Ndugai: Vyombo vya habari vinawabeba wapinzani

Sasa wawabane wapinzania kwalipi? Kwahiyo anakiri kuwa CDM ndiyo mshika Dola mtarajiwa?Gud

Mytake: I don't know what the key to success is, but the key to failure is trying to please everyone.
 
Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai, amesema anakerwa na tabia ya vyombo vya habari nchini kuwakosoa viongozi wa CCM na Serikali tu na kuwabeba wa vyama vya upinzani hata wanapokosea.

Amesema,
viongozi wapinzani ni viongozi wa serikali watarajiwa, hivyo vyombo vya habari vina wajibu wa kuwakosoa kama ilivyo kwa viongozi wa serikali na chama tawala badala ya kuwabeba hata katika mamo ya wazi.

Aliyasema hayo katoka maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya habari Duniani jana jijini Dar.

Alisema umekuwa ni utamaduni wa waandishi wa habari
kuwabeba wapinzani huku viongozi wa CCM na serikali wakikosolewa kutokana na utendaji wao.

"Hakuna jambo lisilokuwa na mwisho :clap2: na leo tukiwabana hawa na kuwaacha wanaotarajiwa kuwa viongozi, sio haki, lazima vyombo vya habari viangalie pande zote na kukosoa", alisema.

Alivitaka vyombo vya habari kubadilika na kuwa na mapenzi na nchi yao badala ya kushabikia wanasiasa na vyama vyao, kwani wanahabari wana nafasi kubwa ya kujenga jamii ama kuibomoa kama watakubali kutumika vibaya.

Kuhusu mahusiano kati ya BUnge na vyombo vya habari, Ndugai alisema, kwa muda mrefu yameendelea kuwa mazuri na kuahidi kuyadumisha.

SOURCE: NIPASHE (pg. 08)
DATE: MAY 04, 2012


Amenikumbusha wakati fulani, nafikiri ilikuwa 2010, kulikuwa na workshop ya waandishi wa habari za bunge. Ndugai alilalamika kuwa inakuwaje katikla vipindi vya televisheni wanaalikwa watu wanaoonekana kuwa ni wa upande mmoja (kuikosoa serikali na chama tawala). Kwa maoni yake alisema wazungumzaji wengi wanaoalikwa huwa ni watu wa upinzani, hata kama hawana direct party affiliation.

Alilalama sana kuhusu wasomi/wanazuoni kuwa wakosoaji sana kwa mihimili ya serikali. Ilikuwa ni baada ya Mwalimu Bashiru Ally kuwasilisha paper yake, ambapo kama kawa alipiga nondo, Ndugai uvumilivu ukamshinda. Akalalama.
 
Kama huyu kilaza naibu spika anamaanisha vyombo vya habari pamoja na Uhuru na Mzalendo, Radio Uhuru, Habari leo nadhani akaanze upya kujenga hoja.

Hivyo nilivyovitaja natumaini ndugai anajua VINAWABEZA WAPINZANI.

Inakuwa vigumu sana kupata ujumbe aliokusudiwa kwenye hoja yake kwa sababu ya utata wa habari za magazeti ya chama cha magamba. Labda hii ni kuthibitisha nyani haoni kundule na mkuki kwa nguruwe.

Nawashauri wanajamvi tuvipe moyo vyombo vya habari pamoja na JF viongeze makali ya kukosoa hawa watawala na chama tawala wachumia tumboni
 
Huyu naye hana jipya, tumemuona akiongoza bunge anavyokuwa, yuko bias sana kwake yeye chama mbele. wapinzani hata wakitoa hoja nzuri zenye mpango wa kujenga taifa yeye anaziweka kapuni, sijui anaogopa yaliyomkuta Sitta!! Ni mchumia tumbo tu huyu na siasa zake uchwara, watu kama hawa hafahi kuongoza bunge.
 
