Ndizi zinazoivishwa kwa umeme Je ni kweli zinawekwa dawa ya kuhifadhia maiti?

kabwigwa

JF-Expert Member
May 17, 2014
933
1,533
Wakuu habari zenu,Katika pita pita zangu masokoni nikakutana na hizi ndizi maarufu kama “ndizi za container” au “ndizi za umeme”.Kilichonistua ni maandalizi ya ndizi hizo mpaka kuiva.Mechanism nzima ni siku tatu mpaka nne ndizi inakua imeiva.Mechanism hii ndiyo iliyonifanya niandike uzi huu.Ndizi mbichi inapigwa dawa ya kukausha utomvu kisha inaingizwa kwenye container kisha inapigwa dawa ya kuiva haraka,kubadili rangi na dawa ya kufanya ndizi ikae muda mrefu bila kuharibika(rumor has it wanaweka dawa ya kuhifadhia maiti).Container linakua na heater ambayo husaidia ndizi kuiva,baada ya siku tatu ndizi inakua imeiva then inapoozwa na kupelekwa sokoni kuuzwa kwa wafanyabiashara na mlaji wa mwisho.
Wanasema “No research no right to speak “ mimi nimeongea ila ni aiomba serikali kupitia TBS na ofisi ya mkemia mkuu kufanya uchunguzi wa kina na kuujulisha umma kama Kuna madhara yoyote kuhusiana na ndizi hizi ambazo zimekua zikiuzwa kila kona Dar Es Salaam sijajua mikoa mingine kama zipo.Ndizi hizi ni aina ya Malindi ni kubwa nene na zina rangi nzuri ya kuvutia.
Nb:Sipo hapa kuharibu biashara za watu bali kutoa tahadhari kwa walaji wa ndizi hizo wanaokula wakiamini wanaimarisha afya kumbe wanaziharibu kwa kula kemikali.

775C47DE-41DD-4EFA-9E71-63605209D825.jpeg


4F7AC76E-3F48-4B5A-BBBE-B2A038C22A39.jpeg
 
hizi story zinajirudia rudia, ni sawa na kipindi flani kulizuka kwamba usipokuta nzi buchani basi hiyo nyama imewekwa dawa ya kuhifadhia maiti, hiyo yote nahisi ni kusadikika tu.
 
Aisee hizi ndizi zimejaa pale gongo la mboto mwisho kituo cha daladala mpaka 150 moja, Nilijiuliza mbona nyingi halafu nene sana na zakuvutia? Pia zinaonekana zinatoka au wauzaji wananunua sehemu moja mana wauzaji wote ndizi zinafanana. Inaweza kuwa kweli au kuna kitu kinacho endana na hilo usemalo, Mi nitafuatilia mana nilitia shaka pia
 
mbona hili jipya mkuu,hivi unajua thamani ya dozi moja tu ya dawa za kukaushia maiti?

maana ungejua thamani yake bas ndiz moka ingeuzwa elf 2 kwa kipande
Sijui bei ila kama zinapatikana hawawezi kuweka? Inaweza ukaweka hata kwa kuspray nk Na vipi kuhusu chemicals nyingine?
 
Ni kweli wanaweka dawa fulani ya kuhifadhia maiti wala sio story za vijiweni kwahiyo eat for your own risk
 
Hamu yangu ya Ndizi mbivu imeishia hapo Never Again bora futari za Matunda mengine sio Ndizi za Dar

Byebye Ndizi mbivu
 
Ni kweli kabisa ili alisemalo mtoa mada,muda sio mrefu sana nilipitaga maeneo ya karume kwenye zile kota nikakuta karibia nyumba nyingi makontena kuuliza ndio nikaambiwa ivyo nikashangaa,kwenda mbele nikakuta mafuso yamepaki yanashusha ndizi mbivu nikashangaa sana,Mpaka hapo najua ndizi ni kweli zinaivishwa na makontena ya Umeme,ila iyo ya kuwekea dawa za kuhifadhia maiti sijalifahamu...ngoja nami nitafanyia uchunguzi wangu kwa wale wahusika
 
