Ndoa zina matukio jamani

Mkuu mbona kama
"Unatufokea...
 
Ndoa ni jambo la kheri na changamoto ndio zinazofanya tunaishi japo sikuhiz ukiingia ndoan ni kama umeenda jela
Kuna mtu alsemaga ukiingia ndoani miaka hii hakikisha unajifanya akili zako sio timamu πŸ˜ƒπŸ˜ƒ
Ila ndoa raha kila mtu akiwa anajua thamani ya mwenzie.

Bahati mbaya watu sasa wanaishi nyumba moja ila wapo matumatu hawaaminiani tena.
 
Bro kutambua thamani ya mwenzio na to cherish it ni jambo linahitaji maamuzi yasiyo na unafiki ndani yake...
Tatizo ni wanawake ...Mwanamke anaweza kuishi na kuolewa na mwanaume ambaye hampendi labda kalazimishwa na wazazi ila mwanaume hawezi kabisa.


Mbaya ni kwamba duniani unajua tu mtu unayempenda na humjui anayekupenda.
 
Komenti yako ya kwanza nimeipotezea, ila sasa naona umedhamiria
Yaani kama unanisema mimi


Mimi huwa ninaamini ndoa inahitaji uingie na akili zako timamu, ila wewe unasema tusiingie na akili timamu

Usinivuruge tafadhali
πŸ˜ƒπŸ˜ƒNdugu usifanye hilo kosa la kuingia na akili namaanisha unaoana na mtu hamfanani chochote hawez kuwa unavotaka Sasa ukitaka utimamu πŸ’― ndo utaharibu inabid nawe ulegeze fuvu πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Komenti tulivu sana.

Unajua hili suala la ndoa watu tunalikompliketisha sana.

Ni kweli ndoa za siku hizi zimekuwa ni delicate sana, na zina misukosuko mingi.
Lakini hii haina maana ndoa ni jambo lisilofaa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…