Huyu Jamaa nafikiri anaongea bila kufikiria,

Kwanza yeye mwenyewe kwa asilimia kubwa hatendi haki bungeni sasa anategemea aandikwe vipi?
pili hawa anaowaita wapinzani tayari ni viongozi kwa taifa hili wanaongoza watu wengi sana hivyo sio kwamba wanaotarajiwa kuwa viongozi, hawa ni viongozi tayari, chukulia mtu kama Dr Slaa, Mbowe, Lipumba wewe unataka wawe viongozi mara ngapi?, Dr Slaa ni kiongozi wa watu wengi sana jamani!! tutazame uongozi kwa upana zaidi asifikiri kiongozi ni kuwa naibu spika tu.Narudia tena Dr Slaa ni kiongozi wetu akipotoka vyombo vya habari vitamwambia lakini haviwezi kumsingizia ikiwa bado hajapotoka.

Pia anatakiwa kukemea na vyombo vingine sio vya habari tu akemee Police, Mahakama, Usalama wa taifa na wengine wengi watende haki na sio kuegemea upande wa serikali tu.

Umenena mkuu.
 
Ndugai ameongea kana kwamba ni mpinzani. Kitu ambacho ameshindwa kukielewa ni kuwa:
Wapinzani hawana serikali hivyo matendo yao hayawezi kuathiri hali za maisha ya kila siku kwa watanzania kwani hawawezi ku-implement sera zao ili waandishi waanze kuzichambua na kuwakosoa. Maana yake ni kwamba Ndugai anataka vyombo vya habari viandika matendo binafsi ya wapinzani kama vile ulevi, ufuska kama upo etc.


  • CCM ni lazima iandikwe kwa sababu ndio wanaoshikilia dola na ndiyo wanaoweza kutoa amri kwa vyombo vya dola kuhusu hatua za kuwachukulia wavunja sheria. Kama mafisadi etc, wapinzania hawana uwezo huo na hawana dola. Hivyo ni fair kwa vyombo vya habari kuandika habari za yule mwenye rungu huku akiacha nguruwe anashambulia mihogo shambani

  • Ndugai anataka wanahabari waamini kuwa failure ya governance inakuwa shared na vyama vyote vya siasa, bila hata kuona aibu. Urais mnao CCM, Umakamu CCM, Uwaziri mkuu CCM, Uspika CCM, Unaibu spika CCM, Majority ya wabunge CCM, Mawaziri CCM, Manaibu waziri CCM, Mahakama CCM, Polisi CCM, TAKUKURU CCM, kila kitu ni CCM. Sasa upinzani unapata lawama kutoka wapi?. Kitu chochote kibaya kuhusu serikali ni lazima kielekezwe kwa anayehusika.

  • Ndugai pia alitakiwa kueleza ni kwa jinsi gani vyombo vya habari vya serikali vimekuwa vikifanya coverage ya wapinzani japo vinalipiwa kwa kodi ya wananchi bila kujali itikado zao?. TBC1 etc.

  • Ndugai anataka serikali isifiwe na vyombo vya habari wakati maisha yakiwa magumu, mfumuko wa bei ukipaa, hospitalini hakuna madawa, usalama wa raia si priority tena kwa polisi etc. Kama vyombo hivi vinategemea wananchi kununua habari zao ili vi-survive basi kuandika kinyume na hapo ni kuwafanya wananchi wavidharau na kuviona unreliable, je Ndugai na serikali ya CCM itatoa ruzuku ya mapato yatakayopotea kwa kuwadanganya wananchi ili hali halisi wanaijua?

  • Ndugai anatakiwa kujua kuwa 'Saying so does not make it so' Hata kama wapinzani wakiandikwa vibaya na vyombo vya habari bado ukweli utabakia palepale kuwa wao hawahusiki na sera zinazoendesha nchi kwa sasa, hivyo basi kusema hali ngumu ya maisha inasababishwa na wapinzani haitaifanya CCM kuweza kuonekana inafanya kazi. Njia pekee ya CCM kuandikwa vizuri si kutaka upinzani nao uandikwe vibaya bali ni kusimamia sera zake na kutekeleza yale waliyoyaahidi kwa wananchi wakati wa kampeni. Mambo yakiwa mazuri, basi hawataandikwa tena kwa mambo mabaya.

