Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 137,687
- 272,551
huyu jamaa asipojirekebisha atachezea kichapo cha umma si siku nyingi !
Watapigwa tu mpaka kielweweke--na bado! Yaani hawa wajinga wanakaba mpaka penati wakati kuna mishahara hewa ya Tsh 1.5 bilion imeibiwa na mafisadi wa CCM na hakuna mtu aliyesurubishwa mpaka sasa? Walaaniwe viongozi wote wanaochumia matumbo yao badala ya kuchumia kwa ajili ya maendeleo ya nchi! Wakati wananchi wanakufa kwa njaa, yenyewe yananenepeana kama nguruwe!!! Haya majamaa ni zaidi ya mafisi, maana fisi akila anasaza mifupa--lakini yenyewe yanakula hadi mifupa, huku wananchi wakizidi kukamuliwa kila uchao! Ipo siku kitaeleweka tu.
View attachment 156564
View attachment 156562
View attachment 156563
Umasikini ulionao hautaondoka kwa wivu na kupiga demo kijana fanya kazi kwa bidii
Watapigwa tu mpaka kielweweke--na bado! Yaani hawa wajinga wanakaba mpaka penati wakati kuna mishahara hewa ya Tsh 1.5 bilion imeibiwa na mafisadi wa CCM na hakuna mtu aliyesurubishwa mpaka sasa? Walaaniwe viongozi wote wanaochumia matumbo yao badala ya kuchuma kwa ajili ya maendeleo ya nchi! Wakati wananchi wanakufa kwa njaa, yenyewe yananenepeana kama nguruwe!!! Haya majamaa ni zaidi ya mafisi, maana fisi akila anasaza mifupa--lakini yenyewe yanakula hadi mifupa, huku wananchi wakizidi kukamuliwa kila uchao! Ipo siku kitaeleweka tu.
View attachment 156564
View attachment 156562
View attachment 156563
kazi ipi mbele ya walafi kama hao ?
Dodoma. Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai amenusurika kujeruhiwa na kundi la vijana waliokuwa wakipinga ongezeko la ushuru wa mazao na kuvamia ukumbi wa mkutano wa Kilimo uliopo Kibaigwa, wilayani Kongwa.
Katika vurugu hizo, ambazo zililazimisha polisi kurusha mabomu ya machozi ili kuwatawanya waandamanaji, pia mali mbalimbali ziliharibiwa, likiwemo gari la Mbunge wa Tanga Mjini, Omary Nundu.
Kamanda wa polisi mkoani Dodoma, David Misime alisema vurugu hizo zilitokea juzi saa 7.30 mchana katika Mji mdogo wa Kibaigwa. Alisema jumla ya watu 34 wanashikiliwa wakihusishwa na vurugu hizo.
Misime alisema vijana wanaokadiriwa kuwa zaidi ya 300, wakishirikiana na wabeba mizigo wa Soko Kuu la Mazao la Kibaigwa walifanya maandamano bila kibali na kungoa bango la Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa.
Alisema bango lililongolewa ni la tangazo la kuzuia wafanyabiashara kuingiza mazao sokoni bila kulipa ushuru uliowekwa kwa mujibu wa sheria.
Kamanda huyo alisema viwango vya ushuru vinavyotozwa vilipanda tangu Julai Mosi mwaka jana. Kwa mujibu wa viwango vipya, ushuru wa gunia la kilo 100 za karanga ulipanda kutoka Sh1,000 hadi Sh3,000, gunia la mahindi kutoka Sh500 hadi Sh1,000, dumu la mafuta ya alizeti lilianza kutozwa Sh500, gunia la mashudu Sh1,000 na gunia la alizeti Sh1,000. Viwango hivyo vinapingwa na wabeba mizigo.
Vijana hao wabeba mizigo walifanya fujo kwa kufunga Barabara kuu ya Dodoma Morogoro kwa mawe na kuchoma matairi, pia walivamia maduka na baa za jirani na kupora vinywaji na kuvunja majokofu na kusababisha uharibifu mkubwa, alisema Misime.
Source: Mwananchi
MAONI YANGU:
Ndugai amekuwa akifanya ubabe sana akiwa bungeni. Ikiwa ataendeleza ubabe wake hadi jimboni kwake, wananchi watampasua kichwa. Lakini suluhisho la kudumu kwa wabunge wababaishaji kama hawa ni kuwanyima kura ktk uchaguzi mkuu ujao. WanaKongwa mtoseni huyu adui yenu wa maendeleo ktk uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.
Binafsi hua nashangaa sana. Utakuta mtu kama huyo ukifika wakati wa uchaguzi wananchi wanampa kura za kutosha kabisa kuwa mbunge baada ya kuwapa mlungula wa khanga, vitenge, fulana, kofia, chumvi na sukari lakini mara tu baada ya uchaguzi wananchi haohao wanageuka na kuanza kulalamika.
Mimi nawashauri wananchi wanaobahatika kupiga kura siku ya uchaguzi wachague mwakilishi bila kuangalia chama wala kujali milungula wanayopewa, kisha walinde kura zao mpaka matokeo kutangazwa.
Kuhusu kukoswakoswa kwa mbunge wa Kongwa liwe fundisho kwa wabunge wengine wa aina hiyo.
Namalizia kwa kunukuu kauli ya waziri mkuu wa Tanganyika pamoja na kuiboresha kidogo, "Wale wabunge wanaokaidi matakwa ya wananchi waliowachagua wapigwe tu maana tumechoka sasa, nami nasema wapigwe tu, ee wapigwe"
Umasikini ulionao hautaondoka kwa wivu na kupiga demo kijana fanya kazi kwa bidii