Asprin
JF-Expert Member
- Mar 8, 2008
- 68,012
- 95,355
Kaka I feel your feelings!! But with due respect kaka sometimes inabidi nanyi mara moja moja muwe mnayatia mapenzi chachu hata kwa kufanya kakitu kadogo kuonyesha kuwa unamsaidia wife. Sio unakuta mwingine kaka yeye anachojua ni kufanyiwa tu mfano
1. Anaamka asubuhi anakuamsha ukamwekee maji kwenye ndoo (na yanatoka bombani na ni master bedroom)
2. Umwekee dawa ya meno kwenye mswaki (usipoweka ataoga kisha atatoka kuja kuulizia mswaki wake)
3. Anatoka bafuni (hapo unakuta pant yake kaivua kaitupia kwenye sink anasubiri uje uife!)
4. Akitoka ushampigia pasi anavaa, anakunywa chai ulomwekea kisha huyooo funguo za gari zi wapi na akifika ndani ya gari ni honi mtindo mmoja unamchelewesha na usipokimbia na viatu mkononi anakuacha unakwenda ofcn kwa daladala au ukifanikiwa kuingia kwenye gari basi kusemwa mtindo mmoja unamchelewesha teke.
MCHANA KUTWA HATA KUKUPIGIA SIMU YA SALAMU AU SMS YA I MISS YOU!
5. Akirudi jioni akute chai yake mezani na maji bafuni
6. Atizame TV huku akisubiri chakula au asome magazeti yake
7. Akishakula huyooo kitandani analala huku akisubiri wewe uje ushushe neti na kumfunika na shuka!
8. Uingie kitandani baada ya kumaliza kazi zako akudake tayari kwa chakula cha usiku.
The life continues!
Kwa style hii kweli unategemea mkeo atakuwa anamapenzi na wewe? Si atajihisi hana tofauti na huyo housegirl jamani!
Jamani mara moja moja ukinisaidia kushusha net au hata kunipigia na mimi pasi I tell you nitaikumbuka kwa muda mrefu na moyo wangu kukongwa vilivyo!!
MJ1 kumbe mmeo anakutendea wema. Mi hayo yote uliyoyataja ndio zangu kasoro hiyo red kwangu inakuwa hivi:
5. Nikirudi jioni napitia bar kupata mija moto moja baridi
6. Nikitoka bar ni moja kwa moja kitandani kwakuwa nakuwa nimeshafakamia makongoro au mkia na ndizi kadhaa. Msosi kula na wanao.