😂😂 ningeziona nisingekuja humu wadau wanawezanisaidia
Kuivisha ndizi watumie vibweka vyote hivyo? Kwa wale watu kutoka Kilimanjaro wanajua ukitaka ndizi ziive haraka dawa zake ni zipate joto. Wanaziweka darini, kufunika na masagasaga ya migomba, na kukoka moto utoe moshi mwingi. Ikiwezekana kwenye moto wanaweka aina ya majani mabichi ili moshi uwe mwingi. Hivyo basi nadhani wanaziweka kwenye container na huenda wanalifunika au kusiliba container ili hewa isiingie na joto libaki ndani. Na umeme inaweza kuwa ni source ya joto. Hayo mengine kwangu nadhani ni hekaya za abunuasi kama zamani tulivyokuwa tunadanganywa wauza ice cream wanakwenda kuchukuwa mabonge ya barafu motuary. Baada ya kukua nikagundua kumbe kule hata ahakuna mabonge ya barafu
 
Yani upige dawa ndizi ziive kwa siku tatu? Si ndio muda wake wa kuiva huo. Ukivundika ndizi ndani ya siku tatu zinaiva. Alafu wabongo muache kuona kama chemicals ni sumu, inategemeana maana mwilini zipo za aina nyingi mfano hizi hormones.

Sasa unakuta mazao yamepigwa gibberrelic acid unalia unasema ni kemikali hatari
 
Wakuu habari zenu,Katika pita pita zangu masokoni nikakutana na hizi ndizi maarufu kama “ndizi za container” au “ndizi za umeme”.Kilichonistua ni maandalizi ya ndizi hizo mpaka kuiva.Mechanism nzima ni siku tatu mpaka nne ndizi inakua imeiva.Mechanism hii ndiyo iliyonifanya niandike uzi huu.Ndizi mbichi inapigwa dawa ya kukausha utomvu kisha inaingizwa kwenye container kisha inapigwa dawa ya kuiva haraka,kubadili rangi na dawa ya kufanya ndizi ikae muda mrefu bila kuharibika(rumor has it wanaweka dawa ya kuhifadhia maiti).Container linakua na heater ambayo husaidia ndizi kuiva,baada ya siku tatu ndizi inakua imeiva then inapoozwa na kupelekwa sokoni kuuzwa kwa wafanyabiashara na mlaji wa mwisho.
Wanasema “No research no right to speak “ mimi nimeongea ila ni aiomba serikali kupitia TBS na ofisi ya mkemia mkuu kufanya uchunguzi wa kina na kuujulisha umma kama Kuna madhara yoyote kuhusiana na ndizi hizi ambazo zimekua zikiuzwa kila kona Dar Es Salaam sijajua mikoa mingine kama zipo.Ndizi hizi ni aina ya Malindi ni kubwa nene na zina rangi nzuri ya kuvutia.
Nb:Sipo hapa kuharibu biashara za watu bali kutoa tahadhari kwa walaji wa ndizi hizo wanaokula wakiamini wanaimarisha afya kumbe wanaziharibu kwa kula kemikali.

View attachment 1753161

View attachment 1753162
Kwa hiyo fomarin wanaenject kila ndizi au application yake ikoje? Kuivisha Kwa kontena naweza kubaliana na wewe Kwa sababu maeneo niliokulia nilikuwa naona linachimbwa shimo la mstatiri, then Kwa juu linafunikwa Kwa kutumia majani na undongo, ndizi zinawekwa alafu unawasha Moto humo shimoni na baadae shimo linafunikwa pamoja na ule Moshi. Baada ya siku tatu ndizi zimeiva zinapelekwa sokoni
 
Ndizi zinaivishwa kwa kutumia container yenye uwezo kupoza na kuongeza joto kitaalamu inaitwa reefer container, na sio kila mtu anaweza kuivisha hizo ndizi. Ni vijana wachache waliopata utaalamu ndio hujishughulisha na uivishaji. Shughuli yake ni kila siku lazima aangalie temperature inavyopanda na kushuka kama mara 3 na ni kweli siku 4 zinakuwa zimeiva. Hakuna dawa inayotumika zaidi ya kupaka majibu kwenye vikonyo vya ndizi ili kuondoa utomvu.
 
mbona hili jipya mkuu,hivi unajua thamani ya dozi moja tu ya dawa za kukaushia maiti?

maana ungejua thamani yake bas ndiz moka ingeuzwa elf 2 kwa kipande
Watanzania wengi hawatumii common sense , afadhali umedadavua vizuri kwa jamii.
 
Ndizi kuivishwa kwenye kontena hii ipo, hata huku mtaani ipo sehemu hiyo, ila kuoigwa dawa ya kuhifadhia maiti, hilo sina ushuhuda nalo, japo akili yangu inaniambia ni stori ya kijiweni tu.
 
Ndizi zinakatwa vichane, kichane kinadumbukizwa kwenye maji, then kinapakiwa kwenye sanduku la mbao, yaan kreti, then linawekwa ndani ya kontena.
 
Back
Top Bottom