Ndoto za mabinti wengi ni harusi

Ndoto za mabinti wengi ni harusi

Kaie

Member
Joined
Oct 9, 2016
Posts
48
Reaction score
24
Ukizungumza na wasichana au wanawake ambao hawajaolewa, unapozungumzia suala la Ndoa, kwa bahati mbaya sana wengi vichwani mwao inajengeka taswira ya harusi.

Ukisema Ndoa yeye anawaza gauni jeupe (Shela) lenye mkia mreeefu na maids wamelishika huku na huku.

Anawaza suti ya mume wake, gari ya kifahari iliyopambwa, sijui wasindikizaji watoto pale mbele.

Anawaza Ukumbini, baharini kupiga picha na mwisho usiku wa Honeymoon.

Ndio maana wengi wanakazana kuchangia harusi za wenzao na kushiriki hata kushona sare ili na yeye kwenye [HASHTAG]#HARUSI[/HASHTAG] yake wamchangie.

Inasikitisha sana kwamba wengi hawafikirii maisha ya Ndoa.

Hawajiulizi maswali ya msingi kama;

1. JE NIKO TAYARI KUWA MKE WA MTU?

2. NIKO TAYARI KUJIDHABIHU KWAAJILI YA FURAHA YA MTU MWINGINE?

3. JE, NIKO TAYARI KUSALIMISHA MATAKWA YANGU KUFANYA MATAKWA YA MTU MWINGINE?
(Surrendering my will)

4. JE, NIKO TAYARI KUWA MAMA NA KULEA FAMILIA?

5. JE, NIKO TAYARI KUPIGANIA NDOTO ZA MTU MWINGINE?

6. JE, NIKO TAYARI KUAMBATANA IKIBIDI KUHAMA MJI NINAOPENDA NA KWENDA KUISHI NISIKOPENDA ILI KUTIMIZA NDOTO YA MUME WANGU?

7. Niko tayari kuingia ukoo mwingine na kuufanya kuwa ukoo wangu, watu wake wawe watu wangu na Mungu wao awe Mungu wangu?

8. Ikitokea umeolewa na Mume wako akapata shida ghafla mfano Ugonjwa na akashindwa kutunza familia, una mbinu gani mbadala ya kuendesha maisha yenu mpaka atakapopona na kusimama tena?

9. Una uwezo wa kubeba majukumu kama Mama maana kuzaa ni jukumu lingine kabisa?

10. Tabia yako vipi?
Inafaa kuwa mke wa mtu?
Au unahitaji muda kwanza na uhuru ujirushe ukichoka ndio utulie uolewe?

11. Kuna msemo "Nyuma ya kila mwanaume aliyefanikiwa kuna mwanamke" ukijiangalia wewe una uwezo wa kumshauri mtu akafanikiwa?

Na hilo tunalipima kwa kuangalia ni nini ambacho binafsi umefanikisha katika maisha yako.

12. Moja jumlisha moja huzaa mbili, wewe una moja gani ya kuchanganya na moja aliyonayo mume wako mkazalisha mafanikio?
Hata ushauri wako kwake ni wa maana sana.

Nadhani kuna mambo ya maana ya kufanya, kupanga na kujiandaa kabla hujawaza rangi ya harusi (Wedding colour), keki ya ngazi saba na hotel ya kwenda Honeymoon.

Me nimemaliza.
Kwa usawa huu hakuna mwanaume anataka kuoa mke asiyejishughulisha hata kama ni kuuza karanga, mchicha, duka, ofcn nk maadamu unajishughulisha.

Usije ukaishia kufurahia harusi na baada ya mwaka ukaanza kutafuta Washauri wa Ndoa.

Na kwa mwanaume mpe nafasi mkeo hata ya kumfungulia biashara ili msaidiane ktk majukumu.
 
Ukizungumza na wasichana au wanawake ambao hawajaolewa, unapozungumzia suala la Ndoa, kwa bahati mbaya sana wengi vichwani mwao inajengeka taswira ya harusi.

Ukisema Ndoa yeye anawaza gauni jeupe (Shela) lenye mkia mreeefu na maids wamelishika huku na huku.

Anawaza suti ya mume wake, gari ya kifahari iliyopambwa, sijui wasindikizaji watoto pale mbele.

Anawaza Ukumbini, baharini kupiga picha na mwisho usiku wa Honeymoon.

Ndio maana wengi wanakazana kuchangia harusi za wenzao na kushiriki hata kushona sare ili na yeye kwenye [HASHTAG]#HARUSI[/HASHTAG] yake wamchangie.

Inasikitisha sana kwamba wengi hawafikirii maisha ya Ndoa.

Hawajiulizi maswali ya msingi kama;

1. JE NIKO TAYARI KUWA MKE WA MTU?

2. NIKO TAYARI KUJIDHABIHU KWAAJILI YA FURAHA YA MTU MWINGINE?

3. JE, NIKO TAYARI KUSALIMISHA MATAKWA YANGU KUFANYA MATAKWA YA MTU MWINGINE?
(Surrendering my will)

4. JE, NIKO TAYARI KUWA MAMA NA KULEA FAMILIA?

5. JE, NIKO TAYARI KUPIGANIA NDOTO ZA MTU MWINGINE?

6. JE, NIKO TAYARI KUAMBATANA IKIBIDI KUHAMA MJI NINAOPENDA NA KWENDA KUISHI NISIKOPENDA ILI KUTIMIZA NDOTO YA MUME WANGU?

