Fisadi Mkuu
Member
- Mar 4, 2011
- 72
- 7
Male |
Zumbe, 2015 ni mbali sana kusubiri katika hali hii. Hatua lazima zichukuliwe mapema. Naanza kupata mantiki ya yule mbunge aliyesema "Tufunge mlango zipigwe"
Wakati mwingine heshima haipatikani kwa kuiomba, bali kuipigania. Hata mnyonge unayemwonea kwa kumtwanga ngumi akiamua kila ukipita anakutungua kwa mawe utaacha kumwonea.
Wananchi ndio wanaotakiwa kukasirika na udhalilishaji kama huu na kuchukua hatua sio kuwaachia wabunge wa upinzani pekee.
Ndungai nilikuwa namuona ana busara sana, kumbe naye wale wale tu!
Na miongoni mwa wapiga kura wake jimboni mwake ni mawaziri waishio mikocheni, makatibu wa wizara na viongozi mbalimbali wa sasa na wastaafu wanaoishi Mbezi Beach, Masaki, Oysterbay na kwengineko.....Siku inakuja.Siku ambayo tutatofautisha nywele za kichwani, za kwapani, za kifuani na kwenginekoits a message kwa wananchi kuwapuuza wao ambao hawajui wananchi wanataka nini. Halima hakuongea kama yeye kama unampuuza halima ina maana unapuuza wapigakura wake wote na watu anaowawakilisha
Nimekupata mkuu lakini hii ni vita na ushindi ndani na nje ya bunge ni muhimu sana.binafsi bado naona ccm wanatumia mbinu dhaifu kuzima hoja nyingi ila cdm haijajipanga kulazimisha hoja za msingi zipewe majibu na wahusika hata kama ni majibu mabovu na si kuzimwa na spika.yule mama spika mwanzo alikuwa anawaogopa waziwazi wabunge wa cdm hadi hofu yake ulikuwa unaweza kuisoma usoni kwake lakini sasa hv anajiamini haswa hata akivurunda!tukumbuke majimbo ya wapinzani hayatapewa kipaumbele kupewa miradi na fedha za kutosha na huku mtaani wananchi wameanza kusema tumechagua upinzani mbona mambo yale yale hakuna hata nukta ya mabadiliko? Lazima tulazimishe kufanyiwa kazi hoja za wabunge wetu na waheshimiwe lakini nao wajipange ili waweze kutimiza malengo yote kwa ufasaha lakini haswa wasigeuzwe walalamikaji tu alafu mwisho kuja kulalamika mitaani bila juhudi za makusudi bungeni.tunataka moto mkubwa zaidi ya huu bungeni maana yapo mengi sana yanayoangamiza taifa.
Nilikuwa nafuatilia Bunge na nikakuta sehemu ambayo walikuwa wanazungumzia suala la Bima za Wabunge - wakijadili kauli ya Kafulila kuwa Wabunge ni "privileged class" kuwa wanapata huduma ya afya wao na watoto wao. Ndugai alipokuwa akijaribu kutoa ufafanuzi alidokeza kitu kuwa wabunge hawana bima ya afya na Bungeni linawafanyia utaratibu. Akatumia muda pia kurusha vidonge vya mwisho na kama utakavyosikia Halima Mdee akataka kupata "taarifa"... well listen
View attachment 33772