MWALLA
JF-Expert Member
- Dec 12, 2006
- 16,992
- 10,497
kama amemuita ASSAD ni MMBWA na antegemea chakula kutoka kwa BWANAWAKE hapa inamaanisha hata yeye pia ni MMBWA kwakuwa hataalipoumwa ule ugonjwa BWANA huyohuyo ndio alimpeleka kumtibia hivyo na yeye ni MMBWA wa BWANA HUYOHUYONdugai , spika wa Bunge la JMT, wakati wa press conference yake na waandishi habari jumapili tarehe 14/4/2019 amesikika akimuita Prof. Assad, CAG kuwa ni mbwa anayemng'ata mtu anayemlisha.
Hili ni tusi kubwa kuliko kutokuelewa kwake juu ya neno DHAIFU. Prof. Assad ni muislamu, kumuita mbwa kunaongeza uzito wa tusi.
Hivi, huyu spika Ndugai ana nini kichwani? Huku kutojua uzito wa maneno si pia kunadhihirisha hadharani UDHAIFU wake?
Hivi Prof. Assad akiamua kwenda mahakamani kufungua kesi ya kuchafuliwa jina/kutukanwa (defamation) dhidi ya spika atakuwa amekosea?