7. Niko tayari kuingia ukoo mwingine na kuufanya kuwa ukoo wangu, watu wake wawe watu wangu na Mungu wao awe Mungu wangu?

8. Ikitokea umeolewa na Mume wako akapata shida ghafla mfano Ugonjwa na akashindwa kutunza familia, una mbinu gani mbadala ya kuendesha maisha yenu mpaka atakapopona na kusimama tena?

9. Una uwezo wa kubeba majukumu kama Mama maana kuzaa ni jukumu lingine kabisa?

10. Tabia yako vipi?
Inafaa kuwa mke wa mtu?
Au unahitaji muda kwanza na uhuru ujirushe ukichoka ndio utulie uolewe?

11. Kuna msemo "Nyuma ya kila mwanaume aliyefanikiwa kuna mwanamke" ukijiangalia wewe una uwezo wa kumshauri mtu akafanikiwa?

Na hilo tunalipima kwa kuangalia ni nini ambacho binafsi umefanikisha katika maisha yako.

12. Moja jumlisha moja huzaa mbili, wewe una moja gani ya kuchanganya na moja aliyonayo mume wako mkazalisha mafanikio?
Hata ushauri wako kwake ni wa maana sana.

Nadhani kuna mambo ya maana ya kufanya, kupanga na kujiandaa kabla hujawaza rangi ya harusi (Wedding colour), keki ya ngazi saba na hotel ya kwenda Honeymoon.

Me nimemaliza.
Kwa usawa huu hakuna mwanaume anataka kuoa mke asiyejishughulisha hata kama ni kuuza karanga, mchicha, duka, ofcn nk maadamu unajishughulisha.

Usije ukaishia kufurahia harusi na baada ya mwaka ukaanza kutafuta Washauri wa Ndoa.

Na kwa mwanaume mpe nafasi mkeo hata ya kumfungulia biashara ili msaidiane ktk majukumu.
ULitaka WAOTE MIMBA??
 
wengi hawajui tofauti ya harusi na ndoa. wanadhani kitu kimoja.
 
UNAJUA MUNGU AWEZI RUHUSU WOTE TUOE KUNA WALIOPEWA NYOTA YA KUTUTUNZIA WAKE ZETU WATARAJIWA ANAPOPATIKANA SAHIHI ANAKUACHA


SO USIOGOPE ENDEELEA KUWATUNZIA
yaani kuna muda najiuliza wakati mungu anaumba mwanamke kutoka kwenye ubavu wangu wa kushoto ule wa kulia aliupeleka wapi
 
Ndio sababu hadi leo naogopa sana kutaka kuoa
Time is against us. Nyie ambao mnaogopa kuoa, mtashangaa mnafika 60 hamna partners, watoto wa kuwasaidia. Na vile vile kila mtu unayemjua mtasikia tu habari kafariki. Ushauri, oeni tu, yote hayo ni changamoto. Ukioa unapata rafiki wa maisha.

-callmeGhost
 
Ngoja nikae kwa hapa, labda atapita nione nini atakacho comment....
 
Tatizo watu mnacomplicate sana mambo ndio maana vijisichana vingi na vijanaume vingi ndoa zinawashinda,mwanaume nimeoa mwanamke nikiwa chuo mwaka wa pili tena kwa bajeti ya BOOM tu wala sikuchangiwa hata senti tano lakini ndoa ilifanyika na maisha yalianza na ndoa hadi sasa mwaka wa tatu wala haina NYUFA.Wanaume wenye kujituliza kabla ya 30 wanakua wameshaoa na mwanamke wenye tabia njema na wanaojari heshima zao kabla ya 30 wanakua wameshaolewa.
NB;Ukimuamini mungu na ukaamua kuoa ili uepukane na zinaa mungu hawezi kukutupa na riziki utapata,matatizo hayaepukiki hata ukae bila kuoa mpaka miaka sitini matatizo yatakupata tu na hauwezi kua masikini kwasababu ya ndoa
 
Hii imebase upande mmoja. Vijana was siku hizi na wenyewe wanapenda maisha ya mafanikio haraka. Mara chache ndoa za siku hizi utakuta kijana anaoa mwanamke asie na kazi.
Hawapendi kumuemdeleza mke wake na hata kama Ana ndoto za biashara au elimu ni wanaume 1 kati ya 10 atamsaidia kufika malengo.
Wanaume hawa hawa anapenda mke mrembo, wa kisasa lakini hawako tayari kumhudumia na kuhakikisha anapendeza!
Mume unakuta anataka kodi alipe nusu na mke nusu, likewise kwa matumizi mengine ya ndani!
Wengi wao huwa wanafikiria ndoa ni kufungua zipu tu. Likija swala la majukumu mnaanza ku dodge....
Wanaume wana expect mke a sacrifice her happiness ila wao wabaki kama walivyo!
Mke abaki home, afue, apike,afanye usafi na kulea watoto wakati yeye yuko bar na marafiki!The lady would as well have loved to hang out with her friends!Kwanini usibaki nyumbani talk her and give her company to make the chores seem lighter!
Ndo sio lele mama... mkitaka kufaidi stand by your partner ila sio kumfanya ajute
 
Mimi ndio Maana nawagonga nawabanjua then nawatema nasepa mbele...

Wazo la kuoa sina hata nukta....
GONGA BANJUA PIGA CHINI SEPA MBELE. OVER.

[HASHTAG]#Chief[/HASHTAG] Eng
 
Back
Top Bottom