Wapinzani kuwa 'Govt inwaiting' hakuwafanyi kuanza kumulikwa kwa ajili ya failures za 'Govt in power'. Ningekubaliana na Ndugai kama bunge lingekuwa na majority ya wapinzani. Hapo ningesema we have a divided Govt and the failure blame should be shared!.
 
Je anakerwa pia na Uhuru, Mzalendo, Daily News na TBC kuwabeba viongozi wa serikali wanaotarajia kupumzishwa?
 
Magamba Wabadilike, wawe na matendo masafi halafu waone vyombo vya habari vitakuwa upande gani. Ukweli ni kwamba jambo lolote geni (liwe zuri au baya) hiyo ni habari. Matendo mabaya yanayofanywa na baadhi ya viongozi wetu ndio yamewafikisha hapo hao waliopo madarakani. Naibu spika nendeni mkajipange.

na hata magwanda wabadilike wakubali kukosolewa na wapanue demokrasia,kwa kuwa wao ni serikali mbadala.
 
anaweweseka huyu nae ni gamba lakini cha msingi

ametambua kuwa CDM tuko mbioni kuchukua nchi
 
Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai, amesema anakerwa na tabia ya vyombo vya habari nchini kuwakosoa viongozi wa CCM na Serikali tu na kuwabeba wa vyama vya upinzani hata wanapokosea.

Amesema, viongozi wapinzani ni viongozi wa serikali watarajiwa, hivyo vyombo vya habari vina wajibu wa kuwakosoa kama ilivyo kwa viongozi wa serikali na chama tawala badala ya kuwabeba hata katika mamo ya wazi.

Aliyasema hayo katoka maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya habari Duniani jana jijini Dar.

Alisema umekuwa ni utamaduni wa waandishi wa habari kuwabeba wapinzani huku viongozi wa CCM na serikali wakikosolewa kutokana na utendaji wao.

"Hakuna jambo lisilokuwa na mwisho :clap2: na leo tukiwabana hawa na kuwaacha wanaotarajiwa kuwa viongozi, sio haki, lazima vyombo vya habari viangalie pande zote na kukosoa", alisema.

Alivitaka vyombo vya habari kubadilika na kuwa na mapenzi na nchi yao badala ya kushabikia wanasiasa na vyama vyao, kwani wanahabari wana nafasi kubwa ya kujenga jamii ama kuibomoa kama watakubali kutumika vibaya.

Kuhusu mahusiano kati ya BUnge na vyombo vya habari, Ndugai alisema, kwa muda mrefu yameendelea kuwa mazuri na kuahidi kuyadumisha.

SOURCE: NIPASHE (pg. 08)
DATE: MAY 04, 2012

Kiongozi asiyependa kukosolewa huyo hafai kuwa kiongozi, na imani 100% mnakosolewa pale mmetenda madudu, hamjasingiziwa, mnaambiwa ukweli, hivyo mngeshukuru, na kujirudi, lakini kwa sababu hamuwezi kujirudi na wala si dhamira yenu kufanya hivyo, sababu mmejaa ubinafisi, wa kushibisha matumbo yenu Wenyewe ndo maana mnaona hamtendewi haki na vyombo vya habari, kitu ambacho si kweli na sahihi. kwa kweli jamii ya kawaida ya kitanzania imewachoka, hata haina imani na nyie (CCM), MABADILIKO KTK MAISHA NI MUHIMU HIVYO TUNATAKA MABADILIKO, ACHENI NA WENGINE WAJARIBU NYIE, N HAMKUJARIBU ILA MMEHARIBU.
 
Back
Top Bottom