Ndoa inaelekea kunishinda

Ukishamchomea ndani.. umeshafikiria hatma yako baada ya hapo?...
Maisha lazima yaendelee..ndio viapo vya "Kwa raha na shida"...

Sent from my SM-A405FN using JamiiForums mobile app
 
Bado naendelea kuona maajabu ya wanaume wa jf!

Utaskia piga chini!😂 (mtoa mada angekua wa kiume)

Dada kuwa busy na mimba yako usimfuatilie utajiumiza kitu ambacho si sawa kwa hali ulionayo.

Ndivyo walivyo.. inawezekana hakukuonesha kipindi chote cha hiyo 5 yrs ya mahusiano ila sasa ameona yupo free ameshakuoa na huna pa kwenda au cha kumfanya kwa kuwa unampenda.
 

Wazo la kumchoma moto litoe kabisa mawazoni mwako,huyo ni shetani mbaya anakuchochea ukishatimiza hiyo azma anakuacha kisha unabaki na majuto mengi.. Uko tayari kujifungua ukiwa jela? PLEASE NO..!
Ishu ya kutoshika simu yake ni the best option.. Matatizo acha yaje yenyewe usiyatafute
Ishu ya kutumia condom ni sahihi pia lakini nyie mkiwa kama wanandoa mnaongeza UFA mkubwa, na pia kumbuka kuna magonjwa mengine kama hepatitis B huo ni afadhali hata ukimwi.. Kuna ishu pia ya magonjwa ya kiroho kama nuksi, mapepo, kupungua kwa kinga za kiroho, kuibiwa nyota, kutekwa na jini mahaba nknk

Kuna ishu nyingine hapa ambayo huwa wengi hawaijadili, sometimes mwanaume kuwa malaya wakati mkewe akiwa mjamzito ni side effect za mimba, kama zile hali zinazompata mwanamke za kutapika, kukosa hamu ama kutamani vyakula fulani fulani, nk kuna baadhi ya wanaume huamkwa na pepo baya la ngono na baada tu ya kujifungua pepo husepa
Kwa sasa shughulika na mtoto aliye tumboni ili asiathike afya ya akili tangu tumboni
 
Huyo mumeo hajaanza kukusaliti Jana wala Leo au baada ya ndoa ulikua unajua tabia yake since mwanzoni but ulijipa moyo atabadilika akikuoa au ulikomaa sana na ndoa ukitaka kuwakomesha wanawake wenzako mliokua ktk kinyang'anyiro cha kuvaa shela.
Tatizo wanawake wengi tunafia ndoa au tunang'ang'ania kuolewa hata km unaona mwanaume kimeo haswaa ndoa za kanisani wadada wanaamini wakiolewa hawaachiki wao ndo wao hapo ndo tunafeli...mwanaume anakuoa na mambo yake anafanya
Nakuja kukushauri:Angalia mema yake na mabaya yake then pima mzani mzani ulikoelekea!ila mwaka mmoja baado sana!
Halafu una kiumbe tumboni tulia usijemdhuru mtoto akaziliwa na shida
La mwisho usipende saaana kupekenyua pekenyua kipindi hiki utamuumiza mtoto na kama huwezi muacha mwanaume usimchunguze!!!
 
Mbona wewe mwenyewe una jichanganya kumpa ushuri,sas akimuacha aendelee kuchepuka ataepukaje na kuletewa magonjwa?usiwe double standard.
 
Asante
 
Huna haja ya kuwashirikisha watu wa nje kwa sasa, nyie ndio watatuzi wa msingi kwenye hili tatizo na mengine ndani ya ndoa.. Mkishindwa kuyamaluza ndani nje itakuwa ngumu
All in all mpe muda kama kweli msamaha alioomba amemaanisha utajua tuu lakini kama ni tabia yake YATAJIRUDIA TENA NA TENA
 
Umemaliza kila kitu
 
✅✅✅✅✅
 
Pole sana best usifikie hukoo!vumilia Lea mwanao atabadilika huyoo!ondoa mawazo hasi au kumfanyia mambo mabaya utafungwa na kusababisha matatizo
Acha kumfatilia na hao wanawake zake unajitia presha buree!
 
