Kabewa
Senior Member
- Oct 30, 2009
- 136
- 56
Mgombea Urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Wilbroad Slaa bado anateswa ishu ya ndoa na sasa kila anapokwenda kujieleza, analazimika kutoa ufafanuzi kuhusu mke wake.
Uchunguzi wa gazeti hili tangu vuguvugu za kempeni za Uchaguzi Mkuu 2010 zianze, umebaini kuwa Dk. Slaa amekuwa akiulizwa swali kuhusu ndoa yake kutokana na kuwepo na taarifa za mkanganyiko kuhusu mambo yake ya kifamilia.
Imebainika kuwa swali kuu kwenda kwa Slaa ambalo limezua matawi mengi ni kile kinachojulikana na wengi kwamba mke wake, Rose Kamili ni kada wa Chama Cha Mapinduzi, aliyewahi pia kushika nyadhifa kadhaa ikiwemo udiwani.
Katika mchakato wa kura za maoni ndani ya CCM, Rose aligombea ubunge lakini kura hazikutosha na kukawa na taarifa kwamba alitishia kuhamia CHADEMA kumfuata mumewe (Slaa).
Jumamosi iliyopita kwenye Kipindi cha Jicho Letu Afrika cha Radio Clouds FM, Slaa alisema kuwa Rose kwa sasa si mke wake na kwamba mke wake mpya anaitwa Josephine Slaa.
Slaa, akijibu swali la mtangazaji wa kipindi hicho, George Njogopa alisema, suala la Rose lilizua mgogoro mkubwa lakini hatimaye waliachana na yeye kupata mke mwingine.
Ni demokrasia, sikuwa na sababu ya kumbana ndiyo maana nilimuacha aendelee na majukumu ya chama chake. Hata hivyo, ni vizuri watu wakatambua tofauti za ndani ya chama na familia, alisema Slaa.
Wakati akizungumza hivyo redioni, baadaye siku hiyo akiwa Uwanja wa Jangwani, Dar katika uzinduzi wa kampeni zake za urais, Slaa alilazimika kumpandisha mkewe jukwaani ili kutuliza mzuka wa mashabiki wake waliojitokeza kwa wingi.
Jamani ndiye mke wangu, anafanya kazi kubwa sana kunitunza na hasa katika kipindi ambacho nilikuwa nimeumia mkono, alisema Slaa na kumtaka Josephine asimame ili awasalimu wapigakura.
Hata hivyo, wapigakura walilalamika kwamba Josephine alisimama mbali, hivyo akaombwa kusogea karibu na kupunga mkono.
Katika uchunguzi wetu, suala la ndoa ya Slaa limekuwa mjadala ndiyo maana amekuwa akilazimika kutoa ufafanuzi mara kwa mara ili jamii ijue ukweli kwamba yule wa zamani hayupo naye tena.
Inafunuliwa kwamba jitihada za Slaa kutaka jamii ijue yeye hayupo na Rose badala yake amemuoa Josephine ni kutaka dhamira yake ya kupingana na Chama Cha Mapinduzi isitiliwe shaka na wapigakura wenye kiu ya mabadiliko
Source Global publisher
Uchunguzi wa gazeti hili tangu vuguvugu za kempeni za Uchaguzi Mkuu 2010 zianze, umebaini kuwa Dk. Slaa amekuwa akiulizwa swali kuhusu ndoa yake kutokana na kuwepo na taarifa za mkanganyiko kuhusu mambo yake ya kifamilia.
Imebainika kuwa swali kuu kwenda kwa Slaa ambalo limezua matawi mengi ni kile kinachojulikana na wengi kwamba mke wake, Rose Kamili ni kada wa Chama Cha Mapinduzi, aliyewahi pia kushika nyadhifa kadhaa ikiwemo udiwani.
Katika mchakato wa kura za maoni ndani ya CCM, Rose aligombea ubunge lakini kura hazikutosha na kukawa na taarifa kwamba alitishia kuhamia CHADEMA kumfuata mumewe (Slaa).
Jumamosi iliyopita kwenye Kipindi cha Jicho Letu Afrika cha Radio Clouds FM, Slaa alisema kuwa Rose kwa sasa si mke wake na kwamba mke wake mpya anaitwa Josephine Slaa.
Slaa, akijibu swali la mtangazaji wa kipindi hicho, George Njogopa alisema, suala la Rose lilizua mgogoro mkubwa lakini hatimaye waliachana na yeye kupata mke mwingine.
Ni demokrasia, sikuwa na sababu ya kumbana ndiyo maana nilimuacha aendelee na majukumu ya chama chake. Hata hivyo, ni vizuri watu wakatambua tofauti za ndani ya chama na familia, alisema Slaa.
Wakati akizungumza hivyo redioni, baadaye siku hiyo akiwa Uwanja wa Jangwani, Dar katika uzinduzi wa kampeni zake za urais, Slaa alilazimika kumpandisha mkewe jukwaani ili kutuliza mzuka wa mashabiki wake waliojitokeza kwa wingi.
Jamani ndiye mke wangu, anafanya kazi kubwa sana kunitunza na hasa katika kipindi ambacho nilikuwa nimeumia mkono, alisema Slaa na kumtaka Josephine asimame ili awasalimu wapigakura.
Hata hivyo, wapigakura walilalamika kwamba Josephine alisimama mbali, hivyo akaombwa kusogea karibu na kupunga mkono.
Katika uchunguzi wetu, suala la ndoa ya Slaa limekuwa mjadala ndiyo maana amekuwa akilazimika kutoa ufafanuzi mara kwa mara ili jamii ijue ukweli kwamba yule wa zamani hayupo naye tena.
Inafunuliwa kwamba jitihada za Slaa kutaka jamii ijue yeye hayupo na Rose badala yake amemuoa Josephine ni kutaka dhamira yake ya kupingana na Chama Cha Mapinduzi isitiliwe shaka na wapigakura wenye kiu ya mabadiliko
Source Global publisher