Ndoa yangu inakaribia kuvunjika,msaada jamani

Ndoa yangu inakaribia kuvunjika,msaada jamani

Kima mdogo

JF-Expert Member
Joined
Sep 17, 2011
Posts
303
Reaction score
46
Mimi ni mpare na mume wangu ni mchaga (MMACHAME)....ndoa yetu ina miaka 6 na miaka yote tumeishi kwa furaha na upendo..Mumgu ametujalia watoto 2 mkubwa 5yrs wa kike mdogo 3 month wakiume...Toka nijifungue mtoto huyu wa kiume mume wangu amepunguza mapenzi na mimi na wala hampendi kabisha huyu mtoto,Nilipomuuliza anadai dada zake wamemweleza kuwa kuzaliwa kwa mtoto huyu ndio mwisho wa maisha yake,Eti mimi nitamuua sbb wapare wanatabia ya kuua waume zao punde wapatapo watoto wa kiume. Yn naumia sana roho kwani nilidhani mtoto angekua furaha kwa mume wangu kumbe amegeuka hofu kwake,Nifanyaje jamani
 
mmeo ana miaka mingapi?
Kapita hata ngumbaru?

Mna maelewano kweli ana unahisi mna maelewano?
 
Mimi ni mpare na mume wangu ni mchaga (MMACHAME)....ndoa yetu ina miaka 6 na miaka yote tumeishi kwa furaha na upendo..Mumgu ametujalia watoto 2 mkubwa 5yrs wa kike mdogo 3 month wakiume...Toka nijifungue mtoto huyu wa kiume mume wangu amepunguza mapenzi na mimi na wala hampendi kabisha huyu mtoto,Nilipomuuliza anadai dada zake wamemweleza kuwa kuzaliwa kwa mtoto huyu ndio mwisho wa maisha yake,Eti mimi nitamuua sbb wapare wanatabia ya kuua waume zao punde wapatapo watoto wa kiume. Yn naumia sana roho kwani nilidhani mtoto angekua furaha kwa mume wangu kumbe amegeuka hofu kwake,Nifanyaje jamani
Duh, kuna imani nyinigine hata shetani mwenyewe hazikubali. Sasa hao dada zake walikuwa wapi kumwambia wakati anakuoa? Kwani wakati mnaoana hawakujua kwamba katika ndoa kuna kuzaliwa mtoto wa kiume au wa kike? Omba nafasi ya mzungumzo rasmi na mmeo juu ya hilo. Maana kuna uwezekano dada zake hawakupendi na hivyo wanatafuata sababu ya mmeo kuachana na wewe. Jaribu kutafuta kiini cha dada zake kuamua kumwambia hayo kaka yao.
 
Labda wapare wa MACHAME mana wao ndo wanadaiwa walikua na tabia ya kufanya matukio kama hayo,Au wanataka kukugeuza hela.wapare original kama mimi hawauwi waume zao hata siku 1 awe tajiri au mpate mtoto wa kiume,Wapare wana mapenzi ya dhati.
 
Na wewe uliolewa na zombie squared. Yaani linaambiwa maneno na dada zake afu linakuja kuhofia home. Lidharau, acha likutaliki usepe, kirundu kabisa!
 
Ndo kazi ya mawifi hiyo,ukizaa tabu,usipozaa tabu cha msingi potezea wao watakua wanavuta bange hao.
 
Huyo mumeo nae njegele kabisa,kaa nae ongea nae kwa kina ila kama ndo ana akili za kushikiwa basi tena
 
Muteni MCHUNGAJI/MGANGA/SHEIKH kutokana na IMANI YENU aje AFUNGE NA KUIKEMEA ROHO YA MAUTI HAPO NDANI!!!!!!! Ikibidi MUAPIZANE KIMILA ili yeyote ATAKAE MTANGULIZA MWENZIE KATI YENU AWAHI YEYE!!!!!!!! IMANI KITU KIBAYA SANA KIKISHAMKAA MTU ROHONI MDA WOTE ANAKUWA HANA AMANI NA WA KUHISIA UBAYA TU!!!!!!!
 
Na wewe uliolewa na zombie squared. Yaani linaambiwa maneno na dada zake afu linakuja kuhofia home. Lidharau, acha likutaliki usepe, kirundu kabisa!
mme ekaiwe na vadada vakwe,ni igonji levendiwe ni mbua
 
Daaaah! Hii kali! Kaa chini na mumeo muongee!

Hizi imani nyingine bhana!
 
nasikia ukiolewa na mmachame hakikisha hana madada,kama ana dada bora usiolewe nae.pole sana vumilia tu hilo nalo litapita
 
Mimi namlaumu mumeo,inakuaje mazoea yamuamulie maisha ya leo?

Hebu tulia,jitahidi kumwonesha kwa vitendo kuwa unamjali na unamwona wa thamani,inaweza kumsaidia akapunguza hofu!
 
Huyo mumeo pamoja na kuoa..bado ana element za kutawaliwa na ndugu zake. Mwananume anaejielewa hawez kufuata mawazo ya kijinga kama hayo ktk kwa dada zake.... Kama unammudu,kaa nae mueleze unavyokereka afahamu..mawazo ya kizaman sana hayo..
 
Back
Top Bottom