Mimi mwenyewe swala la condom tena wanandoa linanipa wakati mgumu Ila sasa nafanyaje mtu mwenyewe ana miaka 30 Ila hasikii dah! Inaumiza sana yani hata haogopi magonjwa Ila itabidi tu tutumie Sina namna Mimi ni muoga sana wa magonjwa yani nisipotumia nae Kinga nitawashwa kumfatilia Ila nikitumia kidogo naweza nikajicontrol kumfatilia
 
Ushauri wako una nguvu za Giza aseeehh!achepukee!two wrong can't make it right man!
 
Shirikisha watu wazima katika hilo tatizo usikae nalo peke yako. Nenda kwa shangazi au mama mkwe wako umweleze watakusaidia.

Vijana wengi wanapooa uwa wanakuwa wagumu kuachana na tabia za ujana mpk upite muda kidogo.
Usifikirie kuondoka kabla ya kusolve hiyo kesi ukiona habadiliki ndio unaweza kuchukua hatua nyingine.
 
Kwa sasa usifanye nae mapenzi, atakuletea magonjwa utaumia zaidi, na usimuulize kitu chochote kuanzia sasa ingawa najua ndo atapata nafasi ya kufanya ujinga wake.

Kama kweli hataki kukupoteza, ukamnyamazia kila kitu, utaona akiumia mwenyewe, usimjibu tusi lolote kaa kimya akilala nje usimuulize kalala wapi. Kama anakujitaji atabadilika, kama hakuhitaji utaona akifurahia hiyo hali .

Jitahidi umalize miaka miwili tuone, ikishindikana baada ya miaka miwili omba taraka, usijitafutie kifo mwenyewe.

Kuna dada mmoja yamempata kama yako baada ya miezi 7 ya ndoa, mwanzoni mwanaume alikuwa akiomba msamaha, siku wamegombana kwa hasira mme akafunguka.

" kwanza wewe ndo ulikuwa ukilazimisha ndoa kisa umri umeenda mimi nilitaka tuendelee kusomana kwa muda zaidi, miaka miwili ilikuwa haitoshi mimi kufanya maamuzi . ndio na mimi ni mtu mzima ila na fulani nampenda nashindwa kumuacha"

Hapo ndo dada wa watu amejua kuwa hakuna mapenzi, dada ana 34 mwanaume ana 38.

Wiki iliyopita ilikuwa wiki ya sheria , dada alikuja kuomba ushauri afanye nini. Nimesituka nikajua ni wewe ila mwisho nimejua sio wewe naana yeye bado hana mimba.

Kweli ndoa ni ngumu.
 
Pole sana dada lakn nachoweza kukushauri ni kuwa mvumilivu ili mradi anakuomba samahani atapunguza ama kuacha kabisa bahati mbaya hao michepuko nao hawawezi kudondoka wote ghafla mpe muda awatoe taratibu kabla hujafanya maamuzi yako, usikute ameanza nao kabla yako na kaamua ww ndo akuweke ndani maana ake ww ndo mwenye mme tulia sana. Ila kama ameanza nao wakati mko kwenye ndoa hiyo itakuwa tabia yake. Fanya kile moyo unataka ili usiumize mtoto wa tumboni.
 
Either uhuni ni hulka yake au kuna nguvu za giza. Shetani hapendagi kuona watu wana furaha. Wewe cha kwanza kama una wifi yako mnaelewana mwambie. Mimi naamini dada wa mumeo hawez yaanika mapungufu ya mdogo ake. Akiendelea na hiyo tabia basi hakufai.

Sio kila ndoa ni lazima mzeeke pamoja. Kuliko kua na mawazo ya kuua bora urudi kwenu aibu utaipata kwa muda mchache lakini utakua na amani ya moyo kwa muda mrefu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…