Ndege ivutwe na wananchi utegemee watu kupona?

Jul 22, 2019
10
27
Kwa taarifa zilizoonekana wazi, wananchi ndio walikuwa mstari wa mbele kwenye uokoaji wa ndege pale Bukoba hasa kwenye hatua za mwanzo za uokoaji hawa ni watu wa kupongezwa sana.

Mara kadhaa kumekuwa na majaribio ya kujiandaa na dharura viwanja vya ndege natumaini mengi wanajifunza, matukio mbali mbali yanayotokea nchini yanatosha pia kuleta changamoto na mafundisho ya kukabili changamoto za usoni.

Kwa hali ilivyokuwa kwenye ajali, uokoaji wa kisasa ulihitajika sana ili kuwapa msaada abiria waliokuwemo kwenye ndege hiyo. kuvuta kamba hakuwezi kufanikisha uokozi wa abiria kwa asilimia kubwa.

Ashukuriwe Mungu watu 26 wameokolewa, poleni sana waliopatwa na msiba kutokana na raia wengine 19 kufariki wakiwa ni abiria na rubani katika ajali hiyo.

Ifike mahali kama nchi, tuweke jitihada kwenye miundombinu ya tahadhari na dharura ili kukabili matatizo ya ajali za vyombo vya moto na moto wenyewe.
 
Kwa taarifa zilizoonekana wazi, wananchi ndio walikuwa mstari wa mbele kwenye uokoaji wa ndege pale Bukoba hasa kwenye hatua za mwanzo za uokoaji hawa ni watu wa kupongezwa sana.

Mara kadhaa kumekuwa na majaribio ya kujiandaa na dharura viwanja vya ndege natumaini mengi wanajifunza, matukio mbali mbali yanayotokea nchini yanatosha pia kuleta changamoto na mafundisho ya kukabili changamoto za usoni.

Kwa hali ilivyokuwa kwenye ajali, uokoaji wa kisasa ulihitajika sana ili kuwapa msaada abiria waliokuwemo kwenye ndege hiyo. kuvuta kamba hakuwezi kufanikisha uokozi wa abiria kwa asilimia kubwa.

Ashukuriwe Mungu watu 26 wameokolewa, poleni sana waliopatwa na msiba kutokana na raia wengine 19 kufariki wakiwa ni abiria na rubani katika ajali hiyo.

Ifike mahali kama nchi, tuweke jitihada kwenye miundombinu ya tahadhari na dharura ili kukabili matatizo ya ajali za vyombo vya moto na moto wenyewe.
Wavuvi walikua wanavuta ile ndege kama kokoro. Itoshe kusema kwamba sijui tija ya kuivuta ilikua ninini, kuiokoa dubwasha lile lisitumbukie ama ninini

Sent from my LM-Q730 using JamiiForums mobile app
 
Ndege ya kurusha matokeo ya sensa ipo ila ya kuokoa watu wanapopata maafa unajibiwa haina mafuta hii nchi imeoza sana kina mpaka na nape wanachezea hela tu halafu mambo madogo kama haya wanashindwa kutatua
 
Kwa taarifa zilizoonekana wazi, wananchi ndio walikuwa mstari wa mbele kwenye uokoaji wa ndege pale Bukoba hasa kwenye hatua za mwanzo za uokoaji hawa ni watu wa kupongezwa sana.

Mara kadhaa kumekuwa na majaribio ya kujiandaa na dharura viwanja vya ndege natumaini mengi wanajifunza, matukio mbali mbali yanayotokea nchini yanatosha pia kuleta changamoto na mafundisho ya kukabili changamoto za usoni.

Kwa hali ilivyokuwa kwenye ajali, uokoaji wa kisasa ulihitajika sana ili kuwapa msaada abiria waliokuwemo kwenye ndege hiyo. kuvuta kamba hakuwezi kufanikisha uokozi wa abiria kwa asilimia kubwa.

Ashukuriwe Mungu watu 26 wameokolewa, poleni sana waliopatwa na msiba kutokana na raia wengine 19 kufariki wakiwa ni abiria na rubani katika ajali hiyo.

Ifike mahali kama nchi, tuweke jitihada kwenye miundombinu ya tahadhari na dharura ili kukabili matatizo ya ajali za vyombo vya moto na moto wenyewe.
Ifike mahali lini?kila ajali itokeapo nchi hii hakuna la kujufunza,mapungufu ni yale yale tu,kama ajali inatokea mita chache tu kutoka uwanja wa ndege,ambapo kuna kituo cha jeshi la zima moto hali ndio hiyo,je ingekuwa ni kilomita hata mbili kutoka ufukweni?cha Kumshukuru mungu ni kuwa ndege haikuzama yote kutokana na kina cha maji cha eneo husika.Tofauti na hapo yangekuww mengine.Kwenye yale mafunzo yao ya utayari utafikiria kweli kuna watu!!!Mimi nilishasema siku nyingi hii nchi ni Mungu tu ndio atulinde kwa ulinzi wake wa haya majanga,lakini kutegemea hawa watu.Leo kuna abiria mmoja baada ya kuokolewa kutoka ndani ya ndege,anafika nje anakutana na mtumbwi wa kasia!!!ndio anaingizwa humo,akasema jamani vipi,hiki nacho c kitazama??alitegemea kukutana na kitu kama FAIBA,lakini kimesaidia!!mita chache tu hapo kuna kambi ya wana maji pale kastam bk,Utasikia tu ni MAPENZI YA MUNGU.
 
Hivi ilishindikana kabisa kutafuta ile caterpillar yenye nguvu, halafu hiyo ndege ikafungwa mnyororo na kuvutwa ndani ya dakika chache tu mpaka ufukweni!
Mkuu hayo mambo yanawezekana kwenye nchi ambazo,vitengo vyote viko active muda wote,na wanaofanya kazi hizo wanaelewa nini cha kufanya endapo hiki kitatokea.Pale uwanja wa ndege Bk una gari kubwa la kuzima moto muda wote huwa liko pale,lisingeweza kutumika kuvuta hiyo ndege pindi tu ajali imetokea??ukilinganisha na nguvu za binadamu?Nasikia ,nyaya/kamba za kuvutia ilikuwa tatizo!!
 
Kwa taarifa zilizoonekana wazi, wananchi ndio walikuwa mstari wa mbele kwenye uokoaji wa ndege pale Bukoba hasa kwenye hatua za mwanzo za uokoaji hawa ni watu wa kupongezwa sana.

Mara kadhaa kumekuwa na majaribio ya kujiandaa na dharura viwanja vya ndege natumaini mengi wanajifunza, matukio mbali mbali yanayotokea nchini yanatosha pia kuleta changamoto na mafundisho ya kukabili changamoto za usoni.

Kwa hali ilivyokuwa kwenye ajali, uokoaji wa kisasa ulihitajika sana ili kuwapa msaada abiria waliokuwemo kwenye ndege hiyo. kuvuta kamba hakuwezi kufanikisha uokozi wa abiria kwa asilimia kubwa.

Ashukuriwe Mungu watu 26 wameokolewa, poleni sana waliopatwa na msiba kutokana na raia wengine 19 kufariki wakiwa ni abiria na rubani katika ajali hiyo.

Ifike mahali kama nchi, tuweke jitihada kwenye miundombinu ya tahadhari na dharura ili kukabili matatizo ya ajali za vyombo vya moto na moto wenyewe.
Ni aibu tosha
 
Back
Top Bottom