wao.
"Hakuna jambo lisilokuwa na mwisho :clap2: na leo tukiwabana hawa na kuwaacha wanaotarajiwa kuwa viongozi, sio haki, lazima vyombo vya habari viangalie pande zote na kukosoa", alisema.
Alivitaka vyombo vya habari kubadilika na kuwa na mapenzi na nchi yao badala ya kushabikia wanasiasa na vyama vyao, kwani wanahabari wana nafasi kubwa ya kujenga jamii ama kuibomoa kama watakubali kutumika vibaya.
Kuhusu mahusiano kati ya BUnge na vyombo vya habari, Ndugai alisema, kwa muda mrefu yameendelea kuwa mazuri na kuahidi kuyadumisha.
SOURCE: NIPASHE (pg. 08)
DATE: MAY 04, 2012
Amesema, viongozi wapinzani ni viongozi wa serikali watarajiwa, hivyo vyombo vya habari vina wajibu wa kuwakosoa kama ilivyo kwa viongozi wa serikali na chama tawala badala ya kuwabeba hata katika mamo ya wazi.
Aliyasema hayo katoka maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya habari Duniani jana jijini Dar.
Alisema umekuwa ni utamaduni wa waandishi wa habari kuwabeba wapinzani huku viongozi wa CCM na serikali wakikosolewa kutokana na utendaji wao.
"Hakuna jambo lisilokuwa na mwisho :clap2: na leo tukiwabana hawa na kuwaacha wanaotarajiwa kuwa viongozi, sio haki, lazima vyombo vya habari viangalie pande zote na kukosoa", alisema.
Alivitaka vyombo vya habari kubadilika na kuwa na mapenzi na nchi yao badala ya kushabikia wanasiasa na vyama vyao, kwani wanahabari wana nafasi kubwa ya kujenga jamii ama kuibomoa kama watakubali kutumika vibaya.
Kuhusu mahusiano kati ya BUnge na vyombo vya habari, Ndugai alisema, kwa muda mrefu yameendelea kuwa mazuri na kuahidi kuyadumisha.
SOURCE: NIPASHE (pg. 08)
DATE: MAY 04, 2012