Ndege ya tatu aina ya Bombardier Kuwasili nchini Mwezi huu

Mkuu hicho alichosema waziri mkuu wa Singapore ndio mada yangu ijayo. Yaani nina wazo hilo hilo. Kwa Bongo hakuna cha kutufaa zaidi ya kilimo. Tutapata chakula na hakuna zao la shamba lisilouzika nje ya nchi.

Nafikiria tujenge viwanda vya kufanyia processing mazao ya shamba na kuhifadhi mazao. Tuna water bodies nyingi. Tusitegemee mvua. Tufanye irrigation hasa hii ya water dripping. Tulime mahindi watu wale ugali na mwingine tuuze nje.

Ila ishu zinakuja serikali haziwi na mashamba. Ila ni kawaida serikali kuwa na mashirika ya ndege. Hapo pakinyooka nani wa kusimamia mashamba bila ya kurudi kwenye vijiji vya ujamaa wala kuwapa ardhi makaburu mimi naona kilimo ndio mkombozi wetu.

Bombardier sio kosa hata hivyo . Tutakuwa nchi gani hatuna ndege? Togo au Burkina Faso? Na usidharau unafikiri Ethiopian airline ni shirika la watalii. Uchumi wa Ethiopia bila ya Ethiopian airline si watakufa njaa tena kama miaka ile?

Kila siku iendayo kwa Mungu Ethiopian airline wanarusha ndege kutoka DC Washington kwenda Addis na mara nyingi inajaa. Kuna wanigeria, waghana na wawest wengine inabidi wapelekwe Addis kabla ya kwenda kwao. Tizama huu mtandao wa ndege unafikiri kwa siku wanaingiza ngapi?
Mbuyu ulianza kama mchicha.

.
a298ff2dd06e7facf84f7f461cad1c8d.jpg
Sijasema kuwa na Bombarder ni kosa... hoja yangu ni kwamba, unavyokuwa na limited resource, unatakiwa ku-invest kule ambako kutatoa higher return ili mapato yake yawe reinvested kwenye maeneo mengine!

Kinyume chake, sioni ni namna gani uwekezaji kwenye ndege unaweza kutoa return ya maana inayoweza kuwekezwa kwenye sekta zingine! Zaidi ya pride, kwamba ikiwa hata Rwanda nchi ndogo wana ndege, kwanini na sisi tusiwe nazo!!! Hiki ndicho kinatuponza badala ya kuangalia commercial and economic viability!

Kampuni nyingi za ndege Afrika ni loss making ukiacha kampuni chache sana kama Ethiopia Airline!! Sasa kwanini tuingize mtaji wetu mdogo kwenye risky investment wakati tuna alternatives lukuki?!

Hivi ni raia kutoka nchi gani anayeshindwa kuja Tanzania kwa sababu tu ATCL hawana ndege?! Hivi ni nani dunia hii anashindwa kwenda kutembelea Serengeti National Park kwavile tu ATCL hawana ndege?! Ni lini na wapi over the past 10 years nchi ilisimama shughuli zake kwa sababu tu ATCL hawana ndege?!

Yote hayo kwangu yasingekuwa muhimu endapo tu kungekuwa na possibility ya kutoa high return ambayo itakuwa reinvested! Lakini, sitarajii hiyo high return?!

So, si kwamba hakuna umuhimu moja kwa moja, lakini kwa sasa sioni ulazima huo wakati hizo billioni kadhaa zingeweza kuwekekzwa kwingine na kutoa return kubwa zaidi ambayo pengine ndo ingekuja kununua hizo ndege in the future!!!

Kuhusu Ethiopian Airline, wala usijaribu kujilinganisha nayo!!! Hivi hujiulizi ikiwa throughout Africa kuna mashirika ya ndege lakini kila wakati ni Ethiopia Airline peke yake ndiyo inatolewa mfano?! Ukiacha Ethiopia Airline labda na South African Airways pamoja na Egypt Air na kwa mbali inafuata Kenya Airways!

Ni shirika lipi kati ya hayo ambayo ATCL wanaweza ku-compete nao? Kwanini tusikusanye kwanza nguvu ili tuingie wakati tupo full prepared?!
 
Ha ha ha ha ha, kajipange upya. Uongo sio kitu kizuri, eti ku-connect dots. "Dots" gani? Hizo dots labda umeziconnect wewe hadi unaishia kuzunguka zunguka.
Turahisishe kazi sasa! Hebu taja sababu kubwa iliyowafanya Ethiopia kuwekeza kwenye airline business ambayo inaendana na huu uwekezaji wenu!!!!
 
Turahisishe kazi sasa! Hebu taja sababu kubwa iliyowafanya Ethiopia kuwekeza kwenye airline business ambayo inaendana na huu uwekezaji wenu!!!!
Sema wewe na uongo wako. Sababu zimeshaelezwa kwenye makala lakini wewe unataka kujifanya unajua zaidi.
 
Halafu ni upuzi kusema Ethiopia hawana ardhi ya kulima. Abysinia highlands wanakolima kahawa ni wapi?
Ethiopia hawana ardhi ya kulima au Ethiopia hawana ardhi mzuri?! Niliosema hawana ardhi ya kulima ni Singapore, soma kwa vituo!! Na hilo suala la kuwepo terrain kama moja ya motivational factor za kuanzisha shirika la ndege nimeweka source yake hapa!!!
 
Yanini mtu aseme Ethiopia wana shida ya ardhi ya kulima wakati kahawa yao inauzwa Marekani bila ya kificho?
5fc60ec54f98dbd79ffde068b7ed533a.jpg
 
Naona ya Ethiopia na Colombia. Tanzania ndio siioni. Shauri ya ngebe na talalila nyingi.
 
Basi ngoja nikupuuze! It's very funny kwamba ulidhani Ethiopia walikurupuka tu kuwekeza kwenye ndege kama alivyofanya JPM na ndio maana umeshindwa kutaja... in short, hujui!!!!

Sasa alichokurupuka JPM ni nini?
 
Sasa alichokurupuka JPM ni nini?
Narudia, defend economic na commercial viability ya hizo ndege! Kukurupuka ndo huku kwa kuwekeza billions kwenye investment ambayo impact yake ni ndogo kwa sababu tu ameona Rwanda taifa dogo lina ndege!!!! Na kimsingi, ndio hoja yako wewe hiyo; kwamba ni taifa gani lisilokuwa na ndege!!! National Pride vs National Economy!
 
Lazima ufanye hivyo kwa sababu huwezi kujinasua toka kwenye uongo wako. Mara nyingine kuwa makini na unalosema. Umenisikia?
Narudia, taja hizo sababu na kama hujui piga kimya au endelea kupigia makofi kila jambo hata kama ni la kijinga!!
 
Narudia, defend economic na commercial viability ya hizo ndege! Kukurupuka ndo huku kwa kuwekeza billions kwenye investment ambayo impact yake ni ndogo kwa sababu tu ameona Rwanda taifa dogo lina ndege!!!! Na kimsingi, ndio hoja yako wewe hiyo; kwamba ni taifa gani lisilokuwa na ndege!!! National Pride vs National Economy!

Hivi wewe una biashara yeyote unafanya? Usicheze na transportation industry. Kuna siku nilipanda boti ya Bakhresa kwenda Zanzibar nikapiga hesabu haraka haraka zile boti zinaingiza ngapi nikaishia kupata kizunguzungu.

Face it, mnaompinga Magufuli kufufua shirika la ndege mnapinga kwa upinzani tu hamna pointi yeyote ya maana.
 
Back
Top Bottom