N-handsome
JF-Expert Member
- Jan 23, 2008
- 2,453
- 556
Kwani hakuwepo bungeni? wakati wanapitisha hiyo sheria?
Sawa mh Jobo.Yale ni mapungufu ya ubinadamu
Tunataka mtu atakayelinda na kuheshimu katiba aliyoapa kuilinda!JAMANI MIMI NAULIZA SWALI HIVI NI NANI KATIKA JAMII HII YA TANZANIA ANAWEZA AKAWA RAIS AMBAYE HATAKUWA NA WA KUMLAUMU YAANI NCHI INATULIA INAKUWA KIMYA KABISA MAANA NAONA SASA HIVI SIASA ZINANIVURUGA TU ILI TUANZE KUMPIGIA DEBE SASA HIVI
Virusi kunasaa wanachachamaaMh. Ndugai kuna wakati yuko vizuri sana ila sijui muda mwingine huwa anayumba wapi.
Kabisa yaniKwa sababu hakuna muswada wo wote unapelekwa bungeni bila Rais kufahamu!
Hatuna Rais bali picha ya Rais!
Kipindi cha magu kulikuwa na mambo worse zaidi ila tofauti tu na haya..Bwana weee Kwan wakat wa magu
Haya mambo mbona hayakua
Inamaana hawakua wanamuona??
Kwan hiz cod tunazopgwaKipindi cha magu kulikuwa na mambo worse zaidi ila tofauti tu na haya..
Mfano matajiri kukimbiza biashara nchi nyingine huku sisi Watanzania wa chini tukikosa michongo mtaani.
Bora huyu Mama anavyowaacha matajiri watanue watu tupate hata vibarua kwa wingi.
Sent using Jamii Forums mobile app
Anafile mirembe kama mwendazakeLakin hakuna wakat mgumu nchi unapitia
Kama sasa nchi imemshinda huyu mama kwakweli
Hata mm nashangaa Sana wakat yeye ndo Kiongoz waoNdugai si ndo bunge lililopitisha hiyo bajeti?..analialia nini sasa?
Sent using Jamii Forums mobile app
Ishu ya kudiscuss kuhusu tozo na kodi ni kwa namna gani zinatumika..kama zitatumika kama Mama anavyosema tatizo hapo hamna..ila zikianza kutafunwa kiholela shida iko hapo..na itabidi tuseme hatukubali.Kwan hiz cod tunazopgwa
Umuhimu uko wapi n Kama unateseka
Ww kuwalisha walio jaza matumbo yao
Anafile mirembe kama mwendazakeView attachment 1926649
Yani sura yake kama mganga wa kucheza ngoma ya majoka
Tatzo hapa n kutafunwa Kama zile za escrow mkuu hapo ndo kuna shda Ila zikijengaIshu ya kudiscuss kuhusu tozo na kodi ni kwa namna gani zinatumika..kama zitatumika kama Mama anavyosema tatizo hapo hamna..ila zikianza kutafunwa kiholela shida iko hapo..na itabidi tuseme hatukubali.
Nchi itajengwaje bila kodi mkuu?..
Sent using Jamii Forums mobile app
Kitu gani cha CCM chama chako hukuwahi kuunga mkono?Naunga mkono HOJA...
Mh.Spika Ndugai yuko sahihi sana....
Ni lazima wabunge wa hiyo kamati wawe makini ili kuitekeleza vyema ilani bora ya uchaguzi ya CCM......
Spika wa Bunge, Job Ndugai ametishia kuifumua Kamati ya Bunge ya Bajeti baada ya kukerwa na kupitishwa kwa sheria inayoruhusu Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA) kuanza kutoza ushuru wa bidhaa wa asilimia mbili kwa mazao nchini.
Spika Ndugai ameyasema hayo leo Jumatatu Septemba 6, 2021 bungeni mara baada ya majibu ya Wizara ya Kilimo yaliyotokana na swali la nyongeza la Mbunge wa Namtumbo (CCM), Vita Kawawa.
Kawawa amesema wakulima wa tumbaku wamekuwa wanalipa ushuru wa wilaya wa mazao, tozo ya vyama vikuu vya ushirika, chama cha msingi.
Amehoji kama ni kweli kuwa TRA mwaka huu itaanza kuwatoza wakulima wa tumbaku ushuru wa bidhaa.
Akijibu swali hilo Naibu Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe amesema ni kweli Bunge lilipitisha sheria ya ushuru wa bidhaa wa asilimia mbili kwenye mazao ya kilimo.
Hata hivyo, amesema bado wizara haijaanza kukata ushuru huo kwasababu mjengeko wa bei ya tumbaku huamuliwa kati ya Februari hadi Aprili. Amesema wakati sheria hiyo inapitishwa tayari mjengeko wa bei wa zao hilo ulikuwa umeshapitishwa.
Hata hivyo, amesema wizara yake imewasiliana na Wizara ya Fedha na Mipango kwa kuwaandikia ili kuona namna gani watatekeleza sheria hiyo lakini kwa kulinda maslahi ya wakulima wa zao hilo.
Ndugai amesema wajumbe wa bajeti wanapaswa kuwa makini sana katika kazi zao kwasababu mambo yakifika bungeni wanaiamini kamati.
“Mkiendelea hivi nitaifumua hiyo, kamati ya bajeti tumeweka watu tunaowaamini sana. Sasa kama mnaenda kule mnalala tu na kupitisha tu vitu vya kienyeji mnatuponza. mnapitishaje kitu kama hiyo bwana,”amesema.
Mwananchi